Historia ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Historia ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Hey pals,,

I hope mko poa

Kwanza tuanze kwa kibwagizo kidogo tu
👇

Baba uliye juu mbinguni,wewe ndo Baba wa taifa,,/
Huyu Baba tuliye pewa hana lolote ni sifa,,,/

Hizo ni line nilizo kuta kwenye clip moja huko you tube ya jamaa mmoja akifanya freestyle kwenye Dakika kumi za maangamizi ambayo huwa segment inayo ruka kwenye kipindi cha planet bongo East Africa radio.
Kusema ukweli sikumwelewa jamaa alicho maanisha ila nilipenda tu jamaa alivyo kuwa akiflow na kumpa sifa Baba yetu aliye mbinguni (MUNGU).

Okay tuacheni hiyo,

Nimekuwa nikifuatilia matamko ya viongozi wa chama hiki bila kusahau Kinaitwa CCM,kama nimekosea jina lake vizuri mtanikosoa wadau,Matamko ya viongozi wa chama hiki kwenye awamu hii ya tano ni tofauti kabisa na awamu zingine zilizo pita,kwa ufupi ni kuwa wanajiamini kupitiliza kiasi kwamba naanza kuwaza baadhi ya vitu,

Moja ya maswali ninayo jiuliza ni haya hapa

👉Walio kianzisha chama hiki walifikiria kuwa ipo siku kuna chama kingine kitakuja kuchukua utawala wa nchi hii?

👉Au kilianzishwa ili kitawale milele?,Na kama Kilianzishwa kitawale milele nini kilifanya Hao watu waanzishe mfumo wa vyama vingi?

👉Je,mfumo wa vyama vingi ni kiini macho tu?

👉Je,haya mambo yanayo fanywa awamu hii ya kuminya demokrasia ndo yalikuwa ni moja ya mikakati ya kuanzishwa chama hiki? viongozi walio pita awamu zingine mbona hatukuyashuhudia haya? Au waliogopa kuyafanya kwa kuwa walikuwa na roho ya utu huku wakienda kinyume na mikakati ya chama chao?

👉Je,Awamu hii ya tano ndo kapatikana kiongozi ambaye anafanya Yale yote ambayo waasisi wa chama hiki waliyaweka kwenye mikakati yao?

👉Au uwezo mdogo wa viongoz wa awamu hii kujibu hoja ndo Ume wafanya CCM kuwabana upinzani?

NB: Kwa yanayo endelea kwa sasa hapa nchini ni kuwa CCM hawataki kutoka madarakani kwa kura labda kuna njia nyingine wanataka upinzani wafanye.

CCM lazima itoke madarakani kwa kura, ila kabla ya kura lazima viongozi wa upinzani wafanye kitu.

Jimmy-De-Lite
 
Hatuna mbadala wa Ccm kwa miaka 50 ijayo

Tusije tukaingizwa vitani na walafi wa madaraka

Zimwi likujualo....
 
Hangaikeni na kuzama kwa chadema CCM iacheni kama ilivyo ni mlima mrefu sana


State agent
 
Ni punguani anaweza kudhani kuna mbadala wa CCM. Tulidhani CHADEMA kingeweza kumbe kilikuwa chama cha Vibaraka wa mabeberu wakaanza kugombana wenyewe kwa wenyewe walivyoona wanaungwa mkono. Watanzania tumekishitukia hicho chama ndo maana kimeangukia pua na hakitainuka milele. Bora CCM itawale milele kuliko vyama vya kikabila kama CHADEMA, vya udini kama CUF na sasa ACT kimekuwa na mlengo wa udini
 
Ni punguani anaweza kudhani kuna mbadala wa CCM. Tulidhani CHADEMA kingeweza kumbe kilikuwa chama cha Vibaraka wa mabeberu wakaanza kugombana wenyewe kwa wenyewe walivyoona wanaungwa mkono. Watanzania tumekishitukia hicho chama ndo maana kimeangukia pua na hakitainuka milele. Bora CCM itawale milele kuliko vyama vya kikabila kama CHADEMA, vya udini kama CUF na sasa ACT kimekuwa na mlengo wa udini
Akili yako fupi kama maisha ya funza.
 
Akili yako fupi kama maisha ya funza.
Magufuli ni moto wa kuotea mbali. Mlidhani mtaleta nyodo mlizokuwa mnamletea mkwere anawachekea? Magufuli kawasoma kuwa hamjui sheria pia CHADEMA woote vilaza. Mmeshindwa kufuata katiba ya chana chenu kumuondoa Mbowe kwenye uwenyekiti wakati muda wake uliisha kitambo ndo muje kukiondoa CCM madarakani? Kujaza form tu za kugombea uwenyekiti wa serikali za mtaa mmeshindwa alafu eti mnazila na kugonea uchaguzi. Kagomeni CCM itaendelea kutawala milele. Magufuli anacheza na akili zenu mbovu
 
Akili yako fupi kama maisha ya funza.
Magufuli ni moto wa kuotea mbali. Mlidhani mtaleta nyodo mlizokuwa mnamletea mkwere anawachekea? Magufuli kawasoma kuwa hamjui sheria pia CHADEMA woote vilaza. Mmeshindwa kufuata katiba ya chana chenu kumuondoa Mbowe kwenye uwenyekiti wakati muda wake uliisha kitambo ndo muje kukiondoa CCM madarakani? Kujaza form tu za kugombea uwenyekiti wa serikali za mtaa mmeshindwa alafu eti mnazila na kugonea uchaguzi. Kagomeni CCM itaendelea kutawala milele. Magufuli anacheza na akili zenu mbovu
 
Kuna muda huwa nafikia hatua ya kumlaumu Mwalimu, yaani kabla ya kuondoka angekivunja hili dude...kuna muda lilitaka eti kumgeuka haya yeye mwenyewe...akatoka Butiama moja kwa moja hadi Dodoma ndani kikaoni...yaliyotokea humo wanayajua.
 
Magufuli ni moto wa kuotea mbali. Mlidhani mtaleta nyodo mlizokuwa mnamletea mkwere anawachekea? Magufuli kawasoma kuwa hamjui sheria pia CHADEMA woote vilaza. Mmeshindwa kufuata katiba ya chana chenu kumuondoa Mbowe kwenye uwenyekiti wakati muda wake uliisha kitambo ndo muje kukiondoa CCM madarakani? Kujaza form tu za kugombea uwenyekiti wa serikali za mtaa mmeshindwa alafu eti mnazila na kugonea uchaguzi. Kagomeni CCM itaendelea kutawala milele. Magufuli anacheza na akili zenu mbovu
Tulia wewe, Uchaguzi mdogo tu huu unawashinda kuandaa na kuukamilisha....aibu kubwa mnalipaka Taifa.
 
HISTORIA ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inakifanya kutumia taasisi za dola ikiwa ni pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama katika kutisha, kutesa, kunyamazisha na kudhoofisha upinzani wa kisiasa au wale wasio na mlengo wa CCM.
CCM, kama chama dola, kimetengeneza mfumo wa kuzif​anya taasisi zote za dola (nchi) kuwa matawi yake yakiongozwa na makada wa falsafa na itikadi yake!

Tazama mifano michache hapa chini jinsi CCM dola inavyotumia vyombo vya dola kudhoofisha upinzani.

1. Mwaka 1982 hadi 1992 kulikuwa na vuguvugu la ndani ya CCM lililochochewa na wanasiasa waliotofautiana na fikra kandamizi za demokrasia ya "chama kushika hatamu" pale nafasi za kisisasa zilipokuwa zikitolewa na kikao kimoja cha chama kwa malengo maalumu yanayotokana na utashi wa chama. CCM ilikuwa inakandamiza demokrasia ndani ya chama kwa kuzuia aina zote za upinzani wa ndani ya chama.

Nguvu za kijeshi na kipolisi zilitumika kuzima aina yoyote ya upinzani wa fikra, mawazo au imani (itikadi) kinyume na viongozi wateule wa CCM wanavyoamini! Hali hii iliwakuta kina Aboud Jumbe Mwinyi, Seif Sharif Hamad, Horace Kolimba na wengine ambao ndio waliokuwa chemchemi ya kukua kwa upinzani tunaoushuhudia leo.

2. Mwaka 1997 Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) ilitengeneza shauri la jinai Na. 279/1997 dhidi ya Machano Khamisi Ali (na wenzake 17) kwa tuhuma za uhaini dhidi ya SMZ. Shauri la uhaini Na. 7, 1999 lilikuja kubainika kwamba lilikuwa la kubambikiza na Mahakama Kuu ya Zanzibar iliwaachia huru watuhumiwa wakiwa wamesota magereza kwa zaidi ya miaka mitatu.

3. Januari 25, 2001 Mwenyekiti wa taifa wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba alipigwa na Polisi na kuvunjwa mkono alipokuwa njiani kwenda kwenye shughuli za kisiasa.

4. Hilo halikutosha kuonyesha jinsi CCM inavyotumia taasisi za ulinzi na usalama; mwaka 2005 aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Omar Idd Mahita alitoa tuhuma za ugaidi dhidi ya CUF na kukituhumu chama hicho kwamba kimeingiza makontena ya majambia kwa minajili ya kuendesha vitendo vya kigaidi!

Haya yalikuwa madai mazito kwa chama cha siasa. Hali hii iliifanya CUF ionekane kama chama kinachochochea vurugu. Na kulithibitisha hili mgombea urais wa CCM kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2005, Jakaya Khalfan Mrisho (Kikwete), alitumia propaganda hiyohiyo alipokuwa akihutubia wananchi wa Kilombero kwenye kampeni ya uchaguzi wa mwaka huo.

Kwa nyakati tofauti na mazingira yanayotatanisha vyama vya siasa vimekuwa vikipata wakati mgumu kuendesha shughuli za kisiasa hususan kwenye kuomba ruhusa (vibali) ya kufanya mikutano ya hadhara na au maandamano ya amani katika kutimiza utashi wa Katiba ya JMT ya 1977 (2005) na Sheria Na. 4, 1992 iliyotoa nafasi ya shughuli za vyama vingi vya siasa Tanzania.

5. Mfano mwingine ni kauli ya aliyekuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Luteni Jenerali, Afande Abdul'Rahman A. Shimbo kutoa "tamko la kijeshi" juu ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31, 2010. Tamko la kijeshi lililotolewa na JWTZ kupitia kwa Afande Shimbo lilikuwa ni "amri" kutoka kwa Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama ambaye alikuwa mwenyekiti wa CCM taifa!

6. Januari 5, 2011 Jiji la Arusha lilishuhudia nguvu za Polisi na taasisi za ulinzi zinazofanya kazi chini kwa chini (under cover) zikifanya mauaji mengine! Mara hii haikuwa CUF; ilikuwa ni maandamano ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kilichokuwa kinafanya maandamano ya amani yaliyogeuzwa uwanja wa majaribio yaleyale ya taasisi za ulinzi na usalama kudhibiti upinzani.

7. Tangu hapo; viongozi wa ngazi za juu wa CHADEMA wamekuwa wakifunguliwa mashauri (kesi) mbalimbali za jinai mahakamani katika kile kinachoonekana kwamba ni uvunjaji wa sheria, kanuni na taratibu unaochukuliwa kwa kisingizio (pretext) kwamba chama hicho kilitangaza kuwa, "nchi haitatawalika." Propaganda zilizokuwa zinatumika dhidi ya CUF baina ya mwaka 2000 hadi 2010 sasa zimegeuzwa upande wa CHADEMA!

Mwisho; kwa kuwa CCM imejijengea nguvu ya uwezo (leverage) kikatiba kwa kuchukua sehemu muhimu ya kutawala na kuendesha shughuli za ulinzi na usalama kama ilivyo kwenye Ibara ya 33(2) na ya 148 ya Katiba ya JMT ya 1977 (2005), taathira ya moja kwa moja juu ya utendaji wa taasisi za ulinzi na usalama ni kuitumikia CCM katika kulinda masilahi ya muda mrefu ya kutawala siasa.

Tazama Ibara ya 148 (2) (a) hadi (d) ya Katiba ya JMT ya 1977 (2005) yanavyompa madaraka ya kutumia majeshi mwenyekiti wa CCM taifa! Hivyo ndivyo anavyoweza kutumia Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) kama inavyoanzishwa kwenye Ofisi ya Rais (kifungu cha 4(1) cha Sheria Na. 15 ya 1996).

Rais wa nchi ndiye anayemuajiri Mkurugenzi Mkuu wa TISS (tazama kifungu cha 6(1) cha Sheria Na. 15, 1996); na yeye (rais wa nchi) ndiye anayeamua kumtumia mwajiriwa huyo vile apendavyo (kifungu cha 6(2) cha Sheria Na. 15, 1996).
Kama taasisi za ulinzi na usalama zote zimeundwa kwa utashi wa CCM na zinafanya kazi kwa mfumo uleule wa "amri baada ya amri" huku mwenyekiti wa CCM taifa akiwa ndiye mtoa amri (Amiri Jeshi Mkuu) unadhani wapinzani wanaweza kupata haki?


8. 02/01/2013 katika kipindi cha TUONGEE ASUBUHI cha ITV naibu katibu mkuu CCM bara Mwigulu Nchemba alitoa kauli nzito ya kwamba ANAYO NA ANAMILIKI CD YENYE VIDEO ya jinsi viongozi wa CHADEMA walivyokaa na kupanga mikakati jinsi ya kutekeleza mauaji nchini. Mpaka wakati huu mwigulu hajawahi kukamatwa wala kuulizwa ukweli wa swala hili.

Ushauri kwa CCM ni kuacha kutumia vyombo vya Dora kwaani wananchi wa leo siyo wa miaka ya 80. dunia nzima imebadlika kama tunaweza kutoa maoni kupitia mitandao ya kijamii.

Tafakalini swala hili kwaani kila mwananchi anajua kuwa ni mchezo mchafu. mfano kama polisi wangekuwa makini basi wangekuwa wanashughulikia issue zote bila kuangalia upande wa kisiasa.

Vyama vya siasa viwe makini kwaani kwa mfumo huu CCM itapandikiza wanachama amabo ni informer (watu wa usalama) kusaidia kuua upinzani.
Ukweli mtupu tuutafakari tujue nini cha kufanya.
 
LKN pia CCM ndicho chama pekee kisichofungamana na kabira lolote,ukanda wowote au dini yoyote, CCM ni chama cha watanźania woote,bira kujari makabira yako na dini zao
Ndabaningi...
Utahitaji utafiti wa kisayansi kusadikisha hoja zako.

Tanzania ukabila si tatizo toka ukoloni wala ukanda ni hisia zilizo chini sana.

Tatizo la Tanzani ni udini.
Fanya utafiti.
 
Unapoitamka Tanzania maana ake ni toka 1964,unapoitamka tanganyika maana ake ni baada ya ukoloni miaka ya1961,nyuma ya hapo ni hakuna tanganyika wala Tanzania,ila ila kuna Dutch ost africa, ya wakoloni, hapo unaiona tanganyika,Uganda,na kenya vikiwa chini ya mtawala mmoja mkoloni,swali langu ni kwa nn kenya kuna ukabila na uganda kuna ukabila,?! Na Tanzania pana utulivu kw nn,!? Ccm ipo madarakani toka mwaka 1958 baada ya uchaguz wa balaza la legco na nyerere kuwa wazir mkuu wa kwanza tanganyika.kw nn ccm ipo mpk leo na haiteteleki inazidi kuimalika?.wewe kw akii yako haya yanatokea kw kudra za mwenyez mungu au ni kwa bahati mbaya tu?
 
Ndabaningi...
Utahitaji utafiti wa kisayansi kusadikisha hoja zako.

Tanzania ukabila si tatizo toka ukoloni wala ukanda ni hisia zilizo chini sana.

Tatizo la Tanzani ni udini.
Fanya utafiti.
Mzee mohamedi tanzania kuna udini???. Hebu fafanua mkuu unijuze?.
 
Back
Top Bottom