Historia ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda: Kilio Cha Mifereji ya Damu iendayo Ethiopia

Historia ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda: Kilio Cha Mifereji ya Damu iendayo Ethiopia

b3be33b9b0d2579a752b13387939edfa.jpg


KILIO CHA MIFEREJI YA DAMU IENDAYO ETHIOPIA



SEHEMU YA PILI





BAHUTU MANIFESTO



“Note sur l’aspect social du probleme racial indigene au Rwanda” (Waraka kuhusu maslahi ya kijamii ya Wazawa halisi wa Rwanda)



Katika sehemu iliyopita nilieleza kwa kifupi sana juu ya Waraka huu. Kwamba mwaka 1957 tarehe 24 March Wasomi wa kihutu na wahutu wenye ushawishi katika jamii ya Rwanda waliandaa waraka huu mahususi kutaka wahutukushika madaraka makuu ya uongozi nchini Rwanda. Hoja kuu ambayo waliijenga ni kwa kutumia nadharia waliyoiita “Statistical Law”. Kwamba wahutu ndio idadi kubwa zaidi ya raia wa Rwanda ambao ni 84% ya raia wote wa Rwanda huku watusi wakiwa ni asilimia 14 na Watwa 15 tu. Kwa hiyo kwa mujibu wao walihisi haikuwa sahihi kuwekwa kama raia wa daraja la pili na pia kuongozwa na kabila ambalo lina watu kiduchu zaidi ndani ya Rwanda.



Waraka huu wa kurasa kumi na wa kichokozi lakini uliojaa hoja nzito uliwasilishwa kwa Gavana wa Rwanda. Katika kurasa hizo kumi wasomi hao waling’aka vikali juu ya unyonyaji unaofanywa na Watusi dhidi ya Watu wakabila la Hutu.



Waraka huu pia ulisambazwa kwenye jamii. Ambako mkazo mkuu uliwekwa kwenye suala ambalo wenyewe waliita “double liberation”. Kwamba Wahutu wanahitaji ukombozi wa vitu viwili kwa mkupuo. Kwanza wanahitaji kujikomboakutoka kwenye makucha ya wakoloni wa kizungu na pili wanahitaji kujikomboa kutoka kwenye makucha ya Watusi.



Waraka huu ndio wenye mchango mkubwa zaidi ambao ulichangia kuweka msingi wa fikra na mtazamo wa Wahutu kuwaona Watusi kama watesi wao, wanyonyaji na wahamiaji kwenye eneo hilo. Pia waraka huu ndio ulifungua macho Wahutu wengi kuona tatizo kubwa la kijamii, kisiasa, na kichumi kutokana na mifumo yote hiyo kumilikiwa na watusi.



Waraka huu pia ndio ambao ulikuja kusababishwa kuzaliwa kwa amri kuu kumi za Wahutu mwaka 1990 (Ten Commandments of The Bahutu) ambazo nitaziongelea hapo baadae.





THE PURGE



Wengi wetu tunafahamu juu ya mauaji ya kimbari ambayo yalitokea mwaka 1994, lakini jambo ambalo wengi tunalisahau ni mfululizo wa matukio ya “kuisafisha Rwanda” ambayo yalitoka kwa muda wa takribani miaka thelathini mpaka kufikia kilele ambacho ndiyo mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.



Nitaeleza kwa ufupi…



Kama ambavyo nimetanabaisha hapo awali kwamba wahutu ni karibia 84% ya raia wote wa Rwanda. Kwa hiyo ulipotoka waraka wa “BAHUTU MANIFESTO” wakoloni wa kibelgiji walitikisika haswa.



Turudi nyuma kidogo…



Moja ya wanaharakati wa kupigania haki za wahutu ambao waliibuka katika miaka ya 1950s aliitwa Gregoire Kayibanda. Kama ilivyo kwa wasomi wengi wa kihutu, Kayibanda alipata elimu yake kutoka kwenye shule za seminari za wakatoliki japokuwa hakutaka kuwa padre. Alipomaliza elimu yake mwaka 1948 alifanya kazi ya ualimu wa shule ya msingi. Mwaka 1952 Kayibanda alipatiwa nafasi ya kuwa muhariri wa jarida la kanisa katoliki nchini Rwanda nafasi ambayo awali ilikuwa inashikiliwa na moja ya wanafalsafa muhimu zaidi nchiniRwanda aliyeitwa Alexis Kagame. Baadae pia alikabidhiwa jukumu la kuwa muhariri wa jarida lingine la kikatoliki lakini lenye mtazamo wa kihutu lilioitwa “Kinyamateka”.

Mwishoni mwa miaka ya 1950s alianzisha vuguvugu lake aliloliita “Mouvement Social Muhutu” (MSM).



Mwanaharakati mwingine wa kihutu aliyekuwa mahiri na maarufu zaidi katika kipindi hicho alikuwa anaitwa Joseph Gitera. Huyu naye alijipatia elimu yake kutoka shule a seminari za kikatoliki. Miaka hiyo hiyo ya 1950sGitera alianzisha chama chake cha siasa kilichoitwa “Association for Social Promotion of the Masses” (APROSOMA). Tofauti na wanaharakati wenzake wa kihutu mfano Bw. Kayibinda, yeye Gitera alikuwa mwanaharakati labda mwenye huruma kidogo lakini pia muda mwingine akiwa na mawazo ya “kihayawani” kabisa au labda tuseme ndoto za mchana. Harakati za Gitera hazikujikita kwenye masuala ya kikabila zaidi mwanzano, yeye alitilia mkazo zaidi kutetea haki za wananchgi masikini ambao walikuwa hawasikilizwi wala kukumbukwa ndaniya Rwanda. Gitera alikuwa ni moja kati ya wanaharakati wa mwanzo kabisa kutaka kuondoshwa kwa utawala wa kifalme nchini Rwanda.



Sasa basi…



Kitendo cha kuibuka kwa wanaharakati wa Kihutu wenye ushawishi ndani ya Rwanda kilianza kumtetemesha mfalme wa Rwanda pamoja na watusi wenye nyadhifa za ngazi za juu. Ili kujiweka katika nafasi salama, Mfalme waRwanda na wenzake walianza kupiga debe la Rwanda kupatiwa uhuru mara moja kutoka kwa Wabelgiji. Walichokuwa wanajiaminisha vichwani ni kwamba, kama Wabelgiji wataipatia uhuru Rwanda basi madaraka yote yataachwa kwa mfalme wa Rwanda na watu wake na hii inewaweka mahala salama kuendelea kuitawala Rwanda na Watusi kuwa Raia wa daraja la kwanza ndani ya Rwanda.



Mwaka 1956 Mfalme Rudahigwa pamoja na baraza lake la ushauri la “Conseil Superieur” walipendekeza kwa wabelgiji kuundwa kwa wizara za Fedha, Wizara ya Elimu, Wizara ya Kazi na Wizara ya Mambo ya Ndani na wakapendekeza watu wa kuongoza wizara hizo ambao wote walikuwa Watusi.


432cfea3e2e31ab56ac55fbe0b59fbbe.jpg

Mwanaharakati wa Kihitu Grogoire Kayibanda

Mwaka 1959 ili kuwafurahisha zaidi wahutu walio wengi, Wabelgiji walitangaza kwamba kuanzia mwaka huo Machifu watakuwa wanachaguliwa kwa kupigiwa kura na si kuteuliwa tena na Mfalme kama ambavyo ilikuwa awali.



Taarifa hii ilipokelewa kwa shangwe na vifijo na Wahutu lakini upande wa Watusi waliipinga vikali. Waltusi wiipinga kwa sababu kuu mbili. Moja, walihisi wanapokonywa tonge mdomoni kwa kuwa nafasi hizi za uchifuzilipokuwa zinateuliwa na Mfalme wote ambao walikuwa wanasimikwa kuwa machifu kwenye maeneo yote nchini Rwanda walikuwa ni Watusi kutokana na yeye mwenyewe Mfalme kuwa mtusi. Sababu ya pili, watusi waliohofia idadi kubwa ya wahutu. Hii ilimaanisha kwamba hakukuwa na tumaini lolote kwao kufua dafu kwenye sanduku la kura kwa sababu wahutu walikuwa ni wengi kupitiliza kuzidi wao.



Hili lilikuwa ni tishio kubwa kwa uhalali na uendelevu wa Ufalme wa Rwanda chini ya Watusi. Woga ambao ulimpata Mfalme Rudahigwa ulimfanya aanze kufanya mambo ya kipuuzi kabisa. Kwa mfano akaanza kutorosha ‘kalinga’(Ngoma kubwa za jadi ambzo ni moja ya ishara kuu za ufalme enzi hizo nchini Rwanda) akaanza kuzitoroshea kwenda nje ya Rwanda. Yote hii ilitokana na Gitera (yule aliyemdhalilisha) kuanzisha kampeni ya kutaka mfalme apokonywe ngoma hizo.

Baadae mfalme Rudahigwa akaanza tabia ya ulevi kupindukia ili kupunguza msongo ambao alikuwa nao kutokana na tishio lililoibuka la wahutu kuelekea kushika hatamu.

Baada ya misukosuko mingi ya msongo wa mawazo Mfalme Rudahigwa alifariki nchini Burundi eneo la Usumbura ambako alienda kutafuta tiba ya ‘celebral haemorrhage’. Japokuwa mpaka leo hii Watusi wengi bado wanaamini kwamba Mfalme wao Rudahigwa aliuwawa kwa kuchomwa sindano ya sumu na kanisa katoliki kwa kushirikiana na Wabelgiji.



Dhahania hii ilifanya vigogo wa Kitusi kuanza kampeni za kulipinga kanisa katoliki pamoja na uwepo wa Wabelgiji nchini humo. Hii iliwafanya pia pasipo kushauriana na Wabelgiji kama ilivyo desturi walimsimika Kigeli V Ndahindurwa ambaye ni ndugu yake yake marehemu Mfalme Rudahigwa kuwa mfalme mpya wa Rwanda.



Watusi wakaanzisha kampeni ya kuwataka Wabelgiji waachie uhuru wa Rwanda haraka kabla ya uchaguzi uliopangwa kufanyika mwishoni mwa mwaka 1959 kufanyika. Wakaunda na chama cha cha kuongoza vugu vugu hilo, ambacho walikiita “Union Nationale Rwandaise” (UNAR).

Kutokana na hasira UNAR walianza kufanya mambo ya kipuuzi ambayo yalisababisha chama hicho kupingwa kila kona sio tu kwa sababu ya kuwa chama cha kitusi tu. Mfano walianza kushinikiza somo la ‘European History’kuondolewa mashuleni. Walishinikiza pia wamishionari wote waondoke nchini Rwanda. Matokeo yake chama hiki cha kitusi cha UNAR kikajenga taswira kuonekana kama chama chenye kupinga ukristo na mahususi kupinga kanisa katoliki.



Hii ikasababisha kanisa katoliki kuanza kuunga mkono wazi wazi vyama vya kihutu kama vile APROSOMA cha Gitera.








47ab2ee1aab616c7b14268b424a7fa02.jpg

df62a81fd348e05e5b9df1368877778f.jpg

4a13a980b1043379f70b968a47544fa5.jpg

Mfalme Kigeli V wa Rwanda miaka ya 1950s

Wahutu wengine wanaharakati nao wakaona fursa hapa. Kwa mfano Kayibanda alisajili rasmi vuguvugu lake la MSM na kulifanya kuwa chma cha siasa ambacho alikiita “Parti du Mouvement de l’Emancipation Hutu” (PARMEHUTU).

Kayibanda na chama chake cha PARMEHUTU wakaanzisha kampeni za nchi nzima kutaka taifa linalojitegemea la kabila la Wahutu pekee.



Mpaka kufika mwezi octoba mwaka 1959 bunge lilikuwa limepitisha kuwa mwezi unaofuata Novemba ndipo uchaguzi ufanyike.



Wahutu walikuwa wanashangilia kwa vifijo kwa kuwa walikuwa wna uhakika wa ushindi kwenye uchaguzi kutokana na wingi wao. Lakini Watusi walikuwa wapo kwenye hofu kuu. Hali ya nchi ilikuwa tete haswa.



‘Wingu’ zito kabla ya ‘mvua’….



Siku ya tarehe 1 November mwaka 1959, Dominique Mbonyumutwa moja ya viongozi wa Kihutu ambaye pia alikuwa mwanaharakati wa chama cha PARMEHUTU akiwa na mkewe wakitokea kanisani mitaa ya Byimana, eneo la Gitarama alifuatwa na vijana wa chama cha kitusi cha UNAR ili atie sahihi barua inayopinga uwepo wa Wabelgiji nchini Rwanda. Yalitokea mabishano makali huku Mbonyumutwa akikataa kutia sahihi waraka huo. Mabishano haya yalisababisha vijana hawa wa UNAR kuanza kumpigaMbonyumutwa na mkewe. Baada ya kipigo kikali Mbonyumutwa na mkewe walifanikiwa kujiokoa na kutimua mbio mpaka nyumbani kwao. Lakini mitaani ukaanza kuenea uvumi kwamba vijana wa kitusi wa UNAR wamempiga mwanaharakati wa kihutu Mbonyumutwa na mkewe mpaka kumuua.



Taarifa hii iliyokuwa inaenea kwa kasi ilikuwa kama njiti ya kiberiti kwenye jamii ambayo tayari ilikuwa kwenye hali tete ya chuki iliyokuwa inatokota kwa miezi kadhaa. Siku hiyo hiyo vijana wa Kihutu nao wakaanzisha kampeni ya kuchoma moto nyumba za Watusi.

Mwanzoni yalianza kama maandamano ya kupinga kitendo cha Mbonyumutwa ‘kuuwawa’ lakini baadae maandamano hayo yaligeuka kuwa machafuko yenye lengo la kuchoma moto nyumba za watusi na kila mtusi ambaye alikuwa anataka kuwazuia vijana wa kihutu wasichome nyumba yake alikuwa anauwawa. Mwanzoni machafuko yalianzia kwenye eneo dogo la Ndiza lakini kufumba na kufumbua machafuko yalienea nchi nzima. Watusi wengi wakaanza kukimbilia Congo na Uganda ili kunusuru maisha yao.



Wabelgiji walikuwa wamenyamaza kimya kabisa wakiangalia Wanyarwanda wakiwa wanauana na kuchomeana nyumba moto. Walikuwa wanaogopa kuingilia mzozo huu kutokana na uwingi wa Wahutu. Kwa kipindi hiki Ubelgiji walikuwa na wanajeshi 300 tu ndani ya Rwanda. Kwa hiyo “wakaacha wafu wauane”. Machafuko yalipozidi na Watusi wengi kuwawa, Mfalme Kigeli aliomba ruhusa kwa Wabelgiji kuunda jeshi la dharura lakini wabelgiji walikataa kata kata. Walikuwa wanaogopa kuwapa silaha Mfalme(watusi) kwani walihisi ndio wangekuwa kama wana mwaga mafuta ya taa kwenye moto na kuukoleza zadi. Machafuko yangegeuka na kuwa mabaya zaidi.



Licha ya Wabelgiji kumnyima ruhusa Mfalme Kigeli kuunda jeshi la dharura lakini Kigeli alikaidi na kukusanya maelfu ya vijana wa kitusi na kuwapa silaha za jadi na












296c3541295c18cfad3d161b6f3088e1.jpg

f08ad2945977d91d59c2cfd54d7f2fd9.jpg

Machafuko ya mwaka 1959 nchini Rwanda


523e5f5865e92892f74718df9aa72d56.jpg

Watusi wakikimbia Rwanda kwenda Tanzania, Uganda na Congo



bunduki chache. Kigeli aliwapa amri ya kuwatafuta na kuua viongozi wote wa kihutu. Mamia ya viongozi wa kihutu waliuwawa. Moja ya hao walio uwawa alikuwa ni ndugu wa Gitera kiongozi wa APROSOMA. Mamia wenginewalikamatwa na kupelekwa kwenye ikulu ya Mfalme iliyoko Nyanza ambako waliteswa na kisha kuuwawa.



Kayibinda, kiongozi wa PARMEHUTU alikuwa mafichoni kusikojulikana kwa hiyo hakuweza kukamatwa. Gitera alijibu mapigo kwa kuunda jeshi lake pia. Siku ya tarehe 9 na tarehe 10 Novemba 1959 vikosi vya kitusi vya mfalme Kigeli vilivamia maeneo ya milima ya Save ambako ndiko kulikuwa na makazi ya Gitera. Mapambano makali yalitokea kati ya wahutu na vikosi vya mfalme Kigeli mpaka ambapo wabelgiji waliingilia kati kuzuia damu zaidi kumwagika.



Ili kuokoa jahazi, Gavana wa Rwanda na Burundi, Mbelgiji Jean-Paul Harroy alimuita nchini Rwanda kanali Guy Logiest ambaye alikuwa anaongoza majeshi ya Ubelgiji nchini Congo. Alipomuita alimpa jukumu moja tu, kurejesha amani na utulivu nchini Rwanda. Akampatia madaraka yote hata ya ‘ku-veto’ maamuzi ya Mfalme wa Rwanda.



Kanali Guy Logiest alikuja na falsafa rahisi tu. Aliamini wamba kadiri ambavyo Watusi wataendela kuwa wengi kwenye nafasi za utawala na kiserikali nchi hiyo kamwe haiweze kuwa na amni kwa kuwa wahutu ndio wengi zaidi. Ka hiyo akafanya mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa serikali. Akateua upya maafisa wote wa kiserikali na nafasi hizo karibia zote aliwapa wahutu tena wanachama wa PARMEHUTU.



Baadae zikaendeshwa kesi kuhusu waliosababisha machafuko nchi nzima mwezi Novemba. Viongozi wengi wa Kitusi walihukumiwa jela huku wenzao wahutu wakiachiwa huru.



Mwaka uliofuata yaani 1960, Kanali Guy Logiest aliitisha uchaguzi nchini humo licha ya Umoja wa Mataifa kupinga uchaguzi usifanyike kwani unaweza kusababisha upya machafuko. Lakini mwezi June na July uchaguzi ulifanyikana jumla ya viti 229 vilikuwa vinawaniwa. Matokeo ya mwisho yalipotangazwa chama cha watusi cha UNAR kiliambulia viti 19 kati ya viti vyote 229 huku chama cha wahutu cha PARMEHUTU wakijizolea viti karibia vyote vilivyobaki.



Mfalme Kigeli akavuliwa madaraka yote na kisha kuwekwa kizuizini nyumbani kwake kusini mwa Rwanda. Mwishoni mwa mwezi July alitoroka na kuanza kuishi kwa kuhama hama akizunguka nchi tofauti tofauti ndani ya AfrikaMashariki. Baadae alikimbilia nchini Marekani ambako aliishi mpaja kupatwa na umauti mwaka jana 2016 Octoba 16 akiwa na miaka 80.



July mwaka 1962 Rwanda ilijipatia Uhuru kamili huku PARMEHUTU kikiwa kama chama tawala na Kayibinda akiwa Rais.



Licha ya wahutu kushika madaraka na kuongoa nchi lakini bado mioyoni walikuwa wanafurukuta kwa visasi na vinyongo kutokana na kuhisi walinyanyaswa kwa miaka mingi sana na watusi. Kwahiyo mateso kwa watusi yaliendelea. Wahutu wengi walihisi kwamba watusi hawastahili kuwemo ndani ya Rwanda. ‘The purge’ ikaendelea.




21a67e6b5455ce0c9d486bc03caf9633.jpg

84108bbf94a45c92e0ce582b0ebe23d5.jpg

Mfalme Kigeli V akiwa nchini Marekani kabla ya kifo chake mwaka jana 2016 October



Hii iliwalazimu Watusi wengi kukimbia Rwanda kwenda Uganda, Congo na hapa kwetu Tanzania na kuwa wakimbizi. Wakiwa huko kwenye kambi za wakimbizi Watusi walianza kuunda vikundi vya wapiganaji ambavyo vilijulikana kama ‘inyezi’ (cockroaches (mende)). Vikundi hivi mara kwa mara vilivamia Rwanda kwa lengo la kutaka kufanya mapinduzi ili kurudisha utawala wa Kitusi, lakni hawakuwahi kufanikiwa wala kufua dafu mbele ya serikali ya PARMEHUTU. Sana sana walikuwa wanazidisha hasira za Wahutu dhidi ya Watusi wenzao ambao bado walibakia ndani ya Rwanda kuteswa, kunyanyaswa na kuuwawa.



Mpaka kufikia mwaka 1964 kulikuwa na karibia wakimbizi wa Kitusi 300,000 kwenye nchi za Congo, Uganda na hapa Tanzania.



Kutokana ma nchi ya Rwanda kutotulia kwa muda wote huu, mwaka 1973 yalitokea mapinduzi nchini Rwanda ambayo yalimuondoa madarakani Rais Gregoire Kayibanda na PARMEHUTU yake na kumingiza madarakati Rais mpya Juvenal Habyarimana.



Kitu cha haraka sana ambacho ni cha kukumbukwa ambacho alikifanya Rais mpya Juvenal Habyarimana ni kuituliza Rwanda. Chini yake miaka hiyo ya 1970s nchi ilitulia kabisa. Machafuko ya mara kwa mara yaliyokuwa yanatokea kwenye utawala uliopita yalikoma. Hata Watusi ambao walikuwa kwenye kambi za ukimbizi Uganda, Congo na Tanzania walianza kurejea. Juvenal Hibyarimana alionekana kama malaika wa ukombozi aliyetumwa kutoka mbinguni. Nchi ilitulia tuliii.!!



Lakini hawakujua… hawakujua kwamba ndani ya miaka michache ijayo Hibyarimana anaweza kuwa ndoto yao mmbaya zaidi kuwahi kuiota. Hawakujua kwamba shetani wa damu alikuwa ametua ndani ya Rwanda.!



Nchi ilitulia kabisa, na kila mtu alikuwa na tumaini jipya. Hata jamii ya kimatifa ilianza kumpongeza Hibyarimana kwa kuituliza Rwanda.

Lakini ulikuwa ni kama moto wa pumba za mpunga. Juu unaweza kuiona inapendeza kufaa hata kucheza ‘cha ndimu’ juu yake lakini kumbe chini kuna moto unatokota. Ilikuwa ni kama vile bwawa lenye maji yaliyotulia tuli kabisa kiasi kwamba hata ukidondosha punje ya mchanga unaweza kusikia inavyodondoka, lakini maji yenye utulivu mkubwa kiasi hiki ndiyo ambayo siku zote yana ‘chunusi’ ndani yake!



Kama kungelikuwa na mtu mwenye pua zenye ufanisi zaidi… labda angeliweza kusikia harufu ya damu kwa mbali ikiinyemelea Rwanda…!



e2766d127057c80b8764e10064075be7.jpg

Rais Juvenal Hibyarimana



Itaendelea…



THE BOLD
To Infinity and Beyond
0718 096 811 (Whatsapp Only)
 
Back
Top Bottom