Historia Pekee ya Pemba na Wapemba

Historia Pekee ya Pemba na Wapemba

Hivi Mzee muhammedi, ungekuwa Raisi wa Tanzania.
Naomba unitajie vipaumbele vyako Vinne ambavyo unge vishughulikia kwa siku zako mia moja(100) za kwanza.

Halafu hebu tueleze ungependa Tanganyika - Zanzibar (Tanzania) iwe Nchi ya namna gani.

Tupo tunakusikiliza Mzee wetu, funguka.
Che...
Cheo kikubwa nilichopata kushika ni mkutubi (Librarian) wa darasa shule ya msingi.

Unaniwazia kuwa Rais wa Tanzania?
 
Che...
Cheo kikubwa nilichopata kushika ni mkutubi (Librarian) wa darasa shule ya msingi.

Unaniwazia kuwa Rais wa Tanzania?
Una haki ya kuwa na cheo chochote hapa Tanzania.
Librarians ni watu wenye akili nyingi sana kwakuwa wanasoma vitabu muda wote.

Kama huwezi kuwa Raisi kwa sababu ya Umri.
Basi mjibie Mwanao yaani Mtoto wako.

Kama mtoto wako akibahatika kuwa Raisi wa Tanzania utamshauri nini kuhusu hayo maswali yangu.
Ayajibu namna gani ?

Watu wanataka kukusikia ukijibu hayo maswali na sio mimi tu.

Wanataka kwa Hekima yako na umri wako unasemaje kuhusu nilivyo kuuliza ?
 
HISTORIA YA PEKEE YA PEMBA NA WAPEMBA

Wenyeji wangu wamenifikisha Wete kiasi cha saa nne asubuhi jua limepanda na mji umechangamka.

Gari yetu imeegesha pembeni na mkuu wa msafara katoka nje na kuvuka barabara kwenda upande wa pili.

Mimi nimelazimishwa lazima nikae kiti cha mbele naambiwa nipate kuiona Pemba vizuri.
Gari nzuri na imefunguliwa nasikiliza FM Station - Radio Istiqama.

Hii ni Radio ya Ibadh.
Nilipokuwa Tanga nilikuwa mjumbe wa Bodi ya Radio Istiqama ya Tanga kituo kilipofunguliwa.

Utastaajabu lakini ndiyo ukweli wenyewe radio inayosikilizwa ni hiyo tu.
ZBC haina wasikilizaji.

ZBC watu huifunguwa muda maalum kusikiliza matangazo ya vifo.
Bado niko ndani ya gari emeegeshwa pembeni ya barabara.

Jicho la camera yangu limevutiwa na mnara mrefu wa msikiti mkubwa lakini naona pia nyumba zilizochakaa kupita kiasi pembezoni yake ingawa mjengo wa nyumba hizi unaonyesha zilikuwa wakati wake nyumba za kupendeza.

Nimewauliza wenyeji wangu kuhusu nyumba moja iliyochoka iweje iachiwe kuporomoka kiasi kile.

"Hiyo ni ofisi ya serikali zamani ilikuwa nyumba ya mtu binafsi na bwana huyu mwenye nyumba hiyo alikuwa mtu mwema, karimu akisaidia shughuli nyingi za Kiislam.

Mtaa mzima huo ulikuwa na nyumba nzuri za watu wema.

Wema huu uliondoka na mapinduzi mwaka wa 1964 na hadi leo mtaa na majengo yote mazuri yamejiinamia."

"In Shaa Allah nema na salama vitarejea," nawaombea dua ndugu zangu.

Nimekuwa mzoefu wa historia ya Zanzibar na mimi binafsi ili kupoza machungu ya historia ya visiwa hivi hupenda kutazama historia hii kama, "tragicomedy," (kichekesho ndani ya huzuni) yaani mimi hutafuta lililo laini ndani ya ugumu wa historia ya Zanzibar kulieleza.

Kukaa ukaekeza machungu matupu kunaumiza nafsi.
Jicho langu linarejea kwenye ofisi ya serikali iliyokuwa nyumba ya kuishi.

Hakika iko hoi.
Kuta zinahitaji rangi.

Nje kuko hivi ndani kutakuwaje?
Kichekesho kikanijia nikacheka.

Jicho langu sasa likaangukia nje ya dirisha la gari.
Nakaribishwa na maandishi yaliyopo kwenye barza ya kahawa: "Karibu Domo Free Kazi Iendelee."

Haraka nikapiga picha kimya kimya.
Nasoma maneno kutoka Qur'an Tukufu: "Fantashiruu Fil Ardhi," hayako mbali na, "Domo Free Kazi."

Najichekea moyoni.
Najiuliza kama hii barza naweza kuipa jina la Kiswahili, "Kazi Bure."

Tupia jicho lako kwenye meza iliyo na jiko la mkaa na mabirika ya kahawa hapo chini kwrnye picha.
Hao hapo ndiyo Wapemba.

Nimeelezwa kuwa Mpemba akikuambia, "Nakuja," msubiri.

Ukimsikia kasema, "Naja ondoka haraka."
Hapana tena salama hapo.

Haya nimeelezwa Kojani.
Wakojani ni mabingwa wa bahari.

Hawaiogopi bahari na vitimbi vyake.
Kwa Wakojani sufuria imepata mfuniko.

Bahari inamuheshimu Mkojani sembuse binadamu?
Nilishuka kutoka kwenye gari nikawatolea salama wanabarza wa "Domo Free," ukipenda, "Kazi Bure."

Waliniitikia na wakaendelea na mazungumzo yao wakizungumza kwa sauti ya chini.
Lakini nilijua toka mwanzo kuwa walikuwa wakinitazama na walijua kuwa mimi ni mgeni.

"Huyu mtu kafuata nini?"
Hili lazima walijiuliza.

Huwa wakati mwingine najiambia mweyewe nimesoma mengi kuhusu Gestapo kiasi kila sehemu nifikayo yenye historia ya mateso naingiwa na hofu.

Pemba ina mgao wake wa kutosha wa historia ya kusikitisha.

Wenyeji wangu wakanifahamisha kuwa barza mfano wa hiyo ziko Pemba nzima na yalikuwa matawi ya CUF sasa ni ya ACT Wazalendo na kahawa katika matawi hayo ni bure si biashara.

Pita barzani toa taarifa au kunywa kahawa nenda na hamsini zako.
Matawi haya yana nguvu isiyomithilika.

Usidanganyike na ile kahawa na chochote kilicho machoni pako.

Wapiga kura wao wanafahamika kwa sura na majina na wanajigamba hawajapata kupiga kura iliyoharibika wala kushindwa uchaguzi.

Barza hii ipo jirani na uwanja ambako baada ya mapinduzi wananchi walikuwa wakiletwa kupigwa viboko hadharani.

Miaka ni mingi imepita na nimesimama mahali watu wakiadhibiwa kwa viboko lakini uwanja ule wa henzerani haupo tena.

Kilichobakia ni historia ya viboko vile na majina ya wapigaji viboko.
Mmoja aliyekuwa akisimamia adhabu hii ya kudhalilisha tulikuja kufahamiana vyema Dar es Salaam.

Lakini naamini kwa wakati ule alikuwa kajuta maana alikuwa mcha Mungu.
Mmoja wa rafiki zangu aliniambia katika sifa zake alikuwa kahifadhi Barzanji yote kifuani.

Turudi vibokoni.

Waliopigwa viboko vile baadhi wa hai na ukisimama mahali pale ukawatafuta utawapata.
Nilibahatika kukutana na mmojawapo.

Pemba ina historia nzito na ina watu tofauti sana kwa kila kitu.
Nidhamu ya watu wake ni ya kipekee.

Historia hii inatisha sana.

Ikawaje Tanzania kupambania uhuru wa Afrika ilihali wananchi wake wapo dhalilili kiasi hiki?

Mzee,
Nasubiria kusoma zaidi hii historia. Kuna mengi sana tumedanganywa mashuleni.

Nchi inahitaji kutubu
 
Mzee Mohamed Said huwa namkubali sana kwa uandishi na simulizi zake. Anabusara sana!
 
Ipo hivi mzee akiwa rais maudhui ya nyuz zake ndo itakua vpaumbele vyake, dully saiks atakua waziri wa michezo na sanaa, bunge litahamia ukumbi wa anatoglo, wazee wake wote wataingizwa kwny mitaala ya shule wajulikane kisawasawa, historia ya taifa itaeditiwa pakubwa kwa mlengo wake, wazee wa barza kunywa gahawa free nch nzma,kariakoo itakua kama dubai
 
Ipo hivi mzee akiwa rais maudhui ya nyuz zake ndo itakua vpaumbele vyake, dully saiks atakua waziri wa michezo na sanaa, bunge litahamia ukumbi wa anatoglo, wazee wake wote wataingizwa kwny mitaala ya shule wajulikane kisawasawa, historia ya taifa itaeditiwa pakubwa kwa mlengo wake, wazee wa barza kunywa gahawa free nch nzma,kariakoo itakua kama dubai
Lugoda,
Unafanya kejeli katika jambo ambalo halistahili kuchezwa shere.

Historia ya uhuru wa Tanganyika sasa ni nyingine si ile iliyokuwa sawa na mchuzi uliotiwa maji ya baridi.

Historia hii ya wazee wangu ipo katika Cambridge Journal of African History toka 1998 na imo katika Dictionary of African Biography toka 2011.

Maprofesa wa historia vyuo vingi duniani wanaposomesha historia ya Mwalimu Nyerere rejea muhimu ni kitabu cha Abdul Sykes na rejea hizo mbili nilizokutajia hapo juu.

Ndani ya Cambridge Journal of African History wanafunzi wanawasoma John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan waliofanya pitio la kitabu changu.

Katika Dictionary of African Biography wanafunzi wanamsoma Dr. Kwegyir Aggrey na Kleist Sykes.

Sababu ya rejea hii ni kuwa ilikuwa Dr. Aggrey ndiye aliyempa Sykes wazo la kuunda African Association alipokuja Tanganyika 1924.

Kleist aliunda African Association 1929 na katika kuona faida ya jumuia akaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) 1933 na taasisi zote hizi zilitoa mchango mkubwa katika kuundwa kwa TANU 1954 na kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
Mkuu kabla hujaondoka Pemba tujuze pia asili au chimbuko la Rashfold wa Manchester United,, yule wakwetu kabisa,, tusiache asili ipotee
 
Mkuu kabla hujaondoka Pemba tujuze pia asili au chimbuko la Rashfold wa Manchester United,, yule wakwetu kabisa,, tusiache asili ipotee
He is of paternal Jamaican descent, and maternal Kittitian descent, with his grandmother being born on the West Indies island of Saint Kitts
 
Una haki ya kuwa na cheo chochote hapa Tanzania.
Librarians ni watu wenye akili nyingi sana kwakuwa wanasoma vitabu muda wote.

Kama huwezi kuwa Raisi kwa sababu ya Umri.
Basi mjibie Mwanao yaani Mtoto wako.

Kama mtoto wako akibahatika kuwa Raisi wa Tanzania utamshauri nini kuhusu hayo maswali yangu.
Ayajibu namna gani ?

Watu wanataka kukusikia ukijibu hayo maswali na sio mimi tu.

Wanataka kwa Hekima yako na umri wako unasemaje kuhusu nilivyo kuuliza ?

Rais wa Kenya William Ruto amewapa uraia watu wa jamii ya Wapemba wasio na utaifa, ambao walitambuliwa rasmi tu kati ya makabila ya nchi hiyo mnamo Februari.

Uraia utawapa kundi hilo “kitambulisho na utambuzi wanaostahili” na kuruhusu jamii kupata huduma za umma, Rais Ruto alisema.

"Hii, kwa hakika, inamaliza hali ya watu wa Pemba kutokuwa na utaifa na kutengwa ambao umedumu kwa takriban miaka 100," alisema wakati wa hafla ya Ijumaa.

Jamii ya Wapemba inakadiriwa kuwa takriban 7,000 kwa idadi na wamejikita katika maeneo ya pwani ya Kenya ya Kwale, Kilifi, Mombasa na Lamu.

Rais alitoa vitambulisho, vyeti vya umiliki wa ardhi, vyeti vya kuzaliwa na hati za kusafiria katika hafla iliyoashiria kukamilika kwa mchakato wa usajili wa wanajamii wote.

Hatua hiyo hatimaye inawawezesha Wapemba kupata huduma kamili za umma kama shule, huduma za afya, hifadhi ya jamii na haki ya kufanya kazi ambayo wamekuwa wakinyimwa kwa muda mrefu.
 
Back
Top Bottom