Historia inathibitisha kuwa Kiongozi mkubwa wa upinzani anapofungwa, mabadiliko ya kidemokrasia yanakaribia

Historia inathibitisha kuwa Kiongozi mkubwa wa upinzani anapofungwa, mabadiliko ya kidemokrasia yanakaribia

Fundi Madirisha

Senior Member
Joined
Jun 30, 2020
Posts
184
Reaction score
988
Kama wewe ni mfuatiliaji wa historia na msomaji mzuri matukio ya kisiasa duniani na mabadiliko ya kidemokrasia katika nchi mbali mbali na hata kwenye ukombozi, utakubaliana na mimi mabadiliko ya demokrasia na katiba katika nchi hizo yaliambatana na maumivu makali ya viongozi wa vyama vyama vya upinzani likiwemo la kufungwa jela kwa kesi za kutengeneza.

Ilitokea kwa kina mzee Kenyatta, Raila Odinga wa Kenya, Mzee Mandela, kina Hakainde Hichilema wa Zambia na wengine.

Ukiona taifa limefikia sasa viongozi wakuu wa vyama vya upinzani wanafungwa jela kwa sababu ambazo ni za kubambikizia, ujue mabadiliko ya kidemokrasia katika eneo hilo hayako mbali. Hii ni kawaida kabisa ni kwa mujibu wa historia zilizopita na ndicho kitakachotokea kwa Tanzania. Kama tutabishana humu basi muda utaongea.

Kesi ya Freeman Mbowe kwa jinsi ushahidi unavyoendelea kwanza haiendani na matukio ya kigaidi, Unaona kabisa ni kama kuna kitu kinachongwa au kinatafutwa ili tu aende jela.

Hakuna ugaidi unaofadhiliwa kwa shilingi laki 6, ugaidi ni neno kubwa sana na linatisha. Huwezi kufananisha na kesi ya Mbowe ambayo unaona kabisa mashadi w upande wa mashtaka anahangaika.

Kuna uwezekano kabisa muda si mrefu CHADEMA wakaja kua sehemu ya serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania au kikaongoza kabisa nchi. Hii ni baada ya Wananchi kua na awareness .
 
mleta mada umeandika andiko zuri la kuwapa tahadhari viongozi wakubwa wa nchi hii waliopo kwenye circle ya kuitafuna keki ya taifa.

ila sidhani kama watajishughulisha kutafakari na andiko lako. watakuupuuza na kuziba masikio yao.
giphy.gif
 
CCM siku zao zinakaribia mwisho na sina wasiwasi na hilo hata kidogo, huwezi kutawala watu wenye akili zao kila siku kwa kuwaibia kura kila uchaguzi
 
Siyo mabadiliko tu sema mabadiliko chanya
 
CCM siku zao zinakaribia mwisho na sina wasiwasi na hilo hata kidogo, huwezi kutawala watu wenye akili zao kila siku kwa kuwaibia kura kila uchaguzi
Naaamini maneno yako na ya wahenga kuwa daima ukiona giza linazidi basi jua kuwa ndiyo mwanga unakaribia.
 
mleta mada umeandika andiko zuri la kuwapa tahadhari viongozi wakubwa wa nchi hii waliopo kwenye circle ya kuitafuna keki ya taifa.

ila sidhani kama watajishughulisha kutafakari na andiko lako. watakuupuuza na kuziba masikio yao.
Mkuu ilusemwa kuwa kenge hawezi amini kuwa ameumia hadi pale damu zitakapo mtoka masikioni.
 
Back
Top Bottom