Historia ya Qur'an

Historia ya Qur'an

Mtibeli kama una majibu naomba tafadhali

Hilo eneo la Makka na Madina kwa karne hizo liligubikwa na ibada ya miungu zaidi ya 360 ambayo iliwekwa hapo Alkaaba.
Huyo Allah mwenyewe kwa zama hizo alikuwa na watoto watatu.

Muhammad yeye kutokana na uswahaba wake na Wakristo akiwemo huyo Waraqa ndiye alibadili mwelekeo wa hayo madudw.

Ila hakukuwa na Uislamu kabla ya MUHAMMAD
 
Mtume alikuwa Muislam kwa miaka 23 (kuanzia miaka 40 hadi 53)..Mimi naomba kujibiwa maswali yafuatayo:

1. Tangu kuzaliwa kwake Mtume hadi alipofika umri wa miaka 40 alikuwa anaabudu wapi?
2. Mungu wake alikuwa nani?
3. Kibla chake kilikuwa wapi?
4. Msikiti wake ulikuwa wapi?
5. Utaratibu wake wa kuswali ulikuaje?
6. Alikuwa akifunga Ramadhan? (Ilikuwa na maana gani kwake?
7. Alikuwa akienda kuzunguruka Kabah? Je Kabah Ilikuwa na midoli au haikuwa nayo?

mgen
Che mittoga
Mimi sioni kama kuna haja ya muda huu kujudge kuhusu maswala ya kiimani katika upande huu wa kidini.!
Kila mtu abaki na dini yake au Aamini anachokiamini.

1)Mtume Muhammad S.A.W kupewa utume akiwa na miaka 40 ilikua ni hekma aliyoitumia Mwenyezi Mungu.kwani kumpa katika umri huo wa miaka 40 kikawaida hata akili ya mtu inakuwa imekomaa kisawasawa na kutambulika ni mtu mzima na mpembuzi wa mambo.
Pia katika swala ilo la kiimani yalitokea mengi hivyo ilihitaji mtu ambae atakua tayari ni matured.! Na kuabudu ukisoma historia katika SIRA Muhammad S.A.W hakuwa akijihusisha na ibada yoyote iliyokua ikiendelea kipindi kile(ibada kuu-kuabudu masanamu,moto,jua,mwezi,wanyama nk) vitu ambavyo hata wewe ndugu yangu sio rahisi kukubadili kuviabudu ambayo vingine mwanadamu mwenyewe alishiriki kuvitengeneza.
Hivyo Muhammad S.A.W mara nyingi alikua akijitenga na kuwa mwenyewe katika sehemu pweke.
2) Mungu wake alikua Allah
03)swala la kibla lilikuja baada ya mtume kukakabidhiwa swala ambazo leo waislam tunaziswali kutwa mara 5 na katika historia ya Kibla hivyo kipindi hiko yeye hakuwa na Kibla
04) hakuwa na msikiti(elewa jibu no 1 na no 3)


05)hakuwa na utaratibu kabla hajapewa kitabu (Quran)
06)hakuwa akifunga Ramadhan kabla hajapewa kitabu (Quran)
07)hakuzuru Kaabah kabla hajapewa kitabu (Quran) na unaposema kulikua na midoli ama lah.? Unamamisha nini masanamu au.?
Kama ni masanamu yalikuwepo kabla ujinga ukiwa unatawala sana katika eneo lile kabla Muhammad S.A.W hajapewa Utume.!

Nawasilisha
 
Hilo eneo la Makka na Madina kwa karne hizo liligubikwa na ibada ya miungu zaidi ya 360 ambayo iliwekwa hapo Alkaaba.
Huyo Allah mwenyewe kwa zama hizo alikuwa na watoto watatu.

Muhammad yeye kutokana na uswahaba wake na Wakristo akiwemo huyo Waraqa ndiye alibadili mwelekeo wa hayo madudw.

Ila hakukuwa na Uislamu kabla ya MUHAMMAD
Wewe unaongea kutokana na uelewa wako jinsi ulivyo.!
Katika mafundisho ya Dini ya kiislam.
Uislam upo toka Enzi nabii Adam anaumbwa na ndio nabii wa kwanza katika historia ya manabii wa kiislam.
Tunapoweka mezani nadharia ya uumbwaji wa binadamu chanzo chake kikiwa ni Kuumbwa na Mungu basi sisi Waislam tunaamini kuwa Adam ndio chanzo cha sisi wote tuliomo ulimwenguni.
Uislam upo tangu Kipindi cha Adam na Hawa. Na manabii/mitume wengi walikuja kuutangaza Uislam kabla ya Muhammad.
Muhammad yeye ndio Mtume wa mwisho na hakuna mwingine baadae yake yeye.!
Sisi waislam ndio tunaamini ivyo.
Wewe icho ulichoeleza ni mtazamo wako...
 
Hilo eneo la Makka na Madina kwa karne hizo liligubikwa na ibada ya miungu zaidi ya 360 ambayo iliwekwa hapo Alkaaba.
Huyo Allah mwenyewe kwa zama hizo alikuwa na watoto watatu.

Muhammad yeye kutokana na uswahaba wake na Wakristo akiwemo huyo Waraqa ndiye alibadili mwelekeo wa hayo madudw.

Ila hakukuwa na Uislamu kabla ya MUHAMM

Hilo eneo la Makka na Madina kwa karne hizo liligubikwa na ibada ya miungu zaidi ya 360 ambayo iliwekwa hapo Alkaaba.
Huyo Allah mwenyewe kwa zama hizo alikuwa na watoto watatu.

Muhammad yeye kutokana na uswahaba wake na Wakristo akiwemo huyo Waraqa ndiye alibadili mwelekeo wa hayo madudw.

Ila hakukuwa na Uislamu kabla ya MUHAMMAD
Allah hakuwa na watoto,na wala hatawahi kuja kuwa nao.hajazaa wala hajazaliwa na wala hakuna anaefanana nae.

Chanzo (Quran Surah Tul al Ikhlas)
 
Mimi sioni kama kuna haja ya muda huu kujudge kuhusu maswala ya kiimani katika upande huu wa kidini.!
Kila mtu abaki na dini yake au Aamini anachokiamini.

1)Mtume Muhammad S.A.W kupewa utume akiwa na miaka 40 ilikua ni hekma aliyoitumia Mwenyezi Mungu.kwani kumpa katika umri huo wa miaka 40 kikawaida hata akili ya mtu inakuwa imekomaa kisawasawa na kutambulika ni mtu mzima na mpembuzi wa mambo.
Pia katika swala ilo la kiimani yalitokea mengi hivyo ilihitaji mtu ambae atakua tayari ni matured.! Na kuabudu ukisoma historia katika SIRA Muhammad S.A.W hakuwa akijihusisha na ibada yoyote iliyokua ikiendelea kipindi kile(ibada kuu-kuabudu masanamu,moto,jua,mwezi,wanyama nk) vitu ambavyo hata wewe ndugu yangu sio rahisi kukubadili kuviabudu ambayo vingine mwanadamu mwenyewe alishiriki kuvitengeneza.
Hivyo Muhammad S.A.W mara nyingi alikua akijitenga na kuwa mwenyewe katika sehemu pweke.
2) Mungu wake alikua Allah
alimjuaje huyo allah kabla ya kuelezewa na korani
03)swala la kibla lilikuja baada ya mtume kukakabidhiwa swala ambazo leo waislam tunaziswali kutwa mara 5 na katika historia ya Kibla hivyo kipindi hiko yeye hakuwa na Kibla
04) hakuwa na msikiti(elewa jibu no 1 na no 3)
alikuwa anaswali wapi
05)hakuwa na utaratibu kabla hajapewa kitabu (Quran)
06)hakuwa akifunga Ramadhan kabla hajapewa kitabu (Quran)
07)hakuzuru Kaabah kabla hajapewa kitabu (Quran) na unaposema kulikua na midoli ama lah.? Unamamisha nini masanamu au.?
Kama ni masanamu yalikuwepo kabla ujinga ukiwa unatawala sana katika eneo lile kabla Muhammad S.A.W hajapewa Utume.!

Nawasilisha
Mkuu kwanini hutaki kukiri kuwa kabla ya Mohamad na korani yake hakujawahi kuwa na uislam
tupe pia historia ya uislam
 
Baadhi ya waandishi na wazungumzaji wanazinukuu aya za Qur’an Tukufu nje ya muktadha wake na kujaribu kuulaumu Uislamu kwa kueneza vurugu na ugaidi. Wanachukua maandishi na wanayatumia nje ya “muktadha” wake.

Ni sawasawa kabisa na mtu anayetafuta ndani ya Biblia na kuchukua maneno au sentensi zifuatazo ili kuthibitisha kwamba Biblia inaendeleza vurugu:

“Chukua viongozi wote wa watu hawa na uwauwe.” (Hesabu 25:7)

“Sasa wauwe watoto wa kiume wote. Na muue kila mwanamke ambaye amelala na mwanaume, lakini muacheni kila msichana ambaye hajalala na mwanaume kamwe.” (Numbers 31:17-18)

“Muue kila mwanaume na kila mwanamke ambaye sio bikira.” (Waamuzi – 21:11)


Hakuna mtu mwenye akili timamu atakayekubali uwasilisho wa “nje ya muktadha” kama huo wa mistari ya Biblia. Hata hivyo, bado tunawaona wainjilisti na wahubiri wengi wa Kikristo wakifanya hivyo hivyo hasa kwenye Qur’an bila hata kusita kokote kule.

Hivyo hebu tuangalie baadhi ya mifano ya kuchukua “maneno” ya Qur’an Tukufu nje ya “muktadha” wake.

Mfano wa kwanza

Sura ya 2 aya ya 191 inanukuliwa kama ifuatavyo:

“Waueni popote mtakapowakuta.”

Ili kuuelewa muktadha kamili wa aya hii, soma kuanzia aya ya 190 hadi 193 kwa pamoja zote:

“Na wapigeni vita katika njia ya Mwenyezi Mungu wale ambao wanakupigeni vita, wala msiruke mipaka, hakika Mwenyezi Mungu hawapendi warukao mipaka. Na wauweni popote muwakutapo, na muwatoe popote pale walipowatoeni, na fitna ni mbaya zaidi kuliko kuua. Wala msipigane nao katika Msikiti Mtukufu mpaka wao wawapigeni ndani yake. Na ikiwa watakupigeni basi nanyi pia wapigeni, kama hiyo ndio malipo kwa makafiri. Lakini watakapokoma, basi (waacheni) hakika Mwenyezi Munguni mwingi wa kusamehe, mwenye kurehemu. Na wapigeni mpaka pasiwepo na mateso, na dini iwe ni ya Mwenyezi Mungu peke yake, watakapokoma basi pasiwepo na uadui ila dhidi ya madhalimu.”

Muktadha huu unafafanua kwamba ile aya ya 191 inawaruhusu Waislamu wa Madina kujihami wenyewe kiulinzi dhidi ya uchokozi na uvamizi wa makafiri wa Makkah. Kwa hakika haisemi kwamba waende wakipita duniani kote ili kumuua kila kafiri watakayemkuta!

Mfano wa pili

Sura ya 4, aya ya 74 ambayo inadhaniwa kwamba inahimiza umwagaji damu:

“Basi wapigane katika njia ya Mwenyezi Mungu wale wanaouza maisha (yao) ya dunia kwa akhera. Na anayepigana katika njia ya Mwenyezi Mungu akauawa au akashinda, basi hivi karibuni tutampa malipo makubwa.”

Wale wanaoinukuu aya hii, kwa manufaa yao, kwa urahisi tu wanaiacha ile aya inayofuatia ya 75 ambayo inaelezea lengo na uhalali wa hii Jihadi ndogo.

“Na mna nini, hampigani katika njia ya Mwenyezi Mungu, na wale wanaoonewa katika wanaume na wanawake na watoto ambao husema: Mola wetu! Tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhalimu, na utujaalie mlinzi kutoka kwako, na utujaalie msaidizi kutoka kwako…………”

Aya hii dhahiri kabisa inawahimiza Waislam kusimama kwa ajili wanaume, wanawake na watoto wanaonewa.

Hivi dini za kimungu zisiwatetee wanaume, wanawake na watoto wanaoonewa?

Mfano wa tatu

Sura ya 9, aya ya 12: “Basi wauweni viongozi wa ukafiri.”

Hii ni sehemu tu ya fungu zima la maneno ambamo Mwenyezi Mungu anazungumzia kuhusu Waislam huko Madina na mkataba wao wa makubaliano ya kusimamisha mapigano na makafiri wa Makkah. Tazama aya ya 12 -14:

“Na kama wakivunja viapo vyao baada ya kuahidi kwao na wakatukana dini yenu, basi wauweni viongozi wa ukafiri kwani viapo vyao havina maana ili wapate kujizuia. Je, hamtapigana na watu waliovunja viapo vyao na wakafunga nia ya kumfukuza Mtume, nao ndio waliokuanzeni mara ya kwanza? Je mnawaogopa? Basi Mwenyezi Mungu anastahiki zaidi mumuogope, ikiwa nyinyi mmeamini. Peganeni nao, Mwenyezi Mungu atawaadhibu kwa mikono yenu, na awahuzunishe na akunusuruni juu yao na avipoze vifua vya waumini aondoe ghadhabu ya nyoyo zao, na Mwenyezi Mungu humkubalia toba ampendaye, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye hekima.”

Muktadha huu kwa uwazi kabisa unatoa haki ya kujihami kwa Waislam, bali kwa hali yoyote ile, hautangazi uchokozi.

Mfano wa Nne

Sura ya 9, aya ya 36: “Na nyote piganeni na washirikina.” Kwa kweli, msitari huu ni sehemu ya aya nzima ambamo Mwenyezi Mungu anazungumzia kuhusu utakatifu wa miezi minne kati ya miezi yote kumi na mbili, ambamo kupigana kumekatazwa. Kisha inasema:

“Na piganeni na washirikina kwa pamoja kama wao wote wanavyopigana nanyi, na jueni kwamba Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wanao muogopa.”

Wale wanaopenda kuzichukua aya za Qur’an Tukufu nje ya muktadha wake kwa faida yao wanaiacha ile sehemu “kama wao wote wanavyopigana nanyi.” Kama unavyoona, aya hii pia inatoa majibu kwa ule uchokozi ulioanzishwa na washirikina dhidi ya Waslamu; haizungumzii juu ya kuanza vita.

c) Hitimisho

Kutokana na mifano hii, ni dhahiri kabisa kwamba Uislam hauzungumzii juu ya Jihadi ndogo kwa ajili ya uchokozi; bali inawaruhusu Waislam kujilinda kivitendo maisha yao, mali zao na ardhi zao dhidi ya uchokozi wowote ule, na pia kupigana kwa ajili ya kukomesha udhalimu dhidi ya wanaume, wanawake na watoto wanaoonewa.

Zile aya kuhusu waabudu masanamu wa Makkah zenyewe ni makhsusi sana na zilizohusika kwa kipindi kile tu. Hebu tuangalie tena ile sura ya 22, aya ya 39 hadi 40:

“Imeruhusiwa kupigana kwa wale wanaopigwa kwa sababu wamedhulumiwa, na kwa hakika Mwenyezi Mungu anao uwezo wa kuwasaidia. Ambao wametolewa majumbani mwamo pasipo haki ila kwa sababu wanasema Mola wetu ni Mwenyezi Mungu. Na kama Mwenyezi Mungu asingeliwakinga watu baadhi yao kwa wengine, bila shaka yangelivunjwa mahekalu na makanisa, masinagogi na misikiti ambamo jina la Mwenyezi Mungu hutajwa kwa wingi. Na bila shaka Mwenyezi Mungu humsaidia yule anayemsaidia Yeye. Hakika MwenyeziMungu ni Mwenye nguvu Mtukufu.”

Uislamu unashughulika na jamii ya mwanadamu yenye uhalisia na sio ya kidhanifu. Katika maneno ya Dr. Sayyed Hussain Nasr, “Waislam wanayaona maadili ya Kikristo ni adhimu sana kwa wanadamu wa kawaida kuweza kuyafuata; inaelekea kwamba ile amri ya sheria ya kugeuza shavu la pili ilikuwa ikilengwa kwa watakatifu tu. Wakristo kwa karne nyingi hawakuonyesha kujizuia katika vita kuliko watu wasiokuwa Wakristo. Wazo lililohubiriwa na utaratibu uliofuatwa vimekuwa wakati mwingi havihusiani.” 2

Tumalizie na Sura ya 109 ya Qur’an Tukufu:

“Sema: Enyi makafiri! mimi siabudu mnachokiabudu, wala ninyi hamuabudu ninayemuabudu. Wala sitaabudu mnachoabudu. Wala ninyi hamtaabudu ninayemuabudu. Ninyi mna dini yenu nami nina dini yangu.”
Nimeipenda hii
 
Hilo eneo la Makka na Madina kwa karne hizo liligubikwa na ibada ya miungu zaidi ya 360 ambayo iliwekwa hapo Alkaaba.
Huyo Allah mwenyewe kwa zama hizo alikuwa na watoto watatu.

Muhammad yeye kutokana na uswahaba wake na Wakristo akiwemo huyo Waraqa ndiye alibadili mwelekeo wa hayo madudw.

Ila hakukuwa na Uislamu kabla ya MUHAMMAD
Huna unalolojua na hii inaongesha huna elimu
 
KatetiMQ nakupa ushauri mmoja, jikite zaidi kwenye mada yako,,, na jibu hoja tu ambazo unaona zina hekima na Busara kwasababu kwa uzoefu wa mambo haya ya dini ubishani wa kipuuzi ni mwingi mno.

Pili jifunze kuwapuuza baadhi ya watu kwani ni wapuuzi mno wanajifanya wanajua kumbe hawana wanachojua

Asante
Sahihi
 
HISTORIA YA QUR'AN.

Sehemu ya Pili(2).

Katika Sehemu ya Pili ya Historia ya Qur'an tutaangalia Sura zilizoshuka Makka na Madina Kama ifuatavyo.... 👇

SURA ZA MAKKA NA MADINA

Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina.

Sura za Makka ni zile zilizomshukia Mtume (s.a.w) katika kipindi cha Utume cha Makka kilichodumu kwa miaka 13. Maudhui ya sura za Makka kwa kiwango kikubwa yamejikita katika kujenga imani za watu kwa kutoa hoja madhubuti zilizozingatia mazingira ya wakazi wa Makka wa kipindi hicho. Muundo wa sura za Makka ni ule wa kishairi. Nyingi ya sura za Makka zimeundwa na aya fupi zenye kufikisha ujumbe moja kwa moja kwa mtindo wa kishairi uliozingatia mazingira ya watu wa Makka wa wakati ule.

Katika siku za mwanzo za kushuka kwa Qur-an, watu wa Makka walidhania kuwa Qur-an ni mashairi aliyotunga Muhammad (s.a.w), lakini baada ya kupitia aya zake kwa makini, kama alivyofanya bingwa wa washairi wa wakati huo, Labiid bin Rabiah, na baada ya kushindwa kutoa angalau sura moja mithili ya sura ya Qur-an, kimaudhui na kimuundo, ilidhihiri wazi kuwa Qur-an si mashairi bali ni Wahy kutoka kwa Allah (s.w).

Sura za Madina ni zile zilizomshukia Mtume (s.a.w) baada ya kuhamia Madina katika kipindi cha pili cha Utume wake kilichodumu kwa miaka 10.

Maudhui ya sura za Madinah yamejikita kwenye kuunda na kuendesha Dola ya Kiislamu. Nyingi ya sura za Madina zina aya ndefu zenye kufafanua mambo kwa uwazi ili kuwawezesha Waislamu kutekeleza wajibu wao katika kusimamisha na kuhami dola ya Kiislamu. Pia aya nyingi za Madina zimeshehenezwa na maamrisho na makatazo mbali mbali ili kuunda jamii imara itakayoweza kusimamisha Ukhalifa katika ardhi.

Inaendelea, InshaaAllah

Allah Ni Mjuzi Zaidi.
 
KatetiMQ nakupa ushauri mmoja, jikite zaidi kwenye mada yako,,, na jibu hoja tu ambazo unaona zina hekima na Busara kwasababu kwa uzoefu wa mambo haya ya dini ubishani wa kipuuzi ni mwingi mno.

Pili jifunze kuwapuuza baadhi ya watu kwani ni wapuuzi mno wanajifanya wanajua kumbe hawana wanachojua

Asante
Nashukuru kinachoniudhi wamejikita kwenye dhihaka sio kujifunza
 
Kabla ya kushushiwa quran muhamad alikua anamuabudu Mungu kwa taratibu zipi kumbuka taratibu zote za kusali za uislamu zimetoka na quran aliyoshushiwa
Hapana Ila nitakupa maele
Walikuwa wana

Hilo eneo la Makka na Madina kwa karne hizo liligubikwa na ibada ya miungu zaidi ya 360 ambayo iliwekwa hapo Alkaaba.
Huyo Allah mwenyewe kwa zama hizo alikuwa na watoto watatu.

Muhammad yeye kutokana na uswahaba wake na Wakristo akiwemo huyo Waraqa ndiye alibadili mwelekeo wa hayo madudw.

Ila hakukuwa na Uislamu kabla ya MUHAMMAD
036.Je, Uislamu ulikuwepo kabla Mtume Muhammad s.a.w?

Naam, ulikuwepo kabla,Uislamu ndiyo Msingi ambao kila mteule wa Mungu Mwenyezi alikuwa akiwahubiria watu wake,kila Zama ilikuwa Ni juu ya watu kutakiwa wasilimu,
Ukisoma hapa utaona Quran.com/4/163 quran.com/42/13

Sasa Soma hapa

127. Na kumbukeni Ibrahim na Ismail walipo inyanyua misingi ya ile Nyumba wakaomba: Ewe Mola Mlezi wetu! Tutakabalie! Hakika Wewe ndiye Msikizi Mjuzi.



128. Ewe Mola Mlezi wetu! Tujaalie tuwe ni wenye kusilimu kwako, na pia miongoni mwa vizazi vyetu wawe umma ulio silimu kwako. Na utuonyeshe njia za ibada yetu na utusamehe. Bila shaka Wewe ndiye Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.



129. Ewe Mola Mlezi wetu! Waletee Mtume anaye tokana na wao, awasomee Aya zako, na awafundishe Kitabu na hikima na awatakase. Hakika Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.



130. Na nani atajitenga na mila ya Ibrahim isipo kuwa anayeitia nafsi yake katika upumbavu? Na kwa yakini Sisi tulimteuwa yeye katika dunia; na hakika yeye katika Akhera atakuwa miongoni mwa watu wema.



131. Na Mola wake Mlezi alipo mwambia: Silimu, Nyenyekea! Alinena: Nimesilimu, nimenyenyekea kwa Mola wa walimwengu wote.



132. Na Ibrahim akawausia wanawe, na pia Yaaqub: Enyi wanangu! Hakika Mwenyezi Mungu amekuteulieni Dini hii; basi msife ila nanyi mmekuwa Waislamu, wanyenyekevu.



133. Je! Mlikuwapo yalipo mfikia Yaaqub mauti, akawaambia wanawe: Mtamuabudu nani baada yangu? Wakasema: Tutamuabudu Mungu wako na Mungu wa baba zako, Ibrahim na Ismail na Is- hak, Mungu Mmoja tu, na sisi tunasilimu kwake.



134. Hao ni watu walio kwisha pita. Watapata waliyo yachuma, nanyi mtapata mtakayo yachuma; wala hamtaulizwa nyinyi waliyo kuwa wakiyafanya wao.



135. Na wakasema: Kuweni Mayahudi au Wakristo ndio mtaongoka. Sema: Bali tunashika mila ya Ibrahim mwongofu, wala hakuwa katika washirikina.



136. Semeni nyinyi: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyo teremshiwa sisi, na yaliyo teremshwa kwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yaakub na wajukuu zake, na waliyo pewa Musa na Isa, na pia waliyo pewa Manabii wengine kutoka kwa Mola wao Mlezi; hatutafautishi baina ya yeyote katika hao, na sisi tumesilimu kwake.



137. Basi wakiamini kama mnavyo amini nyinyi, itakuwa kweli wameongoka. Na wakikengeuka basi wao wamo katika upinzani tu. Na Mwenyezi Mungu atakutosheni kukukingeni na shari yao, na Yeye ndiye Msikizi, Mjuzi.



138. Huko ndiko kupaka rangi kwa Mwenyezi Mungu, na nani aliye mbora wa kupaka rangi kuliko Mwenyezi Mungu? Na sisi ni wenye kumuabudu Yeye tu.



139. Sema: Mnahojiana nasi juu ya Mwenyezi Mungu, naye ni Mola wetu Mlezi na Mola wenu Mlezi, na sisi tuna vitendo vyetu na nyinyi mna vitendo vyenu? Nasi tunamsafia Yeye tu.



140. Au mnasema kuwa Ibrahim na Ismail na Is-hak na Yaakub na wajukuu zao walikuwa Mayahudi au Wakristo? Sema: Je, nyinyi mnajua zaidi au Mwenyezi Mungu? Na ni nani mwenye kudhulumu zaidi kuliko yule aliye ficha ushahidi alio nao utokao kwa Mwenyezi Mungu? Na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na hayo myafanyayo.



141. Hao ni watu walio kwisha pita. Wao watapata waliyo yachuma, na nyinyi mt apata mliyo yachuma, wala hamtaulizwa nyinyi yale waliyo kuwa wakifanya wao.

Quran 2
 
Back
Top Bottom