Historia ya Mkata utepe wa kisiwa cha kusadikika aliyepotea ghafla alikuwa akikabidhiwa majukumu mazito ya kushika usukani mwanzoni mwa kalenda mpya

Nimekupata barabara kabisa
 
Hiyo umeitengeneza au ni habari ya kweli?

Unamaanisha malkia hatogombea?

Kwa hiyo mfalme mtarajiwa yu mzima wa afya tele, na atarejeabaada ya miezi mitatu?

Kwa hiyo yupo nje kwaajili kufunzwa namna ya kuendesha nchi?
Sio hatogombea ila hatofikia siku ya ugombeaji, kwa andiko hili habari yake inaisha mwaka huu ndio maana kasema muongo mmoja na miaka miwili. Let's wait and see
 
Mleta mada unamaanisha trend itaendelea?
2022 mwanzoni Supika kama Supika aliandika barua ya kujitengua na akatenguka.

2022 mwishoni ikaletwa mada humu kwamba mfukunyuzi mkuu atatenguliwa mwaka 2023 mwanzoni, kweli mwezi wa kwanza 2023 mkuu wa wafukuzi wa nyeti nyeti akatenguka.

2023 mwishoni unaleta mada ya dizaini hii.

Ngoja tusubiri majibu ya muda.
 
Hata mtarajiwa wa Zanzibar 2020 alipoteaga lakini leo ndio mfalme Zenji

Siasa ni Sayansi 😂
 
Wapiga Ramli Chonganishi wanazidi kuendelea na kazi yao.
 
Kikubwa zaidi kwetu ni kujua kama huyo Mkata utepe ni Mzima! Hayo mengine siyo ya muhimu!
Niseme tu kama ni hilo limeshajulikana! Anaweza asipewe kibali cha kuongoza kisiwa!
 
Hivi sheria ya kuiwakikisha nchi nje ya nchi kwa mikutano au kazi maalumu kwa viongozi wetu wakuu haina muda maalumu? Kiongozi anaweza kuchukua per diem za siku ngapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…