Elections 2010 Hivi CHADEMA haina wataalamu, au viongozi wake ndiyo wasioambilika?

Mkuu MF
Kama umeshindwa kuisoma yote, nini sababu ya msingi ya kukoti jamvi lote hilo? Si ungeandika tu kwamba umeshindwa kusoma? Kajamvi haka kanakutia uvivu wa kusoma? Vipi umeshamaliza kusoma sera na ilani ya Chadema?
Alafu mbali na kumaliza kusoma ilani nimeirudia mara nyingi tu. Hii imeandikwa kama ya sisi m vile, nimeshindwa kuisoma vizuri ingawa naendelea kuisoma kwa shida. Sijui aliiandika Makamba?
 
Mwenye uvumilivu wa kuusoma mpaka mwisho huo upupu na kukubaliana nao, ampigie kura Kikwete. Sisi tulio na kiu ya maendeleo tutampigia kura Dr. Slaa.
Ule umakini wenu umeishia wapi? Kweli mnaweza ama mnaota tu?
 
Alafu mbali na kumaliza kusoma ilani nimeirudia mara nyingi tu. Hii imeandikwa kama ya sisi m vile, nimeshindwa kuisoma vizuri ingawa naendelea kuisoma kwa shida. Sijui aliiandika Makamba?
Inaonekana Makamba anawakosesha wengi usingizi...!
 
Daboman punguza hasira, Unakuwa na hasira hadi unasahau kuweka paragraph duh pole
 
This discussion reminds me of a guy who said "Iliposemwa Yesu akirudi kila jicho litamuona some hundreds years ago ilionekana ni impossible, but wait - What if it will be thru TV??'' Can someone imagine how a TV of 2095 will b?
 
sorry, your thread is very short i think u didnt have enough time to prepare the long one. tehe tehe tehe tehe,,,,,,
 
This discussion reminds me of a guy who said "Iliposemwa Yesu akirudi kila jicho litamuona some hundreds years ago ilionekana ni impossible, but wait - What if it will be thru TV??'' Can someone imagine how a TV of 2095 will b?

Nyambala, kwa hiyo matumaini ya Dr Slaa kushika usukani ni sawa na yale ya Yesu kurudi? Kama ndio hivyo basi nitakufa kabla yake, mana mamia ya miaka imepita tangu tuambiwe kwamba Yesu atarudi!!!
 
May be slaa he can....! na treni yake ya angani
Mkuu Kibunango, kwa sasa unajishushia hadhi kwani unajibu kihuni. Najua unaumia rohoni na Dr. Slaa anakunyima usingizi lakini hebu punguza munkari kidogo. Kama hukuwa moja wapo wa waliolitafuna taifa hili bila huruma, huna cha kuogopa - bado wiki tatu tu, historia iandikkwe upya.
 
Nyambala, kwa hiyo matumaini ya Dr Slaa kushika usukani ni sawa na yale ya Yesu kurudi? Kama ndio hivyo basi nitakufa kabla yake, mana mamia ya miaka imepita tangu tuambiwe kwamba Yesu atarudi!!!

Shape both ur head and ur ass up!
 
Mzee wa IT kajipange tena japo mada yako ni changamoto
 

huyo toka kitambo hana hadhi. Kule kwa wakubwa kumemtibua akili. Alikuwa kapten kule
 

Maneno mengi sana. Ungeandika paras nne tu badala ya kutuwekea background ya ICTs. Mimi nilifikiri ambayo yangefuata yangeendana na ICTs kumbe hamna!!!

Jaribu kulinganisha ahadi za wagombea wote wa Urais.

Wewe ni sababu mojawapo ya Tanzania kuwa maskini!!!!!!!
 


Nafikiri tatizo ni katika vision. Tatizo kubwa la CCM hawajawahi kuwa na Vision ya Tanzania kama nchi kujiendeleza Kisayansi (Shule za kata) na hawana mpango wa kushindana na taifa lolote duniani (hata shirika la ndege hatuna). Hivyo basi, sisi katika CHADEMA tunaamini katika ushindani wa kisayansi na uwezo wa kuwa na treni yenye kasi hiyo ya 410 km/hr.

Nani kakwambia lengo la treni ya Slaa (PhD) ni kuwa kumbakumba na hivyo kulazimika kupitia Dodoma na nani kakwambia hatuwezi kuwa na reli ambayo ni almost straight line (Approx. 900 km). Hata ahadi ya masaa mawili na nusu ni feasible. Mwandishi anakili technolojia ya speed 410 km/hr siyo ndoto (Ipo China)...Sasa hapo kuna geni chini ya Jua?
 
Mkuu,

Watu kama huyu dabomani wanaotumia muda mwingi madrassa hawawezi kukuelewa

Na wewe umetumia muda mwingi Sunday School, kule mlipokuwa mnaliwa mgongo na mapadri! :tonguez:
 

Huyo huenda akawa ni sababu mojawapo ya Tanzania kuwa masikini lakini WEWE ni sababu kubwa ya Tanzania kuendelea kuwa masikini! :tonguez:
 
Nikisema nawe ni mhuni nitakuwa nimekosea? Soma mara mbili bandiko lako na utajua kwa nini nimediriki kukuita mhuni.
Kwa mujibu wa KAMUSI ya kiswahili sanifu neno mhuni maana yake ni mseja yaani mtu asiye na mke au mume, pili mtu asiye na makazi maalum, tatu mtu asiye na tabia nzuri na nne mtuasiye chungia wengine heshima
Neno kiherehere maana yake ni mpapatiko wa moyo au wahaka au wasiwasi au machugachuga
Machugachuga ni hali ya kutotulia mahali pamoja au wasiwasi au wahaka
wahaka ni hali ya wasiwasi na kupapatika kwa moyo, kiherehere,wasiwasi
Neno ***** maana yake ni mtu mjinga, mpumbavu, bozi au ****
Neno mahaba maana yake ni mapenzi
Neno MAGAZIJUTO (MA=mabano GA=gawanya ZI=zidisha JU=jumlisha TO=toa) hesabu za darasa la tatu enzi za elimu ya mwalimu

Nimetumia kiswahili sanifu katika kukutaka wewe mwana CCM na wana CHADEMA kutoa mchanganganuo wa kimahesabu wa ahadi za wagombea wenu DKT JK na DKT SLAA naomba nipe mchanganuo huo na si kukwepa hoja na kuniita mhuni, eti mimi ni CHADEMA.
MIMI nina mke hivyo mimi si mhuni, MIMI ninamakazi yangu ya kudumu hivyo sitegemei DKT SLAA ashushe bei ya cement na bati ndio nijenge hivyo mi si mhuni kwa tafsiri ya kiswahili sanifu, pia sijakuvunzia heshima wewe au wana CCM na wana CHADEMA au wagombea wenu hivyo tafsiri ya neno mhuni hainihusu, kwa hiyo mimi si mhuni.

Napenda kukuambia kuwa mwanachama wa chama chochote cha kisias ambacho kimesajiliwa kisheria si kosa la jinai, hivyo siwezi kuona aibu kuwa mwanachama wa chama chochote kama mimi ni mwanachama. Hivyo kuwa CUF,CCM,CHADEMA,NRA.NLD,UPDP,APPT nk sio kosa na mtu inapaswa ajivunie chama chake. Narudia tena kujitangaza humu JF kuwa mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa. mimi ni mwanaharakati wa mazingira na uchumi (mjasiriamali) hila ndoto zangu naona zina zimwa na CCM ndio maana naonekana mpinzani wao. Kiukweli nawa support wagombea wanaopigania nchi hii kuitoa katika kongwa la utumwa wa kiakili, na katika makucha ya mafisadi bila kujali chama wanachotoka.

Turudi kwenye MADA naomba ufafanuzi wa kimahesabu ukizingatia kanuni za MAGAZIJUTO kutoa mchanganuo wa uhalisia wa AHADI za mgombea wako wa chama cha jembe na nyundo, je AHADI hizo zinatekelezeka ndani ya miaka mitano? nakukumbusha zingatia utendaji wake ndani ya miaka mitano iliyopita bila kusahau ufisadi uliotamalaki nchini
 


Wala si ulimbukeni, ni kukosa kwako kuelewa zaidi ya mambo yaliyozoeleka. Kwani kufikiri nje ya mazoea (boksi) kunahitaji ubunifu na uthubutu. Vinginevyo kwako hakuna kinachowezekana. Maelezo ya msingi ni kuwa masuala ya reli zilizopo, barabara, shule, maji, nakadhalika hayastahili kuwa kwenye ajenda ya mgombea uraisi kwani ni ya kawaida. Haina maana kuzungumzia vitu ambavyo raisi yeyote atakayechaguliwa atavitendea kazi. Mgombea anatakiwa kuzungumza vile ambavyo vitamuwezesha kujipambanua na wagombea wengine. Anatakiwa atoe maono ambayo yatatufanya tujue kuwa asipochaguliwa tutakosa 1,2,3 … Si kuwa na rais ambaye akiwepo au asipokuwepo yote sawa tu. Wala haina maana kuwa ukianzisha mradi mpya wa reli basi ya zamani lazima ife. Reli inayozungumziwa, hakika ni mpya na ya moja kwa moja kutoka Dar hadi Mwanza. Huwezi ukawa na vituo lukuki njiani kwa treni ya kasi inayozungumzwa.
Wala si lazima reli hiyo ipitie mikoa uliyoitaja, kwani mikoa hiyo nayo inaweza kuwa na miradi kama hiyo. Mradi huo hauzuii kuigwa sehemu nyingine. Unapokuwa na jambo jipya lazima uwe na pa kuanzia. Kwa maelezo yako unakiri kwa limbukeni kuwa kitekinolojia inawezekana na imeshafanyika kwingine duniani kwa mafanikio. Ila kwa mawazo yako pia unaamini kuwa kwa vile hapa ni Tanzania hiyo haiwezekani. Hiyo ndiyo tofauti kubwa iliyopo kati ya wanaoamini kuwa wanaweza na wa aina yako ambao mnaamini kuwa haiwezekani kufanya chochote. Utawala huu kama ungekuwa ndio unaongoza enzi za kujenga reli ya TAZARA basi akina Kibunango wangeshauri iachwe kwani haiwezekani na inapita porini bila kujua kwamba porini kwa leo (2010) ndiko mjini ifikapo 2030.
[Ukipima umbali huo moja kwa moja toka kwenye ramani, utapata kilometa 850.20 hivi. Na sijawahi kuona reli iliyoonyoka toka pointi A hadi B kama ambavyo wewe unavyotaka kutuambia hapa!]
Umbali kutoka Mwanza hadi Dar usikupe shida. Kwa treni za moja kwa moja (ambazo ziko duniani) kama alivyoainisha mtoa kiroja ni kati ya 250 hadi 400 km kwa saa. Kwa hiyo hakuna ubishi kuwa hizo km 1,000 (kwa njia mpya ya mkato na kona za lazima) zinawezekana kabisa kwa saa tatu. Tukubaliane mpaka hapo. Kama nilivyoeleza hapo awali huu ni mpango wa miaka 15. Katika kipindi hicho teknolojia inayoongezeka kila uchao itakuwa na majibu mazuri zaidi.
[Reli ya kati imepita katika mikoa zaidi ya minne(Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, na Mwanza), sasa wewe na slaa wako mnataka kutuambia kuwa mtajenga reli mpya bila kupita katika mikoa hiyo? Mtaipitisha angani nini? Je wananchi wa mikoa iliyobaki wasahau huduma hiyo muhimu kwao kwa usafiri?]

Treni ya sasa itaendelea na shughuli zake kwani huo ni mpango ambao tayari unafanya kazi. Cha muhimu kufahamu ni kuwa tunahitaji kusogea mbele ya hapo. Huwezi kusogea bila kuwa na mipango. Kwa maneno mengine wakati akina Kibunango mnaamini kuwa miaka kumi na tano ijayo Watanzania
waendelee kuwa na treni na reli ya mwaka 47 (kilomita 65 kwa saa) wenzenu wanathubutu kubuni mpango mpya. Huu ni uthibitisho kuwa hakuna ubunifu wala uthubutu upane wa Kibunango. Kila kisichokuwepo, hakiwezekani kana kwamba sisi si binadamu kama binadamu wengine duniani.

Kibunango, ukitaka kuwaua wanao hali wakiwa hai waimbie tu huo wimbo wako mtamu kuwa hawawezi. Kama hamu yako ni kuidhoofisha jamii iaminishe kuwa haiwezi kuthubutu kufanya lolote. Ukitaka kulifuta taifa katika ramani ya dunia huna haja ya kutumia nyuklia, wewe lilishe tu sumu kuwa taifa hilo haliwezi, utakuwa umefanikiwa “kupita maelezo”.
Tuliambiwa na akina Kibunango hatuwezi kuongoza TANESCO wakaletwa Net Group Solution, nini kilichotokea? Haikutosha tukaelezwa hatuwezi kuendesha hata kampuni ya maji ya Dar es Salaam, wakaletwa. Benki eti tumezishindwa, wakaletwa. Hawakuishia hapo, hata reli waliyojenga wakoloni na ambayo imeendeshwa kwa miaka mingi kwa ufanisi mzuri tu, ghafla tukawa hatuwezi, imekodishwa kwa kampuni ya Kihindi. Kweli hatuna tunachoweza? Hatujui hata kulima na hivyo ili kuokoa kilimo kwanza, wako mbioni kuleta walowezi. Mambo haya yakiachwa kuendelea bila kukemewa na kusitishwa, Watanzania tunaweza kujikuta kuwa kivutio tu cha watalii, kama walivyo wahindi wekundu Amerika na Australia.
Kwa maana: Dawa ya Mjinga ni kuumia
 
Tatizo ni chadema na ahadi za kihuni! Hata wafuasi wake wengi ni wahuni na mfano mojawapo ni wewe mwenyewe! Hebu angalia lugha uliyotumia katika posti yako hapo!

Zaidi nimeona uchambuzi wako yakinifu!

UUNGWANA ni vitendo inawezekana nimekukwaza wewe na wana JF wengine kwa maneno(uliyopigia mstari) niliyotumia katika POSTs zangu naomba RADHI kwako na kama kuna yeyote ambaye maneno niliyotumia yamemkwaza. Lakini FAMI na KUGA ni majina ya wagombea wetu wa urais hapa TZ. Nitatoa tafsiri ya maneno haya ktk post nyingine ili mhakiki kama nimeyatumia kimakosa au la.

Lakini kibunango naomba mchanganuo wa kimahesabu kuhusu kutekelezeka au kutotekelezeka kwa AHADI za mgombea wenu
 
Hili li-article halina urafiki na wasomaji. Weka walau aya basi tuweze kusoma hii post yako. Dah!

Malengo ya article siyo kutengeneza urafiki na wasomaji. Malengo yake ni kutoa changamoto kwa wachangiaji waongeze matumizi ya akili zao badala 'KU-COMFORM' tu, hata pale Walalahoi wa nchi yetu wanapodanganywa mchana kweupee!
Wabunifu wa forum hii wameiita kuwa ni 'HOME OF GREAT THINKERS', tafadhali msiwaangushe!
Una haki ya kwenda kumpigia kura Dr. Slaa siku ya tarehe 31/10/2010, lakini haki ya kuzuia tusichambue ahadi zake huna!
Tunaochambua ahadi za Dr. Slaa hatuna makosa kwa sababu timu yake ya PR na marketing inafanya kazi kubwa kuwashawishi Watanzania kuwa Slaa ni 'Mkombozi' wetu. Unataka tukubali tu? Hiyo siyo sifa ya kisomi hata kidogo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…