Hisa zimekua kama Kamali nilinunua za CRDB mwaka 2014 Kwa 5000shares@sh.400 Taangu hapo hisa za CRDB zimekua zikishishuka tuu mwaka 2015 nikapata Gawio la sh.15/share so 5000shares@sh.15 nikajipatia Tsh 75,000 kwa Mwaka Fikiria Unawekeza 2,000,000 ili upate 75,000 kwa mwaka ni Utahira nikaziuza kwa Bei ya Hasara.
Hisa ni Upuuzi Flani hivi inaweza kutoka kwenye IPO zika trade kwa sh. 50 au Sh. 30
Hisa ni Kwa watu wenye mitaji Mikubwa na hawana pa Kuweka Pesa zao I am sure Mtu aliyewekeza Sh. 800,000,000 atafadika kwa Sababu atakua na 2,000,000@sh 15 atapata dividend ya 30,000,000 kwa Mwaka
Lakini bado ni Utoto hiyo Sh. 800,000,000 iweke kwenye Fixed Diposit ambazo nyingi zinatoa Riba hadi ya 12% so Tsh 800,000,000×12% =96,000,000 So utavuna Sh. 96,000,000 kwa mwaka tofauti na kwenye hisa
Mda huu naangalia Hisa za CRDB ni Tsh. 185/Kwa hisa je Utauza hisa ulizonunua kwa sh. 400? Kwa 185 Usiume meno kama unapesa kama 5,000,000 Anzisha biashara hata za Saluni Kubwa ya Kike na Kiume Utapata Faida Kubwa sana kuliko hisa.
Tazama Majedwali haya Bei ya Hisa Kwa Baadhi ya Kampuni Mwaka 2014
View attachment 498547
Bei ya Hisa Leo 20, April 2017 Naona ACCASIA imefanya Vizuri mwaka 2014 hisa zake ziliuzwa kwa 6810 bei ya December Leo tarehe 20/4/2017 zinauzwa 13030 ime double kwa hiyo ni Profitable
Kuna KAMPUNI ya Bima ya Kenya ile ya Jubilee Holdings Ltd Nayo imefanya Vizuri Mwaka 2014 ilikua Tsh. 8510 Leo JHL= sh.10330
Tanzania Breweries Ltd (TBL) imedondokea Pua Bei ya hisa yake December 2014 ilikua ni 14,090 Leo hii TBL=12,000
Kwa Ufafanuzi huo wa baadhi ya Kampuni unajua kumbe Kampuni za Nje zimefanya Vizuri kuliko za Ndani mfano hiyo Accassia ambayo ipo pia katika London Stock Exchange (LSE) pia tumeona Jubilee Holding Ltd ambayo ipo pia katika Nairobi Stock Exchange (NSE) imefanya Vizuri Kampuni za Tanzania Nyingi zimezingua pamoja na TTC hisa zake ziliuzwa kwa 16,740 mwaka 2014 Leo kwenye Jedwali hapa inaonesha zinauzwa kwa 11,500.
Jedwali La Bei za Hisa Leo 20/4/2017.
View attachment 498549