Historia ya Mkata utepe wa kisiwa cha kusadikika aliyepotea ghafla alikuwa akikabidhiwa majukumu mazito ya kushika usukani mwanzoni mwa kalenda mpya

Historia ya Mkata utepe wa kisiwa cha kusadikika aliyepotea ghafla alikuwa akikabidhiwa majukumu mazito ya kushika usukani mwanzoni mwa kalenda mpya

Uchawi hauvuki maji, ukijaribi kuuvusha, unakuua wewe mwenyewe au unaufikisha ukiwa hauna nguvu, sababu kubwa, bahari Ina makazi ya viumbe wakubwa ambao wataunusa na kukufata katika mashua, na kuuliza kwa nini unapitisha mazingara na ushirikina katika himaya yao. Hapo kuna mawili, waipindue mashua, au waivunje nguvu dawa uliyobeba, au mafundi wafanye tambiko katikato ya bahari au ziwa.

Visiwa vinalindwa na hao viumbe.

Usimjaribu mtu wa visiwani kwa uchawi wa bara, utakwisha.
Nimekupata barabara kabisa
 
Hiyo umeitengeneza au ni habari ya kweli?

Unamaanisha malkia hatogombea?

Kwa hiyo mfalme mtarajiwa yu mzima wa afya tele, na atarejeabaada ya miezi mitatu?

Kwa hiyo yupo nje kwaajili kufunzwa namna ya kuendesha nchi?
Sio hatogombea ila hatofikia siku ya ugombeaji, kwa andiko hili habari yake inaisha mwaka huu ndio maana kasema muongo mmoja na miaka miwili. Let's wait and see
 
Mleta mada unamaanisha trend itaendelea?
2022 mwanzoni Supika kama Supika aliandika barua ya kujitengua na akatenguka.

2022 mwishoni ikaletwa mada humu kwamba mfukunyuzi mkuu atatenguliwa mwaka 2023 mwanzoni, kweli mwezi wa kwanza 2023 mkuu wa wafukuzi wa nyeti nyeti akatenguka.

2023 mwishoni unaleta mada ya dizaini hii.

Ngoja tusubiri majibu ya muda.
 
Mleta story unajifanya kuleta mafumbo kama kuongoza nchi hii kunahitaji akili nyingi sana. Hapa jeshi linatii rais yoyote aliye madarakani bila kujali kaingia vipi madarakani. Kwamba sijui kaenda wapi kufanya Nini, na nani ana Siri nyingi ni upuuzi mtupu.
Hata mtarajiwa wa Zanzibar 2020 alipoteaga lakini leo ndio mfalme Zenji

Siasa ni Sayansi 😂
 
Alikuwepo Mkata utepe mmoja aliyetokea Magharibi mwa kisiwa cha Kusadikika alikuwa mpole, mnyenyekevu na asiye na makuu yeye alijua tu kufanya kazi katika wafalme mbali mbali wa kisiwa hicho kilichoko mashariki mwa bara la giza

Umaarufu wa Mkata utepe ulivuma Sana alipopewa kazi ya kutunza kibubu cha kisiwa hicho kwani mfalme wa wakati huo alimwamini Sana kwa misimamo yake ya kutoyumba na uaminifu mkubwa

Baada ya Muda Mfalme yule alitwaliwa kwa Mwenye nguvu zote na Duniani na ulimwenguni na baadaye akaja malkia kama Mrithi wa kisiwa cha Kusadikika.

Malkia yule alimpa kazi ya kukata utepe na wazee wa kisiwa kile walimwambia Malkia kuwa mwanzoni mwa kalenda mpya Malkia inabidi Amwachie kiti cha enzi yule Mkata utepe na hatimaye mkata utepe awe mfalme wa kisiwa cha kusadikika kwa mwaka muongo 1 na miaka 2

Lakini kabla ya mkata utepe yule hajapewa majukumu ya kuwa mfalme wa kisiwa cha kusadikika ilibidi akutane kwanza na wazee wa enzi kumpa nguvu na kumuonyesha njia sahihi na namna ya kuongoza kile kisiwa cha kusadikika

Mfalme huyu alitokea baada ya masaa zaidi ya 2000 na tukio lile lilikuja kuwaacha Hoi waliokuwa wanaulilia ufalme wa kisiwa cha kusadikika na wategemezi wa Malkia aliyejaa siri nyingi na nzito waliangua kilio na walizimia baadhi yao kujiua

Hiyo ilikuwa ni Hadithi ya Kisiwa cha Kusadikika
Wapiga Ramli Chonganishi wanazidi kuendelea na kazi yao.
 
Kikubwa zaidi kwetu ni kujua kama huyo Mkata utepe ni Mzima! Hayo mengine siyo ya muhimu!
Niseme tu kama ni hilo limeshajulikana! Anaweza asipewe kibali cha kuongoza kisiwa!
 
Hivi sheria ya kuiwakikisha nchi nje ya nchi kwa mikutano au kazi maalumu kwa viongozi wetu wakuu haina muda maalumu? Kiongozi anaweza kuchukua per diem za siku ngapi?
 
Back
Top Bottom