Hili la Ngorongoro halijaisha, tumefunika kombe

Kwani kuna wamasai crater?? Hata siku moja hutakaa umkute masai crater., crater kule shimoni wanaishi wanyama tuu. Wamasai wanaishi juu. Na wamasai wanalinda wanyama na hawawaui. Wamasai sio majangili
Tunapoongea crater tunamaanisha eneo lote lililo chini ya NCA (mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro).

Hata mimi nimefika Ngorongoro na nimeingia kwenye crater na najuwa ninachoongea
 
Je wakileta Wazungu utakuwa nanmsimamo sawa?

..kuna ujenzi unaofanyika ktk mbuga na hifadhi zetu ambao ni kinyume malengo ya uhifadhi.

..mgogoro kuhusu suala hilo ulikuwepo tangu wakati wa utawala wa Rais Mwinyi. Wakati huo hata hatujaingia ktk mfumo wa vyama vingi.

..Mh.Patrick Qorro mbunge wa Karatu wakati huo aliwasilisha hoja binafsi kupinga hujuma dhidi ya uhifadhi zilizoanza kuibuka wakati huo.

..mimi nampinga yeyote anayehatarisha uhai wa mbuga na hifadhi zetu za wanyama.
 
Utalii wa watu asili ni utalii mpya tuelekee huko ona aborigines etc.
 
Haya ni maoni yangu mimi, kwamba;

1. Wamasai hawana shida iwapo watashirikishwa kikamilifu ktk uhifadhi wa ikolojia ya Ngorongoro na huko kwingine....

2. Shida iko serikalini hususani kwa Rais Samia Suluhu Hassan mwenyewe na wenzake huko CCM. Kwa sababu sababu za kuwahamisha wamasai ni za kinafiki, uongo na ulaghai mtupu. Wamasai wameliona hili na wakasema, HAIWEZEKANI........!!

3. Sababu hizi za kinafiki toka serikalini zinajengwa ktk msingi kwamba "wamasai wamezidi sana Ngorongoro na hivyo kuathiri ikolojia ya eneo hilo muhimu kwa utalii hivyo waondoke ili kuruhusu wanyama na uoto wa asili kushamiri tena". Lakini ukweli ukiwa ni kuwa "fukuza wamasai kisha karibisha wanaoitwa wawekezaji waendeleze eneo hilo la Ngorongoro kwa kujenga mahotel nk". Hili wamasai wameliona na ndiyo maana ya upinzani huu mkali unaoendelea huko......

4. Kwa sababu hizI za kinafiki na ulaghai mtupu zinazotolewa na serikali, usitegemee kuwa kuna mmasai mwingine ataondoka/atahama tena eneo hilo kwenda popote unless otherwise itumike nguvu ya kumwaga damu za watu hapo.......!!

5. Kama tunataka kuthibitisha kuwa mradi huu wa kuhamisha wamasai umejengwa ktk msingi wa sababu za uongo, kinafiki na ulaghai huku ukiwa na dalili ya 100% kuwa, kuna mataifa ya nje hususani ya uarabuni yamewahonga viongozi wetu (akiwemo Rais) ili kulitoa eneo hilo kwa mwekezaji huyo mhongaji wa viongozi wetu kwa sharti la kuwaondoa wenyeji wote wa eneo hilo (wamasai), tujiulize tu nani anagharamia gharama za uhamishaji huo wa wamasai kwenda Msomera Tanga (zaidi 550km) toka Ngorongoro? Kama ni serikali, bunge liliridhia mpango huo? Bajeti kiasi gani ilipitishwa na bunge kugharamia project hiyo? Lini na wapi?

6. Kama tunataka wamasai wahame Ngorongoro kwa hiari yao; Mosi, serikali iache uongo, unafiki na ulaghai kwa jamii hii. Pili, jamii yote ya kimasai wanaoishi ishirikishwe kwa uwazi kwa kutoa elimu ya kwanini ni muhimu wapungue Ngorongoro. Tatu, pendekezo lako kuwa wachaguliwe wamasai baadhi tu hususani Malaighwani, ni hapana. Hii ndicho kilicholeta shida hata mzozo kufikia hatua hii ya kuelekea umwagaji damu. Kwenye hili kila mmasai anayeishi Ngorongoro mume, mke,kijana na wazee washiriki ktk kufanya maamuzi. Kwa kuwashirikisha hawa wanaoitwa "baadhi ya wawakilishi tu", hapana kwa sababu kwa hii serikali ya kifisadi inaweza kuwahonga hao wachache ili mradi wakubaliane na matakwa ya serikali na kuipa uhalali wa kuwafanya chochote wamasai wote halafu ikitoka hapo watambe kuwa wamasai wamekubalI lakini mwisho wa siku mgogoro unarudi palepale na pengine kuwa mbaya zaidi.....

7. Zoezi hili lifanyike kwa wamasai wenyewe wote kuulizwa wanataka wasogezwe wapi. Kwa maoni yangu, Msomera Tanga ni ardhi nyingine kabisa huko yenye mazingira tofauti na waliyozoea wao. Kama lengo ni kuwatoa tu kwenye hifadhi ya Ngorongoro, ni kwanini basi wasitafutiwe maeneo ndani ya mikoa hii hii ya Arusha au Manyara ambayo ndiyo mazingora yao ya siku zote? Mbona kuna maeneo makubwa tu ktk mikoa hii hata kama baadhi wataingia mikoa ya karibu ya Dodoma na Singida......?

8. Na wakiondoka, kamwe ardhi yao asipewe mtu mwingine hususani mwaarabu kama alivyofanya Hayati Rais Ally Hassan Mwinyi kule Loliondo kwa kuwafukuza wamasai na kuwapa Waarabu. Ni kweli ardhi ibaki kuwa hifadhi kwa ajili ya uoto wa asili na wanyama tu na kwa ajili ya shughuli za utalii kwelikweli......!
 
Je umewahi kufanya tafiti ni wanyama kiasi gani wamepungua baada ya hayo mahoteli kujengwa mbugani?

Pili umewahi kutafiti ni revenue kiasi gani imeongezeka baada ya mahoteli hayo kujengwa??
 
Je umewahi kufanya tafiti ni wanyama kiasi gani wamepungua baada ya hayo mahoteli kujengwa mbugani?

Pili umewahi kutafiti ni revenue kiasi gani imeongezeka baada ya mahoteli hayo kujengwa??

..hilo ni jambo ambalo halihitaji utafiti kwamba mahoteli hawapaswi kujengwa ktk maeneo ambayo yamehifadhiwa na ni mapito ya wanyama.

..kuna maeneo mbadala yanayofaa kujenga mahoteli na hivyo kuongeza mapato yetu ya utalii.

..jambo lingine ni maamuzi ya Rais Samia kuchimba madini ktk mbuga ya Serengeti. Maamuzi hayo yanaonyesha kuwa Samia ni kiongozi asiye na nia ya dhati ya kulinda mbuga zetu.
 
Ukipata muda tafuta idadi ya Mohoteli na Campsites zilizopo Maasai Mara ambayo ni extension ya Serengeti iliyopo upande wa Kenya, halafu linganisha na idadi ya hoteli zilizoko Tanzania (Serengeti). Huku ukizingatia kuwa 3/4 ya pori ni Serengeti wakati 1/4 ndiyo Maasai Mara.

Baada ya hapo urudi hapa na majibu
 

..hatupaswi kuiga UHARIBIFU uliofanyika Maasai Mara kwa kujenga mahoteli mengi ktk hifadhi bila mpango.
 
Jibu ni rahisi.
Hakuna tatizo linalo fumbuliwa kwa "kufunika kombe."
Lakini baada ya kusema hivyo, ni vema pia niseme kuwa mfumbuzi wa tatizo wa uhakika hawezi kuwa mtu/kiongozi huyo huyo anaye funika kombe.

Umeeleza vyema sana kuhusu mkasa ule wa vikongwe. Katika maelezo yako umejaribu kufananisha; lakini mimi nasema hakuna mfanano wa karibu vile.
Hili swala la Ngorongoro, pamoja na kuwa na ukweli kuhusu mazingira ya eneo hilo; lakini pia swala hilo linaingiliwa na maslahi ya kufaidika baadhi ya watu/viongozi kutokana na uwekezaji katika eneo lenyewe, baada ya wamasai kupisha..

Mwalimu Nyerere hakuwa na maslahi katika swala la vikongwe kuuawa, mbali ya wananchi wake kupoteza uhai. Hii leo kwa Ngorongoro, Rais Samia, ambaye anapoza tu moto, kwa kulazimishwa; anahusika na analijua swala hilo katika hatua zote tokea mwanzo na katoa/kashiriki katika maamuzi ya kuwaondoa wamasai katika eneo hilo.

Kwa hiyo, niseme tu mwisho, kwamba, hapa Rais Samia hawezi kuwa mtatuzi wa kweli wa swala hili. Itabidi tuombe sana apatikane kiongozi mwenye dhati ya kweli ya kulitatua tatizo hilo kwa maslahi ya nchi nzima.
 
..hatupaswi kuiga UHARIBIFU uliofanyika Maasai Mara kwa kujenga mahoteli mengi ktk hifadhi bila mpango.
Siyo uharibifu bali ni ushindani wa kibiashara. Na hao wenye mahoteli Masai Mara ndiyo wanawalipa local NGOs na Wanaharakati uchwara kama akina Maria Sarungi ili wapinge hatua zozote za Tanzania kuongeza mahoteli.

Kwa sasa watalii wanapokuja kwenye peak season especially kushuhudia World biggest wildebeest migration, wanalala hoteli za Kenya na kuja Mto Mara kushuhudia na kupiga picha kisha wanarudi Kenya.

Tanzania haipati a right share of tourism revenue due to this landscape
 
Shida nyingine ni kuwaondoa masai na kumuuzia mwarabu ajenge hotels kama ni kulinda mazingira basi wakitolewa maasai wabaki wanyama tu
 
Waarabu pia watoke
 

..mahoteli yajengwe mengi, lakini sio kwa kuhujumu na kuharibu ikolojia na uhifadhi wa mbuga zetu.

..kwa mfano, sasa hivi Mama Samia ameamua kuchimba madini ktk mbuga ya Serengeti. Je, tuwalaumu Wakenya kwa maamuzi hayo ya Mama Samia? Je, anatumika?
 
Kwani walioweka utawaratibu wa mchanganyiko mwanzo walikosea nini? Haya na sehemu zingine zilizopewa Waarabu nako kuna nini? Hii si biashara ya kujali biashara kuliko ubinadamu?
 
Wazo lako ni zuri, tatizo viongozi tulionao sio, ukiwaambia waongee na viongozi wa wamaasai wao watatanguliza bahasha kuwalainisha hao viongozi bila kujua huenda wakauchochea zaidi mgogoro, mmaasai siyo mzaramo. Wasuruhishi toka ulaya wataweza kufanikisha kwani hawatakua na maslahi upande wowote na wanaaminika zaidi kuliko hawa aina ya akina Nape na Makonda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…