Hisa za Kampuni ya kuchimba gas (Swala Tanzania)

Hisa za Kampuni ya kuchimba gas (Swala Tanzania)

Hawajafanya exploration yeyote

Sasa hizo pesa walizochukua sindio sehemu fulani itatumika kufanya hiyo exploration! Mbona hilo linajulikana....biashara yoyote ina risk....wakipata gas basi thamani ya hizo hisa zitapanda maradufu....wakikosa zitashuka thamani...ila wataendelea kufanya exploration sehemu nyingine
 
tufanye mapenzi

Usithubutu kulamba sumu na akati una taarifa kuwa hii ni sumu.pia do you understand about how much is 1.2milion USD per day.na kufanya exploration inachukua zaidi ya miezi.kwanza kwa hisa zote zilizonunuliwa I don't think kuwa inatosha kukodi rig kwa siku 2.
 
Usithubutu kulamba sumu na akati una taarifa kuwa hii ni sumu.pia do you understand about how much is 1.2milion USD per day.na kufanya exploration inachukua zaidi ya miezi.kwanza kwa hisa zote zilizonunuliwa I don't think kuwa inatosha kukodi rig kwa siku 2.

Au nunua halafu utatuletea feedback
 
Kwa kawaida utaratibu wa kuuza hisa za makampuni kwa mara ya kwanza(IPO) hutangazwa kwenye vyombo vya habari,mara zote hutoa muda wa mauzo ambao huwa ni mwezi mmoja hivi. Wakiishafunga mauzo ya awali kila aliyenunua hizo hisa anakuwa na umiliki wa sehemu ya hiyo kampuni kulingana na hisa alizolipia.Kiwango gani mtu ananunua inategemea na mtu binafsi, ni kwa kiasi gani yuko tayari kama mjasiliamali kuwekeza pesa yake pamoja na athali za kukosa ambozo zipo wakati wote katika biashara yoyote ile. Baada ya mauzo ya awali hisa za hiyo kampuni hu-orodheshwa katika soko la hisa,na hapa ndipo aliyewekeza ana uhuru wa kuendelea kuzishikilia hizo hisa kwa kungoja gawio au kuziuza kwa faida. Chukulia mfano wa swala: Hisa moja iliuzwa kwa shs 500... Kama uliamua kununua hisa 10000 maana yake(shs 500*10000=shs5000000)
Hivi sasa ziko sokoni kwa bei kati ya shs 600-700...tuchukulie kuwa unaweza kupata mnunuzi kwa sh 650@ maana
utatengeneza(shs 650*10000=shs6500000) hapa una faida ya shs 1500000 katika kipindi cha mwezi mmoja na hii
ina maana kuwa uwekezaji wako umetengeneza faida ya 30% ambayo unaweza kuiacha ikiwe ukingoje gawio tena au kuchukua pesa yako na kuachana na swala ili kuwekeza kwingine.Nafikiri Maluyaga Ikohi mtakuwa mmeelewa.

Umeelezea vzr sana...hivi sasa hisa za swala ni 650 wanunuzi wapo wengi ikiwemo na mm....ila wauzaji mpaka sasa hakuna....kila mtu kashikilia hisa zake hawaachi
 
Kwa kawaida utaratibu wa kuuza hisa za makampuni kwa mara ya kwanza(IPO) hutangazwa kwenye vyombo vya habari,mara zote hutoa muda wa mauzo ambao huwa ni mwezi mmoja hivi. Wakiishafunga mauzo ya awali kila aliyenunua hizo hisa anakuwa na umiliki wa sehemu ya hiyo kampuni kulingana na hisa alizolipia.Kiwango gani mtu ananunua inategemea na mtu binafsi, ni kwa kiasi gani yuko tayari kama mjasiliamali kuwekeza pesa yake pamoja na athali za kukosa ambozo zipo wakati wote katika biashara yoyote ile. Baada ya mauzo ya awali hisa za hiyo kampuni hu-orodheshwa katika soko la hisa,na hapa ndipo aliyewekeza ana uhuru wa kuendelea kuzishikilia hizo hisa kwa kungoja gawio au kuziuza kwa faida. Chukulia mfano wa swala: Hisa moja iliuzwa kwa shs 500... Kama uliamua kununua hisa 10000 maana yake(shs 500*10000=shs5000000)
Hivi sasa ziko sokoni kwa bei kati ya shs 600-700...tuchukulie kuwa unaweza kupata mnunuzi kwa sh 650@ maana
utatengeneza(shs 650*10000=shs6500000) hapa una faida ya shs 1500000 katika kipindi cha mwezi mmoja na hii
ina maana kuwa uwekezaji wako umetengeneza faida ya 30% ambayo unaweza kuiacha ikiwe ukingoje gawio tena au kuchukua pesa yako na kuachana na swala ili kuwekeza kwingine.Nafikiri Maluyaga Ikohi mtakuwa mmeelewa.

Je unaweza kununua hisa kwa bei zaidi ya uliotolewa na dse? Kama njia ya kumshawishi mwenye hisa akuuzie! Na kwa bei iliyotolewa na dse ni kama bei elekezi!
 
Umeelezea vzr sana...hivi sasa hisa za swala ni 650 wanunuzi wapo wengi ikiwemo na mm....ila wauzaji mpaka sasa hakuna....kila mtu kashikilia hisa zake hawaachi
Ndugu Nalo neno,Hapo ndipo unapokuja kwenye kiini cha kufanya biashara katika soko la hisa.kumbuka anayeshikilia hisa anafahamu ni thamani gani hisa za swala katika industry ya gesi na mafuta inaweza kufika,kama ana taarifa zinazomfanya aamini kuwa thamani ya swala inaweza kupanda zaidi hadi tuseme 2000tsh kwa hisa basi hatauza hisa zake bali ataendelea kuzishikilia, labda wewe unayezitaka uweke dau la tuseme 2500 kwa hisa. Kwako wewe unayezitaka hizo hisa za swala unatakiwa uwe na taarifa muhimu za kampuni hiyo na mwelekeo wake katika hiyo industry, ukiwa na silka ya ujasiliamali basi nenda soko la hisa weka bei yako ya kununulia hisa za swala kwa mfano 800tsh kwa kila hisa, inawezekana wanaozishikilia wakavutwa na bei yako na kukuuzia kiasi walichonacho,kwa maana hiyo basi kadili watu wanavyoshindana kuweka madau bei yake inazidi kupanda.Vinginevyo wale wanaozishikilia wanaweza kuamua kupanga bei hata zaidi ya hiyo iliyoko DSE.nafikiri nimekujibu.
 
Kuna MTU kaeleza vizuri hizi hisa za makampuni ya gesi ni utata sana, Jamaa hawawezi kuchimba gesi na juu mtaji sema kampuni zenye mitaji mikubwa zinaweza kuja nunua blocks za gesi baadae wanahisa wakapata hela ndefu sana ..kumbuka hata BG juzi wametangaza kuuza block zao za gesi Tanzania ili kupunguza gharama za kampuni na Jamaa ndio wawekezaji wakubwa kwenye gesi ..ni kama vile wazungu wanavyopewa vibali vya kuchimba madini alafu wanapeleka London stock kuraise hela lets say £5m exchange baada ya muda utasikia kuna madini ya bil 500 sijui hawana mtaji lakini kampuni kubwa zinawavua hata kwa hela ndefu ..Hapo wanapowavua ndio Jamaa wanapiga hela ..itokeee sasa mashimo Yale hayana kitu ni full hasara ..ila biz zote ni risk tu ..na risk ikiwa kubwa return kubwa ila tujenge Tabia ya kusoma taarifa za makampuni ..industry ..information information muhimu sana kwenye hii game ya hisa hope nimesomeka
 
Naomba kujuzwa,

-Utaratibu wa kununua hisa kwenye masoko ya nje ya nchi ukoje?

- Nikinunua hisa za Swala kwenye soko la hisa hapa Dar(DSE), niza Swala Tanzania au Swala Group, nina maanisha na biashara zao zilizopo Kenya na nchi nyingine?

- Ninaweza kupata hisa za Swala Group kwenye soko la nje kwa bei ya chini ya Tanzania, sh. 650 mdau aliyo mention kwenye huu uzi. Hasara zake ni zipi?
 
Ndugu Nalo neno,Hapo ndipo unapokuja kwenye kiini cha kufanya biashara katika soko la hisa.kumbuka anayeshikilia hisa anafahamu ni thamani gani hisa za swala katika industry ya gesi na mafuta inaweza kufika,kama ana taarifa zinazomfanya aamini kuwa thamani ya swala inaweza kupanda zaidi hadi tuseme 2000tsh kwa hisa basi hatauza hisa zake bali ataendelea kuzishikilia, labda wewe unayezitaka uweke dau la tuseme 2500 kwa hisa. Kwako wewe unayezitaka hizo hisa za swala unatakiwa uwe na taarifa muhimu za kampuni hiyo na mwelekeo wake katika hiyo industry, ukiwa na silka ya ujasiliamali basi nenda soko la hisa weka bei yako ya kununulia hisa za swala kwa mfano 800tsh kwa kila hisa, inawezekana wanaozishikilia wakavutwa na bei yako na kukuuzia kiasi walichonacho,kwa maana hiyo basi kadili watu wanavyoshindana kuweka madau bei yake inazidi kupanda.Vinginevyo wale wanaozishikilia wanaweza kuamua kupanga bei hata zaidi ya hiyo iliyoko DSE.nafikiri nimekujibu.

Nimekuelewa...hivyo pia hii ni biashara huria....mnaweza kupangiana bei zaidi ya bei elekezi. Shukrani
 
Wakuu naomba labda nisaidie wengi wasio fahamu. Jambo la mafuta/gesi limegawanyika sehemu mbili yaani baharini (offshore) na nchi kavu (land/onshore). Kutokana na Swala Energy Plc tutazungumza Nchi kavu (onshore/land). Swala wao sio kampuni ya uchimba kitaalamu (E&P au Exploration & Production) bali wao ni wamiliki wa haki za kuchimba.

Kabla mafuta au gas kuchimbwa lazima sehemu usika ifahamike, kisha lazima kampuni za seismic ( kama Polaris, Geokinetics au CGG veritas) waje wafanye uchunguzi kama sehemu hiyo ina hydrocarbons. Swala wao wana haki za kutafuta mafuta sehemu mbili Pangani Basin (maeneo ya Pangani) na Kilombero Basin (maeneo ya kilombero). Wapo kwenye early stage za kuangalia kama sehemu hizo kuna hydrocarbons, wamekwenda DSE ili wapate mtaji utakao wapa uwezo wa kuajiri contractor (Polaris Seismic) kufanya study kama sehemu hiyo inamafuta au lahasha. Leo Swala wametangaza kumaliza kufanya 2D (2 Dimension) seismic survey (uchunguzi) katika block moja ndani ya Pangani Basin ambayo wameita Moshi Block (walio kwenye mafuta wanajua ni tamaduni kutumia majina ya ajabu ajabu kwenye block, mfano offshore kuna Pweza 1, pale Texas kuna Thunderbird, Maconda). Sasa baada ya kumaliza hii survey kinachofuata ni Geo-scientist kusoma data ambazo zimepatikana, then wao wanaweza kusema kwamba labda kuna mafuta, sasa baada ya hapo Swala Energy Plc wanaweza kuuza hizo block kwa kampuni kama BP, ExxonMobile, na n.k ambazo hizo zinafanya E&P. Kuna njia nyingi ambazo hutumika, wanaweza kuuza kwa vipande vipande (multiclient) au wakauza block nzima kwa mteja mmoja.

Kama huko juu nimekuchanganya jua kimoja Swala Plc sio kampuni ya kuchimba mafuta, na hawana mtaji wa kuchimba mafuta, bali wao wamechukua risk za kutafuta maeneo ambayo wanadhani yana mafuta, wakafanya study kuhakiki kwamba mafuta yapo, baada ya kumaliza study na kupata uhakika wanauza haki za kuchimba. In conclusion wao ni kama madalali lakini wana incur all seismic cost.
 
naona sasa hivi bei za hisa za swala zimefikia kama s 2000 per share listing
 
Mwezi mmoja uliopita niliona kwenye taarifa ya Habari ya Biashara ITV, wakawa wanasema thamani ya vipande vya SWALA imepanda kufikia sh.900 @ share na leo ni tar.20/10/2014.
 
Mmiliki wa machimbo ya gas ni nani?
 
Tuliambia gas itakomesha mgawo wa umeme, gas ni ya nani?
 
Back
Top Bottom