Hili ni Swali Muhimu Kuhusu "Kufungua Nchi"

Hili ni Swali Muhimu Kuhusu "Kufungua Nchi"

Kalamu

Platinum Member
Joined
Nov 26, 2006
Posts
12,096
Reaction score
15,393
Imenilazimu nilete mada fupi hapa, kuhusu hili swali ambalo limenitatiza, tokea nilipoona limeandikwa magazetini.

Mimi siyo mtaalam wa haya mambo, kwa hiyo nategemea kupata mchango mahsusi toka kwa walio na upeo juu ya mambo haya.

Nchi jirani imepata matatizo ya kupungukiwa na pesa ya kigeni, (U.S. Dollar). Habari zinasema kuna baadhi ya wahitaji wa pesa hiyo imewabidi waje huku kwetu kutafuta pesa ili wakidhi mahitaji yao.

Sasa ninajiuliza, itakuwaje hilo? Hii biashara ya pesa ya kigeni inawezekana ikafanyika holela huko mitaani, na hata kuruhusu biashara hiyo nje ya mipaka?

Je, hili nalo linaweza likawa ni sehemu ya "Kuifungua Nchi"?

Ngoja nisiendelee zaidi ya hapa na kuwachosha wasomaji wa mada.
 
Ni nchi gani hiyo imepungukiwa $ na vipi uhitaji wa sarafu ya hiyo nchi hapa kwetu Tanzania
 
Ni nchi gani hiyo imepungukiwa $ na vipi uhitaji wa sarafu ya hiyo nchi hapa kwetu Tanzania
Jaribu kunielewa. Sarafu pungufu siyo ya hapa kwetu wala sarafu ya nchi hiyo jirani (Kenya).

Upungufu mkubwa ni pesa ya kigeni (dollar ya Kimarekani) ndiyo pungufu kwenye nchi hiyo.

Sasa inadaiwa kwamba imelazimu wafanya biashara ya huko wahangaike kutafuta hiyo hela ya kimataifa ili waweze kufanikisha shughuli zao.
Baadhi yao wamekuja kuitafuta hiyo pesa huku kwetu.

Sasa swali linaanzia hapo. Sisi kuwa chanzo chao cha pesa za kigeni.
 
Nijuavyo hizi dollar za kimarekani huwa zinanunuliwa na kuuzwa, wapo wanaonunua na kuziweka ndani, bei ikipanda wanaziuza wapate faida, nadhani hili ndilo linalofanywa na hao wafanyabiashara toka Kenya.

Tatizo naloliona hapa kwetu, naamini hali ya individuals kumiliki hizo dollar za kimarekani ilipungua sana, hasa kwasababu ya yale yaliyotokea awamu iliyopita, maduka ya kubadili hizo fedha mengi yalifungwa, na waliokuwa wafanyabiashara kuachwa kwenye hali mbaya kiuchumi, siku hizi hiyo biashara inafanywa na mabenki tu.

Labda hao wakenya waende kununulia kwenye mabenki, au kwa baadhi ya individuals ambao walifanikiwa kuzificha wakati wa awamu ya tano.
 
Nijuavyo hizi dollar za kimarekani huwa zinanunuliwa na kuuzwa, wapo wanaonunua na kuziweka ndani, bei ikipanda wanaziuza wapate faida, nadhani hili ndilo linalofanywa na hao wafanyabiashara toka Kenya.

Tatizo naloliona hapa kwetu, naamini hali ya individuals kumiliki hizo dollar za kimarekani ilipungua sana, hasa kwasababu ya yale yaliyotokea awamu iliyopita, maduka ya kubadili hizo fedha mengi yalifungwa, na waliokuwa wafanyabiashara kuachwa kwenye hali mbaya kiuchumi, siku hizi hiyo biashara inafanywa na mabenki tu.

Labda hao wakenya waende kununulia kwenye mabenki, au kwa baadhi ya individuals ambao walifanikiwa kuzificha wakati wa awamu ya tano.
Kitendo hiki kina athari zipi kiuchumi hasa ukiangalia shilingi ya Kenya ina thamani kubwa kuliko ya Tanzania?
 
Ni nchi gani hiyo imepungukiwa $ na vipi uhitaji wa sarafu ya hiyo nchi hapa kwetu Tanzania
Kwamba Tanzania tunaakiba kubwa ya fedha za kigeni kiasi tunawazima wafanyabiashara wa nje?
 
Back
Top Bottom