Hiv/AIDS huonekana kwenye full blood PICTURE?

coyyote

Member
Joined
Aug 12, 2018
Posts
53
Reaction score
88
Wadau, habari za humu, baada ya miaka mingi ya kwenda hospitali pindi ninapo umwa tu sasa nataka niende kufanya check up ungali mzima wa afya. Sasa nataka nikafanye full blood picture, sasa katika kujiandaa kisaikolojia swali langu ni je wale wadudu hatari wa HIV pia huonekana?
 
Sasa nataka nikafanye full blood picture,
- Je ni hospitali ipi unapendekeza?
- Je makadirio ya gharama yakoje?

- My Take-
Ni uamuzi mzuri sana kuangalia afya, angalau mara moja kwa mwaka.
 
Hapana Hiv/aids haiwezi kuonekana kwenye full blood picture direct ila unapofanya fbp huwa kuna parameter ambazo zinaweza kuwa mwanzo mzuri wa kufikiria Hiv japo pia sio direct maana hizo parameter zime generalize tu mfano ni kama lymphocytes zimepanda sana moja kwa moja una suspect ni viral infection au immune disorders lakini pia leukemia
Jibu fbp pekee haiwezi kuonesha moja kwa moja kama una HIV
 
Asante mkuu
 
Full blood picture ndo vipimo ghani mkuu??
Nipen maarifa kidogo
 
Full blood picture(fbp) ni kipimo cha damu ambacho huonesha parameter mbalimbali ambazo zipo kwenye damu ni kipimo ambacho huweza kusaidia kuangalia kama kuna mabadiliko yaliyopo mwilini hasa kama unaanza kusikia mwili una shida ya ugonjwa na huonesha cells zote zilizomo kwenye damu na idadi inayotakiwa(normal ranges) hapa ukikuta zimezid basi kuna shida pia zikipungua kuna shida mfano hapo chini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…