I'm so fu*ck upset, this world is about to end and Jesus doesn't arrived yet/
I choose to be an atheist, so if you judge you won't be the first....
Vipi kama imani ni kizuizi imewekwa ili tushindwe kuhoji, unahangaika kufunga na kusali usiku kucha huku wanaojua ukweli wame mbonji/
Ulichokiona sio muujiza, nyuma ya pazia ni njama iliyowekwa ili kukukandamiza/
Hawataki uifikie hiyo siri ndomana wameifichwa ndani ya kiza, Joho la mhubiri limeficha mengi yanayotendeka wakati wa misa/
Wanafanya maigizo kukuteka kiakili wakuibie senti uliyoidunduliza, hawana huruma hawajali kua umechoka wao wanazidi kukukimbiza/
Kwanini ukubali kudhurumika, jiulize tumia akili waweza salimika/
Kama tunafundishwa kua yuko kila Kona, Iweje tunakufa kwa corona/
Tumepewa uhuru wa kuchagua lakini hatuna uhuru wa kupona, nini lengo la kumpa tv kipofu wakati unajua hawezi kuona/
Vipi kama hayupo na tumefundishwa uongo, au sala zetu zinapuuzwa kwasababu katupa kisogo/
Vipi kama wanalijua hilo ila wameamua kutumia dini kama mchongo, wao wale na kusaza masikini akisugua magoti madhabahuni akisubiri makombo/
Haiingii akilini napitia msoto na kutaabika, wakati dini imenifunza kulia na kushoto nina walinzi ambao ni malaika/
Kwanini kila dini inahubiri kua ni ya kweli, wakati matamanio yao juu yetu ni kututapeli/
Kwa nini wanatufundisha somo ambalo wenyewe wamefeli, kama tajiri ni ngumu kuiona pepo Why pasta anapush benz waumini baiskeli/
Scars sioni sababu ya kuabudu, sioni sababu ya kulala njaa kwa kuikana kibudu/
Kusudi la dini ni nini,,,kama watu bado wanapata tabu, Tunajizuia kuzini,,,lakini ndoa zinatuweka sub/
Sioni sababu ya kuikacha tamaduni na kuikumbatia misaafu, siwezi kumkataa mwanamalundi na kumkubali mtoto wa yosefu/
Hivi ni kweli yesu anaponya, kwanini sadaka zetu zinatumika kujenga hospitali ili kutibu wagonjwa/
Hivi ni kweli vipofu wakiombewa wanapona, mbona wachungaji wanavaa miwani ya macho ili waweze kusoma/
Mambo ni mengi yanatendeka kanisani mengine naogopa kuyasema, nilipoumwa kidole niliombewa na mchungaji mwenye kilema/
Ni ngumu kuamini kama uwepo wa rasi mwenye kipara, au fundi selemala kwenye jangwa la sahara/
Inaniwia vigumu kuamini tumekombolewa kwa kafara, wakati mtaani watu wazima na watoto wanasota kwa ufukara/
Kama tunachofunzwa hakiendani na uhalisia basi dini ni biashara, kuendelea kuwatukuza wakati tunakandamizwa huo ni ufala/
It's Scars