HIV postive and negative @ the same time?

mkuu mpeleke hospitali ya wilaya yako na muulizie mteknolojia wa maabara wa wilaya au mratibu wa ukimwi wa wilaya.watampima na kuamua hatua zinazotakiwa kufuatwa.
Kuna muongozo maalum wa suala hili.
Nina wasiwasi na uelewa wa hao wahudumu wa AMREF!

Lakin@Meningitis nadhani wako sahihi kuna kipimo kimoja kama nilivyoweka kwenye picha kile cha blue ndio kilionyesha postive kile kama cheupe kikaonyesha negative wakarudia tena kujiridhisha na ikabidi wachukue kipimo kingine kumpima kama ana maambukizi ya magonjwa ya zinaa kukuta hana ndo wakaonelea nimrudishe after 3 month.ok nitajaribu kumpeleka hosp kama mlivyonipa ushauri thank u
 
Word!

Kwa hilo suala la kushinda na mtoto mmmhhhhh!...pana kazi kidogo...inabidi uwe mpole sana kwake, usije ukamkata hela za mshahara kisa kavunja glass zako, atalipiza kisasi kwa njia isiyofaa!


thanks my shemeji niliongea na dr hivyo akamshauri mapema namna ya kuishi kwa kipindi hii mie pia siku zote namchukulia kama ndugu ingawa hawa wenzetu huwa ahawatabiriki
 
NEVER ON EARTH!Na kama ipo twende tukaweke records kwenye WORLD GUINNESS BOOK OF RECORDS...Nitalipia Meal and Accomodation nad Transport!

kwa macho yangu nimeshuhudia nachokuomba jaribu kuongea na wataalam wakupe habari zaidi .thanks
 
Watanzania, the theory behind hii kitu (-ve or +ve) ni matokeo ya nchi zilizoendelea kutaka kutumaliza nchi maskini haswa africa. Kwa nini nasema hivyo?
  1. Soko la ARVs ni kubwa sana africa (Gharama zinakuwa subsidized na organs za umoja wa mataifa
  2. Fake results zinazopelekea mtu kutambulika ni mwasirika humfanya huyo mtu kutumia dawa za ARVs
  3. Atumiapo ARVs mtu asiyekuwa muathirika dawa hii huua kinga ya mwili
  4. Mwisho huyu muathirika fake hufa mapema (life expentancy inakuwa imepungua in totality ktk taifa)
  5. Na kifo chake huwa ni kama cha muathirika (kwani kutokana na ARVs anakuwa na UKIMWI=Upungufu wa Kinga Mwilini unaosababishwa na ARVs)
Kwa hiyo ushauri ni kuacha ngono zembe (ingawa wao wao wanaotuletea dawa wanafanya sana ngono zembe na wao waathirika ni wachache). Ni bora kuchukua individual preventive measures, otherwise ukitegemea vipimo matokeo yake hayatabiriki.
 
Pole FirstLady... Huu ulio nao ni mtihani. Ushauri wangu utaelemea zaidi kwa hapo nyumbani ambapo pakutia wasi... Mie naona hadi kukuambia kwake huyo binti hali yake halisi inaonesha ni walau ni kwa kiasi gani mwaishi nae vizuri, kuwa yupo huru to the extent anaweza kukuambia kitu chake nyeti kama hicho. Kama tunavyoelewa mara nyingi waathirika wa HIV/AIDS ni wasiri na hawapendi watu wajue else kama wanamuamini saana huyo mtu.

Kwa upande wa matunzo ya mtoto; from my understanding ni kuwa mtoto ni mdogo but sio mdogo sana kwa level ya uchanga... Ni hatari mtoto kuhudumiwa na muathirika kama huyo mtoto ni mdogo kuliko kama huyo mtoto mkubwa kidogo - hivo kwa kiasi fulani wasi wasi wako unaweza pungua kidogo.

Kikubwa nadhani ni bora kutumia vipimo vikubwa na katika hospitali ambayo wana kitengo cha kueleweka cha HIV/AIDS related.
 

thanx kwa ushauri my dear ,ni kweli nimemuweka karibu ndo maana anakuwa na confidence ya kunieleza hayo.mtoto ana 6 years sema huwa anamwandaa kwenda shule huduma za hapa home nikiwa kazini..nitampeleka hosp ya wilaya soon as possible ili nipate amani na kujua nini kifanyike
 
Kama wamekwambia umrudishe baada ya miezi mi 3. Kwa usalama wa familia mtoto na mume mkware.huyo anastahili kalikizo kwenda kwao for 3 months, then akirudi ukampime tena.DONT RISK YOUR FAMILLY.
 
Naona watu wanaconfuse vipimo vinavyotumika ktk research institutes na vipimo vinavyotumika kila siku ktk hizi hospitali zetu.Mimi naona utahangaika sana tu kuzunguka,maana hata huko utakapokwenda sidhani kama utawapangia watumie vipimo gani;wanaweza kutumia hivyo hivyo na matokeo yakatoka hayo hayo.Kwa nini usisubiri tu hiyo miezi mitatu?

Na kuhusu usalama wa mwanao siko sure 100% kama kuna risk kiasi hicho,maana hata kama atakuwa ameathirika huyu house girl hakuna mwenye uhakika wa lini hasa, maana kwa kipindi chote hicho amekuwa akimuhudumia bila tatizo.Anyway,to be in the safe side unaweza ukatafuta njia nyngine kama labda kumrudisha kijiji hadi hiyo 3 moths ipite.

On the other hand,sina hakika wewe una mtazamo gani juu ya social discrimination ya watu waishio na VVU!Maana unapokuwa unafikiria kumtenga huyu binti,usisahau kuwa wewe(kwa mtazamo wangu) ndiye mtu ambaye huyu binti amesurrender maisha yake kwako;just imagine mpaka ameona wewe ndiye mtu pekee wa kushare naye hisia alizonazo,halafu u-weigh out na impact ya kumtimua kwa kisingizio cha kusubiri miezi mitatu!

Vipi kama angekaa kimya halafu akaamua kufanya hicho tunachokutaka uamini kwamba anaweza kukifanya kwa mwanao?Naamini wewe ni mtu mzima,una maamuzi yako;na bahati nzuri umekuja humu,sio kutuomba ushauri wa nini cha kumfanya huyu binti,bali kutaka uhakika wa uwezekano wa majibu kutoka namna hiyo!

Tafakari...
 

thanks kwa ushauri ndugu mie pia sikuwa na wazo la kumrudisha kwao hasa nikifikilia hali halisi ya maisha ya kwao pia ameitunza family kwa upendo na uaminifu...amekuwa muwazi na mkweli kwangu nikiwaza ndio nachoka.....ila kwa sababu ni binti anaswali sana nilimkalisha na kumwambia namna ya kuishi sasa wakati tunasubiri majibu....na dr pia alimwambia awe makini sana kwa kipindi hiki ...ni muelewa sana ingawa sijui kama anaweza kubadirika ....Hapo Amref aliyempima ni Dr mstaafu wa wilaya ndo aliweza kumpa maangalizo ya maisha wakati akisubiri majibu..nikimwondoa sasa itakuwa namyanyapaa
 
Mwandalie special diet ya kutosha
 
Pole sana mamy, si wewe tu bali kesi hizi huwakuta wengi, mi nakushauri usisubiri hiyo miezi mitatu, nenda kampime tena ili upate uhakika zaidi, jitahid kutafuta muda, tena uende hosp ya mkoa au wilaya usiende huko kwenye hivyo vituo tena,umenikumbusha wapendwa fulani hivi walikua wanataka kufunga ndoa walivyoenda angaza majibu yakaja kama hivyo, yaani ilikua balaa,.so we jipange mpeleke tena kwa uhakika zaidi.
 
Pole First lady.. Mungu akusaidie kupata majibu sahihi na mwongozo wa kipi cha kufanya.



Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Vipimo vingi vya HIV TANZANIA viliingizwa na mama mpiga dili blandina nyoni, vingi ni hovyo jamii ya watanzania wanateketea kwa kupewa majibu ya ama wanaugua au hawagui HIV/AIDS nina ushahidi wa madaktari na wakaguzi wa performance audit kutoka WHO na UNACTAIDS ukionyesha mapungufu ya vipimo na vitendashi ( yale maji ) vya kupimia HIV.
Ni kuomba mungu tu ndugu zangu.
 
Kama uko Dar, nenda Lugalo kwa wajesi huyo binti akapimwe tena wala usisubiri miezi mitatu!! Jipe moyo!
 
Pole sana na majaribu.Ila ukae ukajua wote tunapita kwenye hii dunia.Naomba usimtenge wala kumwonyesha dalili yoyote ya mabadiliko hata kama akikutwa nao
 

Nakumbuka miaka mitano iliyopita, nilikwenda kupima, wapimaji wakaniuliza natokea wapi kwa sababu accent yangu sio ya mzawa, nikawauliza ni kwa nini wananiuliza natokea wapi? Wakaniambia Africa kuna HIV1 na HIV2, na vipimo vya HIV1 haviwezi kuona HIV2, kwa hiyo wanataka kujua kama nimetoka africa ili watumie vipimo vyote viwili. Sasa hivyo vipimo viwili walivyotumia vinaweza kuwa ni vya kuangalia aina tofauti pia.
Fuatilia ujue kiundani zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…