Hisa za NMB kushuka

real G

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2013
Posts
5,227
Reaction score
5,299
Habari wana JF.

Nilikua naangalia trend ya bei za hisa hapa soko la DSE nikaona za NMB zimeshuka kutoka 4300 hadi mwezi huu ni 3500.

Je, benki inafanya vibaya au ni nini, Pia ningependa kujua timing nzuri ya kununua hisa ni kipindi gani cha mwaka.

Natanguliza shukrani
!
 
Kununua hisa si kama kilimo cha mahindi (hakuna kipindi maalumu). Ni sawa na bei ya mafuta ktk soko la dunia. Pitia taarifa za fedha, mipango ya kampuni, utendaji kazi wa viongozi, ....kisha fanya maamuzi. Ni vizuri kununua bei ikiwa chini. Nwaka 2012 - 2013 hisa za NMB zilikuwa kama Tsh. 800, CRDB Tsh. 150
 
Ndo maana sitakuja wekeza kwenye soko la hisa
 
angalia kama walikuwa wanatoa dividends maana wakiwa wanatoa bei hupanda wakishatoa bei inashuka ,baada ya hapo hupanda tena
 
Huu ndo muda muafaka wa kuzinunua hizi hisa, bei ikipanda unachukua dividend yako na unaziuza....
Zikishuka unazinunua tena...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…