Hisa ni nini?

Mfano crdb wametangaza hisa zao je nikinunua nafaidikaje nazooo?
 
Mfano crdb wametangaza hisa zao je nikinunua nafaidikaje nazooo?

CRDB waliuza hisa zao kwa mara ya kwanza miaka kadhaa imepita (IPO)

Na zimekuwa zikiuzwa ktk soko la hisa la Dar es salaam.

Wanachofanya saiv ni kuongeza mtaji tena, hivyo wanauza tena kwa mara ya pili ,lakin safari hii hawauzi kwa watu wote wanauza tu kwa wanahisa ambao tayari wana hisa za CRDB (inaitwa Right issue au Hisa stahili)

So kama unataka hisa za crdb au kampuni yeyete iliyopo ktk soko la hisa la Dar es salaam inabd ununue kupitia madalali (brokers) wa soko hilo ambao ni makampuni 8 yaliyosajiliwa na DSE na kusimamiwa na CMSA (capital market and securities authority)

Faida za kumiliki hisa.

1.Gawio: Kampuni zinafanya biashara, mfn hyo CRDB faida yake itakayo ingiza kwa mwaka,kuna ambayo itagawiwa kwa kila mwanahisa kutokana na hisa anazomiliki

2.Kuongezeka kwa thaman ya uwekezaji : hela utayonunulia leo hisa za CRDB si hela utakayo uza mwakan au hata baada ya miaka mitano tuseme, kwa kadri CRDB itavyozid kufanya vzur katika soko na kuzid kupata faida na kukua kila siku, na hisa zako zitazid kukua kila siku.

Mfano unaweza nunua leo hisa kwa kila kipande kwa sh 300 au 500 lakin baada ya miaka kadhaa ukakuta ile thaman imekuwa maradufu had 5000 au 10000 kwa kila hisa. Kwa kadri kampuni inavyoperform

Angalizo: kampuni inaweza kufanya vibaya pia na kufilisika na ukapoteza pesa zako.

3.Kuwa na haki ya kuhudhuria mikutno na kupiga kura juu ya maamuz ya namna ya kuendesha kampuni.
Kwa mfano huo wa CRDB ni kuwa Utahudhuria mikutano muhim kama ile AGM na kupiga kura au kuamua namna ambavyo kampuni itafanya mambo kadha wa kadhaa kwa mwaka husika.

4.Cheti cha Hisa hutumika kama dhamana ktk mabank na wakopeshaji wengine ktk kuombea mkopo.

5.Hisa zinagawanyika: Tofaut ya uwekezaj wa hisa na uwekezaji wa vitu vingine kama Nyumba au mashamba ni kuwa ukihitaj hela ,kama ni shamba utalazimika kuuza lote au nyumba yote hata kama pesa unayohitaj ni nusu tu ya ile ya investment yako,lakin hisa zinagawika, unaweza uza kias kidogo tu ukapata tu unachohitaj. ukihitaj Tsh million 20 na unanyumba ya million 30 mara nyingi utalazimika kuuza nyumba yote ili upate hyo hela,

Lakin kama ni hisa unazo hizo za million 30 na unahitaji 20M utajiuzia tu hizo hisa za 20M million na ukajibakizia za 10M

6.Uwekezaji wa hisa ni rahis unaweza kuanza na kiwango chochote kile kuanzia Tsh 10,000 had Mabillion.
 
Shukran kwa wadau wote, mwanzisha mada/hoja, wachangia hoja na kuuliza kwa niaba ya wengne

Naomba kufahamu masuala yafuatayo:

Moja, mfano, ikitokea mwenye hisa amefariki, je hisa zake zitarithiwa na mtoto/ndugu yake?

Pili, ukishamiliki hisa ktk kampun fulan, je inakuwa moja kwa moja mpk mwisho wa maisha yako au mpk pale unapoamua kujitoa?

Mwisho, je kampun ikifilisika na kufa, je wanahisa wanafidiwa vp na wkt kampun ipo hoi kiuchumi?

Naomba kuwasilisha wadau
 

Moja: hisa huweza kurithiwa au hata kugawiwa kama mali nyingine yeyote.Cha muhim ni kuwa na share certificate na hizo taarifa za mirath zilizokamilika.

Pili: ukimiliki hisa ni moja kwa moja had ,aidha utakapoamua kuuza hisa zako, au utakapofariki na mtu mwingine kuzirith ni kama mali nyingine zozote zile mfano nyumba ,tifaut yake ni kuwa zenyewe hazionekan kwa macho ila zipp kwenye kikaratasi kinachoitwa hati ya hisa au share certificate.

Tatu: Kampuni ikifilisika au wakati ipo hoi kiuchumi kuna namna nyingi ambazo serikali huwa inafanya ili kulinda maslahi ya wanahisa, na moja kati ya mambo hayo ni kuweka mali zote za hiyo kampuni chini ya mwangalizi au mufilisi ,wakati michakato ya kumaliza kampuni na kuifunga salama inaendelea.

Kwa wamiliki wa hisa hiz za kawaida (ordinary shares) ambazo ndizo zinazouzwa ktk soko la hisa sisi ndo huwa tunakuwa na bahat mbaya kidogo sababu endapo kampuni itafilisika basi, wataanza kulipwa watu wengine mfano, Wanaoidai kampuni mikopo ya muda mrefu mfano banks, Kama kampuni ilikuwa na imetoa bonds ,Na kama kulikuwa na hisa za upendeleo (preffered shares) watalipwa kwanza hao ndipo tuje tulipwe sisi.

Na utaona tunakuwa na hatari zaid, hapo unaweza kupoteza fedha zako ,

Na ndo maana unashauriwa kufanya uchunguz wako vizur kabla haujawekeza ktk kampuni husika, ujue utendaji wa kampuni upoje?, biashara inayofanya je inalipa? Unadhan kampuni husika itakuwa wapi baada ya miaka kadhaa? Siyo ununue hisa tu kwa kushawishiwa au kwa kuangalia kampuni kwa nje
 

Nilianza kuelewa ila mwisho ndo umenivuruga tena!!

Je unavosema unaweza kuuza hisa 500,ukabaki 1500 je hizo 500 utaziuza kwa kiasi gani??? Na anayenunua atapataje faida
 
Nawashukuru wote mliotuelimisha kuhusu swala zima la hisa ila naomba msaada kwa swali langu hili kwamba.....ukiamua kujitoa katika kampuni kuna fidia ambayo inabidi ulipe au ni free at any time kujiondoa?
lakini pia naomba kujua, ukitaka kuuza hisa zako unawezaje kumpata mnunuzi?
Naomba msaada kwa mwenye jibu tafadhali
 
Hizo issue ni kama kamali so kuna kula na kupuswa.. so take care. Design kama una bet niko na 8m nahitaji kuziweka mahali zinizalishie hata kwa one year lakini sio kwenye hisa...any idea nipeleke wapi?
 
Hizo issue ni kama kamali so kuna kula na kupuswa.. so take care. Design kama una bet niko na 8m nahitaji kuziweka mahali zinizalishie hata kwa one year lakini sio kwenye hisa...any idea nipeleke wapi?

Kwanini hutaki kuzipeleka kwenye hisa? Kwani kuna uwekezaji gani ambao haunaga hasara?
 
niko na 8m nahitaji kuziweka mahali zinizalishie hata kwa one year lakini sio kwenye hisa...any idea nipeleke wapi?

Tafuta sehemu yoyote wanapojenga saana nunua kiwanja baada ya mwaka thamani ya hicho kiwanja itakuwa imeongezeka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…