Hisa ni nini?

Hisa ni nini?

Ngwananzengo

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2012
Posts
1,911
Reaction score
1,315
Wengi miongoni mwetu wamekuwa wakitaka kujua HISA ni nini, shauku hii imenifanya nidodose kidogo juu ya hisa kwa faida ya wengi. Kwa tafsiri lahisi HISA NI UMILIKI.

Mtu akisema nina hisa NMB anamaanisha ana miliki NMB. Umiliki huu unajionyesha wazi na bayana wakati wa kufanya maamuzi na kugawana gawio (faida inayopatikana katika kampuni). Mwenye hisa nyingi huwa na sauti au ushawishi mkubwa katika kufanya maamuzi na hupewa gawio kubwa kwa uwiano wa hisa zake.

Mfano- Kampuni yaweza kuwa na hisa 1000, ikaamua kuuza hisa 500 na hisa 500 zikabaki akiba. Wale watakaonunua hizo hisa 500 , wanakuwa wametoa mtaji kwa kampuni na kwa maana hiyo ndio wamiliki. Mwenye kuweza kununua hisa 251 atakuwa amenunua hisa nyingi zaidi kuliko yeyote na anakuwa na nguvu ya maamuzi katika vikao na gawio atapata kubwa kwa sababu ndie aliechangia mtaji mkubwa.

Faida za kuwa na hisa:

1. Unapata fursa ya kuwa mmoja ya wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ama moja kwa moja au kwa kuwakilishwa.
2. Mwanahisa anapofariki shughuli za kampuni haziwezi kuyumba kwa sababu jukumu la kazi za kila siku lipo mikononi mwa menejimenti
3. Ni lahisi zaidi kuuza HISA pindi unapoona hauhitaji kuendelea na umiliki
4. HISA ni dhamana (badala ya kuweka nyumba/shamba ili uweze kukopeshwa na taasisi za fedha waweza kuweka dhamana ya hisa zako)
5. Kampuni inapofanya vizuri sokoni ama kwa kutoa huduma/bidhaa bora au kwa kuwa na mipango mkakati mizuri thamani ya HISA hupanda. Wapo walionunua hisa za NMB tshs 600 lakini leo ni zaidi ya tshs 950.

Kwa maana hiyo mbali ya gawio mtu anaweza kuuza hisa kwa bei inayomlipa akilinganisha na bei ya kununulia.

NAOMBA NIKOMEE HAPA.
 
Ngwananzengo umetoa darasa zuri... Asante. Mie ningependa nijue na upande wa pili wa shillingi. Hasara zake ni zipi?
 
Last edited by a moderator:
lahisi ni rahisi
hisa ni umiliki
hisa 1000 umiliki elfu moja
swali langu kampuni idadi ya hisa za mwanzo/ awali kabla haijapeleka sokoni zinatoka wapi?
 
Yaan mim sielewi kbs yaan hizo Hisa ndo nin HUDUMA,BIDHAA au kitu gan ktk kampun husika?
 
Ngwananzengo umetoa darasa zuri... Asante. Mie ningependa nijue na upande wa pili wa shillingi. Hasara zake ni zipi?
Hasara ni pale unapokuwa na hisa chache kwani unakuwa kama unasindikiza wengine. Gawio unapata dogo na unakuwa huna ushawishi katika maamuzi. Hasara nyingine ni pale kampuni inapofanya vibaya, thamani ya hisa hupungua, waweza nunua hisa 1 kwa tsh 1000 ukauza 500 au hela zako zikazama. Ni vyema kupata ushauri wa kitaalamu kabla ya kununua HISA
 
Wengi miongoni mwetu wamekuwa wakitaka kujua HISA ni nini, shauku hii imenifanya nidodose kidogo juu ya hisa kwa faida ya wengi. Kwa tafsiri lahisi HISA NI UMILIKI.

Mtu akisema nina hisa NMB anamaanisha ana miliki NMB. Umiliki huu unajionyesha wazi na bayana wakati wa kufanya maamuzi na kugawana gawio (faida inayopatikana katika kampuni). Mwenye hisa nyingi huwa na sauti au ushawishi mkubwa katika kufanya maamuzi na hupewa gawio kubwa kwa uwiano wa hisa zake.

Mfano- Kampuni yaweza kuwa na hisa 1000, ikaamua kuuza hisa 500 na hisa 500 zikabaki akiba. Wale watakaonunua hizo hisa 500 , wanakuwa wametoa mtaji kwa kampuni na kwa maana hiyo ndio wamiliki. Mwenye kuweza kununua hisa 251 atakuwa amenunua hisa nyingi zaidi kuliko yeyote na anakuwa na nguvu ya maamuzi katika vikao na gawio atapata kubwa kwa sababu ndie aliechangia mtaji mkubwa.

Faida za kuwa na hisa:

1. Unapata fursa ya kuwa mmoja ya wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ama moja kwa moja au kwa kuwakilishwa.
2. Mwanahisa anapofariki shughuli za kampuni haziwezi kuyumba kwa sababu jukumu la kazi za kila siku lipo mikononi mwa menejimenti
3. Ni lahisi zaidi kuuza HISA pindi unapoona hauhitaji kuendelea na umiliki
4. HISA ni dhamana (badala ya kuweka nyumba/shamba ili uweze kukopeshwa na taasisi za fedha waweza kuweka dhamana ya hisa zako)
5. Kampuni inapofanya vizuri sokoni ama kwa kutoa huduma/bidhaa bora au kwa kuwa na mipango mkakati mizuri thamani ya HISA hupanda. Wapo walionunua hisa za NMB tshs 600 lakini leo ni zaidi ya tshs 950.

Kwa maana hiyo mbali ya gawio mtu anaweza kuuza hisa kwa bei inayomlipa akilinganisha na bei ya kununulia.

NAOMBA NIKOMEE HAPA.

Kuna kitu nataka kufahamu,malipo ya hisa hutolewa kila baada ya kipindi fulani cha wakati au kutegemea na mapato ya kampuni husika,na je kuna mipaka ya chini kabisa ya kiasi cha umiliki wa hisa?
 
lahisi ni rahisi
hisa ni umiliki
hisa 1000 umiliki elfu moja
swali langu kampuni idadi ya hisa za mwanzo/ awali kabla haijapeleka sokoni zinatoka wapi?
Hisa za mwanzo zinaamuliwa na wamiliki. Kampuni ni lazima iwe na watu walioianzisha hawa huweka mipango mikakati. Hubainisha kampuni itajihusisha na nini na umiliki wake utakuwaje. Hapo kwenye umiliki ndipo huamliwa kampuni iwe na hisa ngapi, ngapi ziuzwe na ngapi ziwekwe akiba. Pia huamua hisa za kampuni ziwe na thamani ipi (kwa kuanzia).
 
Hasara ni pale unapokuwa na hisa chache kwani unakuwa kama unasindikiza wengine. Gawio unapata dogo na unakuwa huna ushawishi katika maamuzi. Hasara nyingine ni pale kampuni inapofanya vibaya, thamani ya hisa hupungua, waweza nunua hisa 1 kwa tsh 1000 ukauza 500 au hela zako zikazama. Ni vyema kupata ushauri wa kitaalamu kabla ya kununua HISA

Kwa maneno mengine suala si kuwa na HISA tu, ila ni kuwa na HISA katika kampuni ambayo inafaa ku invest.

Kuna mdau mmoja hapa jamvini kwa ID name ya thinka aliuliza ni kwa nini HISA za CRDB zilishuka thamani. Nilipata darasa toka kwa TUKUTUKU kuwa akisema haya;

Kushuka kwa dhamani ya hisa za CRDB zimesababishwa na kuongezeka kwa hisa zilipelekwa sokoni kwa ajili ya kuuzwa,ukilinganisha na mahitaji halisi ya hisa zinazohitajika sokoni!(Refer to the law of demand and supply in determination of price)!Hili ni zao tu,cha kujiuliza hapa ni kwamba,kwanini watu wengi wamepeleka hisa zao sokoni?
Kulingana na utafiti mdogo nilioufanya (As financial analyst) ni kwamba hivi karibuni CRDB wametoa taarifa zake za fedha kwa robo ya pili ya mwaka,ambazo kwa upande wa faida ,benki imepata faida ya Tshs 20.04 bilioni ukilinganisha na Tshs 16.51 bilioni iliyoipata kwa robo ya mwaka iliyotangulia,hii ni sawa na ongezeko la aslimia 24.Ukija kuangalia suala la mikopo ambayo hailipwi kumekuwa na ongezeko kubwa kutoka Tshs 124.169 bilioni mpaka 139.307 bilioni jambo ambalo si zuri kwa kampuni (Source:CRDB published information for second quarter).

Kwa kuwa wanahisa kwa kushirikiana na financial analysts na brokers, huwa wapo very sensitive na hizi taarifa za kifedha wengi wameshauriwa kuuza hiza zao kwa kuwa benki imeonyesha uzembe mkubwa katika ukusanyaji wa madeni,na hivyo kuhatarisha its going concern(Uwepo wake kwa siku zijazo).

Lugha iliyotumika katika kujibu swali la kushuka kwa hisa, inafanya mtu wa kawaida kuwa mwoga sana wa kununua HISA. Sababu unajiuliza maswali kama 2nd quarter ilikuwa na faida zaidi ya 1st quarter inakuwaje HISA zishuke thamani sababu tu zimeingia sokoni?

Au better yet, ikiwa kampuni imesha amua HISA 500 ndio zitakuwa kwa wale ambao ni wanunua HISA si inatakiwa ziendelee kupanda/kushuka tokana na kupanda/kushuka kwa thamani ya kampuni yenyewe?

Samahani, ni mchanga kabisa katika sekta hii, na hivi nimepata mtu wa kunielewesha naona nibanane nawewe unipe darasa.


CC: Wakuu TUKUTUKU, Bulesi, burden, Madewa, Prisoner 46664, KIBANGA Ampiga Mkoloni na wengine wengi mnaweza mkawa msaada kwa mada hii kama hamtajali. Tunaomba darasa.
 
Last edited by a moderator:
NJELLU, Gawio la hisa hutolewa baada ya kipindi Fulani na hutegemea na faida pia. Makampuni mengi kila baada ya miezi 12 (kipindi cha mwaka wa kifedha wa kampuni) huandaa mahesabu ya kampuni na kisha wakaguzi wa nje huja kukagua na kutoa ripoti. Baada ya hapo Bodi ya wakurugenzi hukaa kuona je, kampuni imepata faida? Kama kuna faida je, kiasi gani igawiwe kwa wanahisa na kila hisa ipate kiasi gani. Si lazima faida yote ikatolewa kama gawio, wakati mwingine faida huwekwa kama akiba au hutumika katika shughuli za uwekezaji wa kampuni.
 
ASHADII, kushuka kwa thamani ya hisa kunachangiwa na mambo mengi. Thamani za hisa zaweza kushuka kwa sababu Kampuni inajihusisha na vitendo vya rushwa, hailipi kodi inavyostahili, inanyanyasa wafanyakazi kwa kuweka mazingira mabaya ya kazi au inalipa ujira usio stahiri, inajihusisha na uchafuzi wa mazingira au ubora wa huduma/bidhaa kushuka na ''poor nanagement''. Wahasibu hutumia nenO moja ''GOODWILL''.
 
Hisa za mwanzo zinaamuliwa na wamiliki. Kampuni ni lazima iwe na watu walioianzisha hawa huweka mipango mikakati. Hubainisha kampuni itajihusisha na nini na umiliki wake utakuwaje. Hapo kwenye umiliki ndipo huamliwa kampuni iwe na hisa ngapi, ngapi ziuzwe na ngapi ziwekwe akiba. Pia huamua hisa za kampuni ziwe na thamani ipi (kwa kuanzia).

thanks
 
Lugha iliyotumika katika kujibu swali la kushuka kwa hisa, inafanya mtu wa kawaida kuwa mwoga sana wa kununua HISA. Sababu unajiuliza maswali kama 2nd quarter ilikuwa na faida zaidi ya 1st quarter inakuwaje HISA zishuke thamani sababu tu zimeingia sokoni?

Au better yet, ikiwa kampuni imesha amua HISA 500 ndio zitakuwa kwa wale ambao ni wanunua HISA si inatakiwa ziendelee kupanda/kushuka tokana na kupanda/kushuka kwa thamani ya kampuni yenyewe?

Samahani, ni mchanga kabisa katika sekta hii, na hivi nimepata mtu wa kunielewesha naona nibanane nawewe unipe darasa.

CC: Wakuu TUKUTUKU, Bulesi, burden, Madewa, Prisoner 46664, KIBANGA Ampiga Mkoloni na wengine wengi mnaweza mkawa msaada kwa mada hii kama hamtajali. Tunaomba darasa.

Salaam AshaDii,...hope all is well...

Nitachangia kidogo...

Kwanza kabisa, huku nikiheshimu jibu la mkuu TUKUTUKU hapo,,ningependa pia kusema kuwa hisa, zikiwa kama sehemu ya umiliki wa kampuni, soko lake ni kama la bidhaa nyingine yeyote..mtu atakubaliana na mimi kuwa kuna sababu zaidi ya moja inayoweza kupelekea kupanda au kushuka kwa bei ya bidhaa fulani sokoni wakati fulani. Inaweza kuwa ni sababu ya kupungua/kufurika kwa bidhaa husika sokoni, kuwepo kwa bidhaa shindani bora zaidi, hisia ya wateja kuhusu kukosekana kwa bidhaa hiyo hapo baadaye na hivyo kutaka kununua kiasi kikubwa leo na kadhalika....

Primarily, alichokisema TUKUTUKU kwamba bei ya hisa sokoni inakuwa determined solely na demand vs supply ya hisa at a time ni kweli kabisa. Lakini je, ni nini kinachopelekea mtu kutaka kuuza au kununua hizo hisa na hivyo kuathiri kiasi hicho cha demand/supply ya hisa sokoni at a time? Sababu ni nyingi..mfano:

1) Current company profits - Kuna watu wanaodhani kuwa kampuni ikipata faida kubwa mwaka huu kuliko uliopita basi itakuwa inafanya vizuri na hivyo wanaamua kuwa sehemu ya wamiliki na hivyo kutaka kununua hisa zake. Hata hivyo faida ya sasa ya kampuni inaweza isiwe kipimo tosha cha uzuri au ubaya wa kampuni. Mfano, kwenye hii case ya CRDB, inawezekana faida yake kubwa imetokana na vyanzo visivyoweza kujirudia mwakani (one - off transactions) kama kuuzwa kwa baadhi ya assets zake n.k..mwekezaji anapoona kuwa kampuni imeshindwa kutengeneza faida kwenye ile biashara yake kuu, basi ataona kuwa uwezo wa kampuni kutengeneza faida utakuwa mdogo pia huko miaka ya mbele na hivyo kutaka kuuza hisa zake.

2) Company prospects/Investment plans (Mipango endelevu) - Kampuni inaweza kutengeneza faida nzuri leo, lakini kwa kulinganisha mipango mikakati yake ya muda mrefu, faida yake haitaongezeka kwa kasi kama ile ya washindani wake wa karibu. Kwa matarajio ya kupata faida zaidi baadaye, mwekezaji anaweza kuamua kuuza hisa zake na kununua za kampuni nyingine yenye mipango yenye faida zaidi huko mbeleni.

3) Decline in company's market share -
Wawekezaji siku zote hutaka kuweka pesa zao pale ambapo wanahisi zitakuwa na faida kubwa zaidi. Kampuni inaweza kuwa imepata faida leo, lakini ukubwa/umahiri wake kwenye soko lake la bidhaa ukawa unapungua taratibu. Hivyo wawekezaji wataona uwezekano wa kutengeneza faida zaidi ikiwa watawekeza kwenye hiyo kampuni nyingine inayoonyesha ukuaji wa soko lake la bidhaa ingawa hapa walipowekeza sasa kumepatikana faida pia.

4) Temporary buyers/sellers -
Masoko ya hisa duniani kote siku hizi yametawaliwa na watu wanaotaka kununua hisa na kukaa nazo kwa muda mfupi tu mpaka hapo bei itakapopanda kidogo ili wauze wapate faida, halafu wanunue nyingine na kuuza tena kwa mtindo huo huo. Hii inaweza kuwa kweli kwa case ya CRDB pia. Kwamba hawa wawekezaji waliopeleka sokoni walikuwa wanasubiria kampuni itangaze gawio la faida kwa mwaka (dividends), wachukue faida yao halafu wauze hisa zao na kupeleka sehemu nyingine. Utashangaa kuwa kuna watu huwa wanawekeza ada za shule za watoto wao kwenye hisa na wakati wa kulipa ada ukifika inabidi tu wauze ili walipe ada..no matter what!

5) Wawekezaji kulipa mikopo - hii hutokea mara nyingi wakati kampuni nzuri ikiingiza hisa zake sokoni kwa mara ya kwanza. Wawekezaji huweza kuchukua mikopo benki, kununua hisa na kukaa nazo, na kuziuza pindi bei inapopanda sokoni (au wakati wowote muda wa kurejesha mikopo hiyo benki unapofika, bila kujali bei ya hisa sokoni wakati huo!)

6) Speculative buyers (wanunuzi watabiri) - Hawa ndio wameshamiri kwenye masoko ya hisa duniani kote, na ndio chanzo kikuu cha financial crisis iliyoikumba Marekani miaka ya juzi. Ni kwamba badala ya watu kununua hisa za kampuni kwa sababu ya uwezo wake wa uzalishaji wa sasa hivi, ununuzi wa hisa unakuwa umeegemea zaidi kwenye yatakayotokea kwenye kampuni miaka hata 20 au 100 ijayo. Kunakuwa na watu wapiga debe, wanaochimba (au kupika) habari za mipango ya kampuni (au ya serikali, itakayoneemesha mapato ya kampuni) hata miaka 10 huko inayokuja. Kwa hivyo basi watu hawa kwa maneno yao wanaishia kusababisha bei ya hisa kuongezeka ama kupungua...

kwa hivyo kwa kujibu swali lako dada Ashadii, kutokana na kuwepo hasa hasa kwa wanunuzi/wauzaji wa hisa wa category namba sita (6) hapo juu, mara nyingi bei ya hisa sokoni haiendani moja kwa moja na ubora wa kampuni kwenye kuzalisha fedha kwa sasa. Kifupi kuna mambo meengi tu yanayoweza kufanya prospective investors wakaongeza ama kupunguza imani yao kwa kampuni fulani. Ndiyo maana unaweza kuona wakati mtu kama Steve Jobs alipokuwa anakaribia kujiuzulu kama Apple CEO ilibidi kufanyike marketing campaign ya kutosha ku-restore investor confidence na kuwadhihirishia watu kuwa kampuni itaendelea kuwa kwenye mikono salama, itaendelea kupata faida, na hivyo watu hawana haja ya kuuza hisa zao kwa hofu ya kupata hasara huko mbeleni.

In a nutshell, the best way to buy or sell shares is to just act like a smart layman, huhitaji technicalities nyiingi kuhusu sijui faida ama hasara ya kampuni leo, earnings per share, etc...angalia mifano ya maswali anayotakiwa kujiuliza layman hapa:

(a) Twiga/Simba Cement zinazalisha cement? Je cement itaendelea kuwa bidhaa inayohitajika na watu wengi? Je demand yake ni kubwa? Je bidhaa za kampuni zina ushindani mkubwa sokoni? Je kampuni ina uongozi mzuri? kama majibu ni ndiyo badi nunua hisa..lakini mwaka 2014 ukishasikia Dangote Cement imeanza kuzalisha cement kule mtwara kwa kiwango kinachotosheleza demand ya Afrika Mashariki yote,,,you should know it is a sign that Twiga's share of the cement market is about to decline and..may be, may be you need to sell your shares!

(b) Hisa za Precision Air...ilikuwa ni sahihi kabisa kwa watu kununua hisa za Precision Air wakati ambapo kampuni ilikuwa inaoperate kama monopoly, bila mshindani. Hii ni kwa sababu lazima kampuni ingetengeneza pesa tu, iwe isiwe (walau ikiwa na uongozi makini kidogo). Lakini je, baada ya kuja kwa fast jet, Precision ina uwezo wa kuendelea kutengeneza pesa?Je ina uwezo/mipango gani ya kupambana na hii bei ndogo ya mshindani wake ilhali wote tunajua wateja wanavyopenda kulipa gharama ndogo kuliko kubwa?..haya ni maamuzi ambayo yanaweza kufanywa na a smart layman...trust me,hayo ni muhimu kuliko expert advice...
 
Sina haja ya kuongeza katika darasa alilotoa PRISONER kwani kwa kiswahili cha mtaani ningesema kaua bendi!! He has covered all the basics as far as selling and buying on the stock exchange is concerned!
 
So till nw kwamtazamo wangu plus mchanganuo hasa wa u monopoly hisa nzuri kununua ni za TBL na TCC...
Naomba ushauri kwahili wadau
 
Wakuu,

Mimi sifahamu nini maana ya HISA naomba mwenye uelewa anielezee kwa undani.
 
Wakuu mimi sifahamu nini maana ya HISA naomba mwenye uelewa anielezee in deep.

Mkuu

Hisa ni sehemu ya umiliki wa kampuni.

Mtaji wa kampuni huwa unagawanywa katika vipande au visehemu vilivyo sawa, na hivyo visehemu ndo vinavyoitwa hisa.

Mfano:- wewe na rafiki zako watatu mkiamua kuchanga Tsh 2M kila mtu ili muanzishe biashara ya duka, ina maana jumla ya mtaji wenu itakuwa ni Tsh 6M

Kwa lugha nyingine itakuwa ni sawa na kusema kila mtu anamiliki asilimia 25% ya kampuni.

Sasa inaweza fika kipindi mmoja wenu anataka kujitoa, au kuna mtu mwingine anataka kuingia, mtafanyaje fanyaje ili aingie au atoke bila kuharibu hesabu zilizopo za mtaji wenu?

Ndo hapo ambapo wataalam walikuja na hii dhana ya Hisa kwamba, Mtaji ule wenu jumla yake yaan Tsh 6M zinagawanywa ktk vipande vilivyo sawa, lets say vipandw vya 6000 vilivyo sawa ambapo kwa mfano wetu huo kila kipande kitakuwa na thaman ya Tsh 1000.

sasa hapo utagundua kuwa kila mmoja wenu ktk wale watatu akogawanya hela alotoa ile 2M kwa thaman ya kila kipande (Hisa) itakuwa sawa na kusema kila mtu anamiliki hisa 2000.

na ndo hapo inapokuja kuwa rahis kumuuzia yeyote yule sababu unakuwa unajua unamiliki nini, na kina thaman gan? Unaweza tu kuamua kuniuzia hisa zako 500 we ukabakiwa na 1500 na maisha yakaendelea bila kuvuruga mahesabu ya kampuni.
 
Mkuu

Hisa ni sehemu ya umiliki wa kampuni.

Mtaji wa kampuni huwa unagawanywa katika vipande au visehemu vilivyo sawa, na hivyo visehemu ndo vinavyoitwa hisa.

Mfano:- wewe na rafiki zako watatu mkiamua kuchanga Tsh 2M kila mtu ili muanzishe biashara ya duka, ina maana jumla ya mtaji wenu itakuwa ni Tsh 6M

Kwa lugha nyingine itakuwa ni sawa na kusema kila mtu anamiliki asilimia 25% ya kampuni.

Sasa inaweza fika kipindi mmoja wenu anataka kujitoa, au kuna mtu mwingine anataka kuingia, mtafanyaje fanyaje ili aingie au atoke bila kuharibu hesabu zilizopo za mtaji wenu?

Ndo hapo ambapo wataalam walikuja na hii dhana ya Hisa kwamba, Mtaji ule wenu jumla yake yaan Tsh 6M zinagawanywa ktk vipande vilivyo sawa, lets say vipandw vya 6000 vilivyo sawa ambapo kwa mfano wetu huo kila kipande kitakuwa na thaman ya Tsh 1000.

sasa hapo utagundua kuwa kila mmoja wenu ktk wale watatu akogawanya hela alotoa ile 2M kwa thaman ya kila kipande (Hisa) itakuwa sawa na kusema kila mtu anamiliki hisa 2000.

na ndo hapo inapokuja kuwa rahis kumuuzia yeyote yule sababu unakuwa unajua unamiliki nini, na kina thaman gan? Unaweza tu kuamua kuniuzia hisa zako 500 we ukabakiwa na 1500 na maisha yakaendelea bila kuvuruga mahesabu ya kampuni.

shukrani sana mkuu.
 
Back
Top Bottom