Historia ya Bangladesh chini ya watawala wanawake wawili marafiki waliogeuka mahasimu

Historia ya Bangladesh chini ya watawala wanawake wawili marafiki waliogeuka mahasimu

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kwa miaka 33, tangu mwaka 1991 taifa la Bangladesh limetawaliwa na wanawake wawili mawaziri wakuu kwa vipindi tofauti kwa kila mmoja wakipokezana miaka mitano mitano. Aliyeanza kutawala alikuwa Khaleda Zia kisha akaja Sheikh Hasina halafu akarudia Zia tena ndipo akarudi Hasina tena kuanzia mwaka 2009 mpaka sasa alipotimuliwa na waandamanaji.

Wote wawili wametokea katika familia za Urais au Marais. Sheikh Hasina ni mtoto wa Rais wa Kwanza wa Bangladesh ambaye aliongoza mapambano ya Bangladesh kujitenga kutoka India na ambaye baadaye alipunduliwa na kuuwawa na wanafamilia wake wengi, Khaleda Zia ni mke mjane wa Rais aliyepindua nchi kijeshi kabla na yeye kupinduliwa tena baadaye.

Wanawake wote wawili waliibuka kama marafiki wapigania demokrasia na wanamegeuzi waliogeuka baadaye kuwa mahasimu, mafisadi na madikteta.

Enzi za uhasama kulikuwa na vurugu nyingi za kisiasa, kutekana na kuuana kati ya kambi zao. Sheikh Hasina aliweza kujisimika mamlakani vizuri zaidi kama waziri mkuu mwenye nguvu na kumfunga hasimu wake na rafiki yake wa zamani Zia kifungo cha gerezani, leo hii Hasina alivyotimuliwa na waandamanaji Rais wa Bangladesh kaamuru Zia na wafungwa wengine wa kisiasa kuachiwa huru!
 
NYONGEZA

Serikali imeondolewa madarakani kwa maandamo yalioanzishwa na wanafunzi wa vyuo vikuu. Wiki chache zilizopita walikua na total shutdown, hakuna internet, kupiga simu wala kusafiri nchi nzima.

30% ya ajira za serikali zilikuwa zikitolewa kwa vizazi vya freedom fighter wa nchi hiyo wasio kidhi ambayo ilisabibisha wasomi wengi wa nchi hiyo kukosa ajira. Wanafunzi wa vyuo vikuu kupitia social media n.k wakaorganize maandamo ya kupinga 30% quota, maandamano yakaenea nchi nzima mpaka kufika hatua serikali Sheikh Hasina kutoka madarakani hii leo. Maandamano hayo yamesababisha vifo vya zaidi ya wanafunzi 500.
 
Ah, Jana nimecheka sana. Sikuamini kama Kuna siku nitashuhudia Sheikh Hasina akikimbia na kumwacha Khaleda Zia Bangladesh. Alitawala Kwa mkono wa chuma. Siamini kama alikimbia na chochote kati ya alivyovuna Kwa miaka 15 mfululizo aliyoyawala.
Alimtesa mwenzake mno. Japo yupo mahututi kitandani ila yeye kawakimbia waandamanaji Kwa helikopta ya kijeshi. Hapo ndo unaamini serikali inawekwa na Mungu na inaondolewa na Mungu. Ruto ana bahati kubwa sana.
Watawala wajifunze, Kuna muda huwa wanajisahau. Waliingia madarakani Kwa kuiba makura wanafikiri wanapendwa. Ikifika muda wa kuondoka ni lazima tu Mungu atawaondoa.
 
Kwa miaka 33, tangu mwaka 1991 taifa la Bangladesh limetawaliwa na wanawake wawili mawaziri wakuu kwa vipindi tofauti kwa kila mmoja wakipokezana miaka mitano mitano. Aliyeanza kutawala alikuwa Khaleda Zia kisha akaja Sheikh Hasina halafu akarudia Zia tena ndipo akarudi Hasina tena kuanzia mwaka 2009 mpaka sasa alipotimuliwa na waandamanaji.

Wote wawili wametokea katika familia za Urais au Marais. Sheikh Hasina ni mtoto wa Rais wa Kwanza wa Bangladesh ambaye aliongoza mapambano ya Bangladesh kujitenga kutoka India na ambaye baadaye alipunduliwa na kuuwawa na wanafamilia wake wengi, Khaleda Zia ni mke mjane wa Rais aliyepindua nchi kijeshi kabla na yeye kupinduliwa tena baadaye.

Wanawake wote wawili waliibuka kama marafiki wapigania demokrasia na wanamegeuzi waliogeuka baadaye kuwa mahasimu, mafisadi na madikteta.

Enzi za uhasama kulikuwa na vurugu nyingi za kisiasa, kutekana na kuuana kati ya kambi zao. Sheikh Hasina aliweza kujisimika mamlakani vizuri zaidi kama waziri mkuu mwenye nguvu na kumfunga hasimu wake na rafiki yake wa zamani Zia kifungo cha gerezani, leo hii Hasina alivyotimuliwa na waandamanaji Rais wa Bangladesh kaamuru Zia na wafungwa wengine wa kisiasa kuachiwa huru!
Jana nilicheka sana. Nimewafuatilia toka 2007 Zia akiondolewa na wanajeshi. 2009 Hasina anachukua nchi na kuondoa caretaker government. Ametawala Kwa mkono wa chuma. Jana anakimbia na ndege ya kijeshi? Kweli maisha yanaenda Kasi. Ni kama kule Sri Lanka. Ile familia ya Rajapaksa haikuamini Kuna siku wataachia madaraka Kwa aibu. Walikua, teka na kufanya wawezavyo. Siku Ile raisi anakimbia Kwa ndege ya kijeshi ndo nikaamini wananchi wakichoka waogope sana. Hawanaga msalie mtume.
 
NYONGEZA

Serikali imeondolewa madarakani kwa maandamo yalioanzishwa na wanafunzi wa vyuo vikuu. Wiki chache zilizopita walikua na total shutdown, hakuna internet, kupiga simu wala kusafiri nchi nzima.

30% ya ajira za serikali zilikuwa zikitolewa kwa vizazi vya freedom fighter wa nchi hiyo wasio kidhi ambayo ilisabibisha wasomi wengi wa nchi hiyo kukosa ajira. Wanafunzi wa vyuo vikuu kupitia social media n.k wakaorganize maandamo ya kupinga 30% quota, maandamano yakaenea nchi nzima mpaka kufika hatua serikali Sheikh Hasina kutoka madarakani hii leo. Maandamano hayo yamesababisha vifo vya zaidi ya wanafunzi 500.
Kudai haki kokote lazima kugarimu maisha ya watu.
 
Ah, Jana nimecheka sana. Sikuamini kama Kuna siku nitashuhudia Sheikh Hasina akikimbia na kumwacha Khaleda Zia Bangladesh. Alitawala Kwa mkono wa chuma. Siamini kama alikimbia na chochote kati ya alivyovuna Kwa miaka 15 mfululizo aliyoyawala.
Alimtesa mwenzake mno. Japo yupo mahututi kitandani ila yeye kawakimbia waandamanaji Kwa helikopta ya kijeshi. Hapo ndo unaamini serikali inawekwa na Mungu na inaondolewa na Mungu. Ruto ana bahati kubwa sana.
Watawala wajifunze, Kuna muda huwa wanajisahau. Waliingia madarakani Kwa kuiba makura wanafikiri wanapendwa. Ikifika muda wa kuondoka ni lazima tu Mungu atawaondoa.
Hivi kuandama kwa kuwa wananchi wamemchoka kiongozi inahitaji kibali?
 
Watanzania tunalakujifunza.Hawa wanawake hawafai kabisa hata kidogo kuwakabidhi nchi.bangladesh wamekataa Nchi Yao kugeuzwa shamba la bibi kama hapa Danganyika
 
Hivi kuandama kwa kuwa wananchi wamemchoka kiongozi inahitaji kibali?
Haihitaji kibali, watu wanaamka asubuhi wanaingia mtaani, kesho yake wanaingia ikulu, bungeni na mahakama kuu. Then unashangaa mkuu wa serikali anakimbia nchi. Mara nyingi wanaokabidhiwa nchi huwa ni wanajeshi.
 
Ni fedheha sana Duniani Nchi kuongozwa na Mwanamke.
Ndio maana mataifa makubwa China,Russia na USA hayajawahi ongozwa na Wanawake.
 
Ni fedheha sana Duniani Nchi kuongozwa na Mwanamke.
Ndio maana mataifa makubwa China,Russia na USA hayajawahi ongozwa na Wanawake.
US wanaweza kuongozwa na mwanamke mwaka huu,
 
NYONGEZA

Serikali imeondolewa madarakani kwa maandamo yalioanzishwa na wanafunzi wa vyuo vikuu. Wiki chache zilizopita walikua na total shutdown, hakuna internet, kupiga simu wala kusafiri nchi nzima.

30% ya ajira za serikali zilikuwa zikitolewa kwa vizazi vya freedom fighter wa nchi hiyo wasio kidhi ambayo ilisabibisha wasomi wengi wa nchi hiyo kukosa ajira. Wanafunzi wa vyuo vikuu kupitia social media n.k wakaorganize maandamo ya kupinga 30% quota, maandamano yakaenea nchi nzima mpaka kufika hatua serikali Sheikh Hasina kutoka madarakani hii leo. Maandamano hayo yamesababisha vifo vya zaidi ya wanafunzi 500.
Ukiona kiongozi wa nchi katolewa madarakani kwa maandamano ya raia,usiamini kuwa kweli ni maandamano ya raia,raia ni chambo tu
 
Back
Top Bottom