Historia ya Dkt John Pombe Magufuli

Historia ya Dkt John Pombe Magufuli

unauhakika alizaliwa CHATO? tuwekee cheti chake cha kuzaliwa na utuambie alizaliwa hospital gani
Wapi umesikia au umesoma kazaliwa Chato?
Mbona hamtaki kuelewa? Kuna sehemu hapo imetaja kuwa kazaliwa Chato?
 
Wapi umesikia au umesoma kazaliwa Chato?
Mbona hamtaki kuelewa? Kuna sehemu hapo imetaja kuwa kazaliwa Chato?
lete ushahidi wa kuzaliwa huko katoma na ututajie hospital aliyozaliwa vinginevo utakuwa ni walewale wakulungwa.
BEN SAA8 hii ilimkost alipoamua kuingia deep kujua MEKO ni mtanzania au tumepigwa FAMBA
 
lete ushahidi wa kuzaliwa huko katoma na ututajie hospital aliyozaliwa vinginevo utakuwa ni walewale wakulungwa.
BEN SAA8 hii ilimkost alipoamua kuingia deep kujua MEKO ni mtanzania au tumepigwa FAMBA
Umeanza Chato umeona umekosea umerudi katoma.
Sawa mkuu kwa vile unataka kufahamu ni vyema kuanzia leo tambua kuwa Magufuli ni mzaliwa wa katoma pia na makaburi ya wazazi wake upande wa baba yapo katoma.
Pia mimi ni mtu wa maeneo hayo.
 
lete ushahidi wa kuzaliwa huko katoma na ututajie hospital aliyozaliwa vinginevo utakuwa ni walewale wakulungwa.
BEN SAA8 hii ilimkost alipoamua kuingia deep kujua MEKO ni mtanzania au tumepigwa FAMBA
Kuhusu hospitali usizani kila mtu kazaliwa hospitali.
Asilimia kubwa ya watu wanao zaliwa kijijini wamezaliwa nyumbani wala si hospitali maana hata hospitali ni shida kupata.
Magufuli amezaliwa nyumbani kwao katoma.
 
lete ushahidi wa kuzaliwa huko katoma na ututajie hospital aliyozaliwa vinginevo utakuwa ni walewale wakulungwa.
BEN SAA8 hii ilimkost alipoamua kuingia deep kujua MEKO ni mtanzania au tumepigwa FAMBA
Rudi mkuu mbona umepotea
 
Hatimaye kesho mwaka mmoja tangu mwamba atoke umefika.
 
WASIFU:

Taaluma yake;

Dkt, John Joseph Pombe Magufuli ni mwalimu na mtalaamu wa kemia akiwa na Shahada ya Uzamivu (PhD).



Kuzaliwa
Alizaliwa Oktoba 29 mwaka 1959 huko Katoma tarafa ya Bugando wilayani Geita jimbo la Geita vijijini.

Kipindi hicho Geita ikiwa ni moja ya wilaya mkoa Mwanza.

Baadaye wakahamia Chato mkoani Geita, Kaskazini Magharibi mwa Tanzania.

Elimu
Magufuli alipata elimu ya msingi katika shule ya msingi Chato kuanzia mwaka 1967 hadi 1974.

Mwaka 1975 alijiunga na Seminary ya Katoke iliyo Biharamulo, Kagera kwa Elimu ya sekondari na kisha kujiunga na shule ya sekondari ya Lake iliyoko Mwanza hadi 1978 alipohitimu.

Mwaka 1979 alijiunga na shule ya Sekondari ya Upili ya Mkwawa, Iringa kwa ajili ya masomo ya kidato cha tano na sita na kuhitimu Mwaka 1981.

Mwaka 1981 hadi 1982 alisomea Stashahada (Diploma) ya Ualimu wa masomo ya Sayansi katika Chuo cha Ualimu cha Mkwawa, Iringa Masomo makuu yakiwa Kemia na Hisabati

Akiwa kazini, Magufuli aliamua kujiendeleza kwa kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka 1985 hadi 1988 alipotunukiwa Shahada ya Ualimu katika masomo ya Kemia na Hisabati.

Mwaka 1991 hadi 1994 alisomea Shahada ya Uzamili ya Kemia (Msc. Chemistry) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Tanzania na Chuo Kikuu cha Salford, Uingereza

Mwaka 2009 alitunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) ya Kemia kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Mafunzo ya Kijeshi
Kati ya Mwaka 1983 na 1984, Magufuli alipitia mafunzo ya kijeshi kwa mujibu wa sheria kwenye Kambi za Jeshi la Kujenga Taifa Makutupora - Dodoma, Makuyuni - Arusha na Mpwapwa - Dodoma.

Kazi
Baada ya kufuzu Stashahada ya Ualimu, alifundisha masomo ya Hisabati (Mathematics) na Kemia (Chemistry) katika shule ya Sekondari Sengerema kuanzia mwaka 1983.

Baada ya hapo akafanya kazi kama Mkemia katika Chama cha Ushirika cha Nyanza huko Mwanza hadi mwaka 1995.

Siasa
Nyota ya Magufuli liana kung’aa katika siasa, alipogombea na kushinda ubunge eneo la Chato mwaka 1995. Mwaka huo huo aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi, nafasi aliyohudumu hadi Mwaka 2000.

Baada ya uchaguzi Mwaka 2000, aliteuliwa kura Waziri wa Ujenzi, nafasi aliyohudumu hadi Mwaka 2006 alipohamishwa kwenda Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi alipokaa hadi Mwaka 2008.

Mwaka 2010, aliteuliwa kawa Waziri wa ujenzi kwa mara ya pili na kudumu kwenye nafasi hiyo hadi Mwaka 2015.

Urais
Mnamo Tarehe 12 Julai 2015, alichaguliwa kuwa mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Akiwa na Samia Suluhu Hassani kama mgombea mwenza.

Tarehe 29 Oktoba 2015 alitangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ushindi wa kura 8,882,935 sawa na 58.46%.

Magufuli aliapishwa kama Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 5 November 2015.

Muhula wa Pili
Mnamo tarehe 30 Oktoba 2020, Tume ya Uchaguzi Tanzania ilimtangaza John Pombe Magufuli kama rais kwa muhula wa pili kwa kupata kura milioni 12.5 hiyo ikiwa ni sawa na asilimia 84 akiwa amemshinda mshindani wake wa karibu, Tundu Lissu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Ameacha watoto 7 ambao ni Suzan, Edina, Joseph, Jesca, Ruth, Jurgen na Jeremiah.
Lakini pia mwanae mmoja aitwaye Juliana yeye alifariki.
Pia amemuacha mjane Janeth Magufuli.

Magufuli majina yake kamili ni John joseph pombe Magufuli mtoto wa Suzan.

Jina pombe alipewa na bibi yake likiwa ni Jina la utani lenye maana ya jina walwa yaani pombe katika lugha ya kisukuma.

Kwa sababu kipindi Magufuli anazaliwa bibi yake alikuwa akitengeneza pombe.


Simple and Clear,
What a history for our Fithy President Generous Man John Pombe Joseph Magufuli
May his soul rest in eternal peace
Thank you.
 
Baada ya magufuli kuwa,watanzania walizizima kwa kilio,wengine walizimia,lkn kwa sasa limetokea kundi linamshambulia jpm na kumwita majina yoote mabaya,
 
Baada ya magufuli kuwa,watanzania walizizima kwa kilio,wengine walizimia,lkn kwa sasa limetokea kundi linamshambulia jpm na kumwita majina yoote mabaya,
Hao wanatafuta kiki. Wameshindwa kuvaa viatu vya mwamba ni vikubwa.

Wataishia awamu hii hii. Mwamba aliwafungua macho watz.
RIP JPM
 
Back
Top Bottom