Historia ya Ali Msham, mwalimu na mama Maria Nyerere Magomeni Mapipa 1954

Historia ya Ali Msham, mwalimu na mama Maria Nyerere Magomeni Mapipa 1954

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Katika historia za wazalendo waliopigania uhuru wa Tanganyika lakini wamesahaulika historia ya Ali Msham ina sehemu ya pekee moyoni kwangu.

Tafadhali isikilize historia yake:

 
Hapakuwa na Wakristu waliosahaulika? Harafu Walisahaulika vipi nawe umewakumbuka Mkuu!?
 
Hapakuwa na Wakristu waliosahaulika? Harafu Walisahaulika vipi nawe umewakumbuka Mkuu!?
Scale,
Unaniuliza kama hakuna Wakristo waliosahaulika mfano wa Ali Msham waliojitolea kama Ali Msham?

''Harafu'' ni ''halafu.''

Unaniuliza vipi nimewakumbuka?
Vipi nimewakumbuka?

Hujasikiliza video umefanya haraka kurejea kwangu.
Kuwa na subira unasikiliza kisha ndiyo unarejea hapa kama una maswali unauliza.

Najua kwa nini una haraka ya kuja kuuliza maswali.
Historia hii kwa ukweli inataabisha wengi.

Wanajiuliza imekuwaje watu kama akina Ali Msham walijitolea kupigania uhuru.
Wanajiuliza imekuwaje wengine walijitenga na harakati hizi?

Wanajiuliza imekuwaje watu kama Ali Msham wakafutika katika historia ya TANU?
 
Mohamed Said tatizo la kimfumo la nchi yetu. Elewa kabisa hicho ndicho wapigania uhuru wetu baada ya kupata uhuru walijikita kwenye fitina za kisiasa na kujiimarisha badala ya kuangalia historia ya nchi kwa miaka 100 ijayo. Chukulia mfano tu Dkt Magufuli aliposema hukumu za mahakama ziwe kiswahili au historia yetu ifundishwe mashuleni in addition iliyopo, lakini Mama Samia kaja waziri yule yule akabadili na kupiga marufuku hilo somo lisifundishwe. Kwa hiyo nadhani wabobezi kama wewe mnatakiwa mpewe fungu zuri la kuandika historia mpya ya nchi yetu ili ifundishwe mashuleni na tupate ma profesa wabobezi kwenye historia yetu.
 
Kila unayemzungumzia Ni Muislamu tu
Uzalendo...
Ikiwa ni historia ya TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika ni tabu sana kuwakwepa Waislam.

Katika historia ya TANU Waislam ndiyo waliokuwako mbele na kwa uhakika kuanzia wakati wa kuunda African Association 1929.

Angalia hayo majina ya waasisi wa African Association:

Cecil Matola, Kleist Abdallah Sykes, Ibrahim Hamisi, Mzee bin Sudi, Ali Said Mpima, Raikes Kusi, Rawson Watts, Suleiman Majisu na Zibe Kidasi.

Pembeni ya African Association wakaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933 hili lilikuwa jaribio la kujaribu kuitenganisha African Association na ushawishi wa Waislam.

Wanachama wa mwanzo wa TANU walitoka Rufiji na walikwenda kuandikishwa na Said Chamwenyewe.

Kuna historia ilikuwaje wanachama wakafuatwa Rufiji.
Siwezi kuiweka hapa ni kisa kirefu lakini nimekieleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

Hawa walikuwa ''murid,'' wa Tariqa Quadiriyya ambayo Khalifa wake alikuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir.

Wako waliodhani wanaweza kuandika historia ya TANU kwa kuwakwepa Waislam kwa makusudi.
Hii ndiyo sababu leo unamsoma Ali Msham hapa na unauliza kwa nini Waislam?

Angalia picha hii ya 1955:

1653160809014.png
 
Labda ni mume wa FaizaFoksi
Asprin,
Imekuwa kawaida kutukanwa.

Kwa kweli historia ya uhuru wa Tanganyika niliyoandika baada ya kuona kuwa historia iliyokuwa ikisomeshwa si ya kweli inawataabisha watu wengi sana.

Lakini nitafanya nini?
Huwezi kummzuia mtu kutukana.
 
Uzalendo...
Ikiwa ni historia ya TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika ni tabu sana kuwakwepa Waislam.

Katika historia ya TANU Waislam ndiyo waliokuwako mbele na kwa uhakika kuanzia wakati wa kuunda African Association 1929.

Angalia hayo majina ya waasisi wa African Association:

Cecil Matola, Kleist Abdallah Sykes, Ibrahim Hamisi, Mzee bin Sudi, Ali Said Mpima, Raikes Kusi, Rawson Watts, Suleiman Majisu na Zibe Kidasi.

Pembeni ya African Association wakaunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933 hili lilikuwa jaribio la kujaribu kuitenganisha African Association na ushawishi wa Waislam.

Wanachama wa mwanzo wa TANU walitoka Rufiji na walikwenda kuandikishwa na Said Chamwenyewe.

Kuna historia ilikuwaje wanachama wakafuatwa Rufiji.
Siwezi kuiweka hapa ni kisa kirefu lakini nimekieleza katika kitabu cha Abdul Sykes.

Hawa walikuwa ''murid,'' wa Tariqa Quadiriyya ambayo Khalifa wake alikuwa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir.

Wako waliodhani wanaweza kuandika historia ya TANU kwa kuwakwepa Waislam kwa makusudi.
Hii ndiyo sababu leo unamsoma Ali Msham hapa na unauliza kwa nini Waislam?

Angalia picha hii ya 1955:

View attachment 2233523
Tunaweza kupata historia ya Cecil Matola au Rawson Watts?
 
Tunaweza kupata historia ya Cecil Matola au Rawson Watts?
Gobole,
Nimejitahidi sana kutafuta historia ya waasisi wote wa African Association nimeshindwa.

Niliyonayo kuhusu hawa wazalendo ni yale ambayo Kleist Sykes aliandika katika mswada wa kitabu cha maisha yake kabla ya kufariki mwaka wa 1949.
 
Asprin,
Imekuwa kawaida kutukanwa.

Kwa kweli historia ya uhuru wa Tanganyika niliyoandika baada ya kuona kuwa historia iliyokuwa ikisomeshwa si ya kweli inawataabisha watu wengi sana.

Lakini nitafanya nini?
Huwezi kummzuia mtu kutukana.
Mzee wangu Mohamed

Labda ili wengine wafurahi na waone uko fair hizi historia mara nyingine uwe unazitoa ukiwataja wale wenye majina ya kiyahudi.

Makala zako mara nyingi husifia wale wenye majina ya wafuasi wa Mtume.

Hebu siku moja tuambie mtu mmoja aliyesaidia sana kupambania Uhuru wetu ukimuacha Nyerere.
 
Mzee wangu Mohamed

Labda ili wengine wafurahi na waone uko fair hizi historia mara nyingine uwe unazitoa ukiwataja wale wenye majina ya kiyahudi.

Makala zako mara nyingi husifia wale wenye majina ya wafuasi wa Mtume.

Hebu siku moja tuambie mtu mmoja aliyesaidia sana kupambania Uhuru wetu ukimuacha Nyerere.
Asprin,
Kumtaja mtu mmoja aliyesaidia sana katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika ni kazi ngumu sana na naweza kusema haiwezekani.

Haiwezekani kwa kuwa ni tabu kupima kwa uhakika kuwa huyu fulani ndiye.
Ngoja nikupe mfano kwa wazalendo waliokuwa Dar es Salaam.

Hapa nitakutajia majina yao na waliyofanya kila mtu kwa kile alichokuwa na uwezo nacho na hii michango yao baadhi haikuwa ya siri wanachama wote wa TANU wakijua.

1950 kulikuwa na wajumbe wa TAA Political Subcommittee: Dr. Vedasto Kyaruzi, Abdul Sykes, Hamza Mwapachu, Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Said Chaurembo, John Rupia na Steven Mhando.

Katika kamati hii alikuwapo pembeni ingawa jina lake halipo katika orodha ya wajumbe, Earle Seaton mwanasheria aliyekuwa akiishauri kamati hii kuhusu Tanganyika kuwa katika Udhamini wa Uingereza.

Huyu Earle Seaton ndiye aliyeishauri TAA iweke nguvu ya kwenda UNO kuwasilisha madai ya uhuru wa Tanganyika.

Katika kamati hii mjumbe aliyekuwa na heshima kubwa na wafuasi wengi nje ya duru hili la wanasiasa wa TAA alikuwa Sheikh Hassan bin Ameir aliyekuwa na wafuasi Tanganyika nzima na hawa wote walijiunga na TANU kwa wakati mmoja TANU ilipoasisiwa 1954.

Lakini mambo hayaweza kwenda bila fedha.

TAA hadi TANU ilikuwa hapa Dar es Salaam na wafadhili wake wakubwa: John Rupia, Dossa Aziz na Abdul na Aly Sykes.

Abdul Sykes ndiye aliyekabidhiwa kuishi na Nyerere nyumbani kwake Mwalimu alipoacha kazi mwaka wa 1955, Dossa akatoa gari yake kuipa TANU imsaidie Nyerere katika shughuli zake za chama kama President wa TANU.

Kulikuwa na askari wenda kwa miguu, ''foot soldiers,'' waliopita nyumba kwa nyumba kuwashawishi wananchi kujiunga na TANU - Bi. Titi Mohamed, Bi. Tatu Bint Mzee, Hawa bint kwa kuwataja wachache na hawa wanakwenda pamoja na Bantu Group akina Rashid Sisso na wenzake akina Juma Mlevi wahamasishaji umma na walinzi wa viongozi.

Sheikh Hassan mwenyewe akiuza kadi za TANU misikitini nchi nzima alipokuwa anakwenda kwa ajili ya kusomesha.

Abdul Sykes akiuza kadi za TANU Kariakoo Market alipokuwa Mkuu wa Soko, yaani Market Master.

Hii ni Dar es Salaam peke yake akini nchi nzima palipofunguliwa matawi ya TANU wazalendo kama hawa walikuwapo.

Huwezi kusema kuwa Nyerere ndiye aliyepigania uhuru wa Tanganyika peke yake kama ilivyo katika historia au anaweza kupatikana mtu zaidi ya Nyerere aliyepigania uhuru wa Tanganyika.

Swali lako halikukaa vyema limehitaji kutengenezwa.
Nyerere peke yake asingefika popote.

Hakuna mtu yeyote aliyekuwa anamjua wala hakuwa na fedha za kuendesha chama si wakati wa TAA wala wakati wa TANU.

Umefika wakati historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika iwekwe wazi.
Kuwa ''fair'' ndiyo huku.

Katika picha hiyo hapo chini yuko Bi. Titi Mohamed, John Rupia, Mohamed Jumbe Tambaza na wazee wa Dar es Salaam wana TANU.

1653218496505.jpeg
 
Back
Top Bottom