Mtazamo wangu
1. Sijaona ubaya bongo movie kuungana katika msiba wa marehemu Masogange hata kama hajaigiza movie yoyote,huko tunaita kujumuika kijamii(socialize) kama hujui maana uliza usaidiwe.Ndio maana hata katika misiba yetu sis tulioko kitaani ukifiwa majirani huja msibani je wale ni ndugu zako wa damu? je wanajipendekeza au wanakuja kukufariji?
2. Tuache kujidai wajuaji katika mambo ambayo yametuzidi kimo.Tuwe na akiba ya maneno,kuongea sana sio kuzuri.
3. Kwa desturi ya mwanadamu pindi binadamu mwenzetu anapofariki tulio hai tuna mafunzo ya kujifunza na kukumbuka kwamba duniani tupo kwa msimu tu kwa hiyo pumzi uliyonayo isikufanye ujifarague kwamba wewe ni bora kuliko aliyekufa wakati ni wewe ni marehemu mtarajiwa,isitoshe kati yetu hakuna ajuaye kifo chake kitakujaje.
Asante