Historia ya Komandoo Tarimo

Historia ya Komandoo Tarimo

Thread yako haijatosheleza tueleze baada ya kupata mafunzo Cuba aliifanyia nini nchi yake hadi atambuliwe na jf maana kama ni makomandoo tunao wengi waliosoma CUBA, ISRAEL, URUSI, MAREKANI NA kwingineko Duniani kuna nini special juu ya huyu Tarimo wako? Kama hakuna nenda kwao watakupa kila kitu.

jamani mbona simfahamu hata mmoja?
 
Hans Poppe mambo yake yako vizuri sana sasa hivi. He has been able to fight his way up in business arena.
 
hivi makomando wanjulikana mpaka uweze andika histolia yake? ladba ya komando Salmini wa Unguja!
 
si ni wewe bana. ebu tuambie uko wapi na unafanya nn. ungekuwa msanii kama kanumba si ungekuwa mbali eeeeh? unajuta kuwa komando eeeeh! mara ya mwisho kupigana ilikuwa j3 ya pasaka eeeh! mwe long time aiseee.
 
labda muingie maktaba ya sheria hasa Mahakama Kuu kutafuta KESI YA UHAINI.Mtuhumiwa mmoja akiitwa Eugene Maganga ambaye aliandika simulizi zake kwenye gazeti la RAI mwishini mwa 1990s kwa kirefu, alifariki dunia mwaka 2010, huyu alikuwa Luteni wa JWTZ na wakati anakutwa na dhahama alikuwa akisoma shahada hapo UDSM.

Pengine simulizi hizi zingepatikana kule HABARI CORPORATION maana Maganga alipenda kuzifanya kitabu lakini mambo ya kiuchumi, na hata kukataliwa kwa kiwangio cha juu na jamii iliyomwona kuwa yeye ni haini kulizima ndoto za kuchapisha kitabu kabla mauti haijamaliza kila kitu.Pengine nduguzake wanazo cd alizorekodi masimulizi hayo
 
Uncle Tom alipigwa risasi na kuuawa siku moja kabla ya siku ambayo yangefanyika mapinduzi ya serikali ya Tanganyika.

Baada ya maiti yake kupekuliwa alikutwa na karatasi yenye majina ya viongozi mbalimbali wa jeshi pamoja na mawasiliano yao jambo ambalo liliwatia mashaka wana Usalama maana uncle Tom alikuwa most wanted na ilikuwa ishatolewa amri ya kukamatwa au kuuawa pale atakapoonekana ndani ya Tanganyika.

Ndipo ukaanza msako wa kukamata kila aliyeonekana kwenye ile karatasi na mpango mzima wa mapinduzi kuwa wazi....
aliyeuawa nni Tamimu pale pande za Mkwajuni kinondoni Uncle Tom au Pius Lugangira alitoroka ukonga au keko na akapelekea Wazir mambo ya ndani muda ule Brigedia Natepe kujiuzulu. Lugangira almefia UK
 
walikuwepo akina Vitalis Mapunda, chris Kadengo , zakaria (na nduguye)Hans pope,Eugene, Roberts,Tamin, Hatibu Gandi na wengineo raia walikwa Christopher Ngaiza, Zera Banyikwa etc
 
Back
Top Bottom