Hili ndilo pambano la Millenium

Hili ndilo pambano la Millenium

Hance Mtanashati

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2016
Posts
20,137
Reaction score
26,189
Baada ya kushuhudia mpambano wa kukata na shoka kati ya undefeated world champion Floyd Joy Maweather na Conor Anthony MacGregor ,hatimaye macho yote kwa wapenda boxing wote duniani tutayaelekeza katika viwanja vya T mobile arena Las Vegas.

Pambano hilo ambalo kwa namna moja au nyingine linatazamiwa kuwa pambano la kuvutia zaidi na litakalodumu kwenye vichwa vya watu na kuweka historia kwenye mchezo huu wa boxing litawakutanisha bondia asiye pigika Gennedy Gennadyevich Golovkin na Saul Santos Alvarez (Canelo)


GGG amepambana jumla ya mapambano 37 ameshinda yote , hajawahi kutoa sare wala kupigwa mapambano 33 ameshinda kwa K.O manne ameshinda ushindi wa kawaida.


Kwa upande was Canelo Alvarez yeye amepambana mapambano 51 ,ameshinda 49 ,34 ameshinda kwa knockout,ametoka sare pambano moja na Jorge Juarez mwaka 2006 pia amepigwa moja na Floyd Mayweather katika viwanja vya MGM Grand Arena mwaka 2013 .

Canelo pia alimtandika kwa knockout Kali sana bondia Amir Khan mwaka jana round ya sita .


Sasa je Canelo anaweza kuandika historia mpya kwenye mchezo was boxing kwa kumtandika Gennady Gennadyevich Golovkin(GGG)?

Jibu la kitendawili chetu tutakipata mnamo tarehe 16 September 2017 katika kiwanja cha T mobile Arena.


Screenshot_2017-09-02-00-12-04.jpg



Screenshot_2017-09-02-09-42-33.jpg
 
Hili ndiyo pambano asilia na kali sana la ngumi. Hapa ndiyo mkono halisi utaonekana. Achana na kelele za wale waingereza na wamarekani.
Mkuu hapa umerusha dongo kwa Floyd nini?[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
halafu huyu ggg kwanini wasingempambanisha na mayweather mbona kizazi hichihichi, mbona kanelo alipigana na mayweather, kuna kila dalili mayweather alikuwa anakwepa baadhi ya mabondia wazuri kama huyu
GGG ni mdogo sana kwa Mayweather.

Ricky Hotton alipanda ulingoni akiwa na rekodi ya kupambana mapambano 43 bila kupigwa wala kutoa sare lakini alipopambana na Floyd Mayweather alitandikwa knockout round ya kumi.


Hata Canelo naye alikuwa na rekodi ya kupambana mapambano 43 kashinda 42 katoa sare moja lakini alipokea kipondo kitakatifu kana kwamba hakuwahi kucheza ngumi hata siku moja.
 
huyo Canelo alimtoa jasho Mayweather na ushindi ulikuwa wa utata kwann wasirudie mpambano wa Canelo Vs Mayweather

G.O.M.D
 
Back
Top Bottom