Elections 2010 Hivi CHADEMA haina wataalamu, au viongozi wake ndiyo wasioambilika?

Elections 2010 Hivi CHADEMA haina wataalamu, au viongozi wake ndiyo wasioambilika?

[SIZE=3]Malengo ya article siyo kutengeneza urafiki na wasomaji. Malengo yake ni kutoa changamoto kwa wachangiaji waongeze matumizi ya akili zao badala 'KU-COMFORM' tu, hata pale Walalahoi wa nchi yetu wanapodanganywa mchana kweupee! [/SIZE]
Wabunifu wa forum hii wameiita kuwa ni 'HOME OF GREAT THINKERS', tafadhali msiwaangushe!
Una haki ya kwenda kumpigia kura Dr. Slaa siku ya tarehe 31/10/2010, lakini haki ya kuzuia tusichambue ahadi zake huna!
Tunaochambua ahadi za Dr. Slaa hatuna makosa kwa sababu timu yake ya PR na marketing inafanya kazi kubwa kuwashawishi Watanzania kuwa Slaa ni 'Mkombozi' wetu. Unataka tukubali tu? Hiyo siyo sifa ya kisomi hata kidogo!

Kwa hiyo na wewe ni msomi???????????
 
Toa sababu kwanini iwezekane Ulaya ishindwe Tanzania huo ndiyo uchovu wa mawazo unaoedeshwa na CCM. Treni kutoka mwanza mpaka dar kwa masaa matatu inawezekana, kuna miujiza gani hapa?
 
Wala si ulimbukeni, ni kukosa kwako kuelewa zaidi ya mambo yaliyozoeleka. Kwani kufikiri nje ya mazoea (boksi) kunahitaji ubunifu na uthubutu. Vinginevyo kwako hakuna kinachowezekana. Maelezo ya msingi ni kuwa masuala ya reli zilizopo, barabara, shule, maji, nakadhalika hayastahili kuwa kwenye ajenda ya mgombea uraisi kwani ni ya kawaida. Haina maana kuzungumzia vitu ambavyo raisi yeyote atakayechaguliwa atavitendea kazi. Mgombea anatakiwa kuzungumza vile ambavyo vitamuwezesha kujipambanua na wagombea wengine. Anatakiwa atoe maono ambayo yatatufanya tujue kuwa asipochaguliwa tutakosa 1,2,3 … Si kuwa na rais ambaye akiwepo au asipokuwepo yote sawa tu. Wala haina maana kuwa ukianzisha mradi mpya wa reli basi ya zamani lazima ife. Reli inayozungumziwa, hakika ni mpya na ya moja kwa moja kutoka Dar hadi Mwanza. Huwezi ukawa na vituo lukuki njiani kwa treni ya kasi inayozungumzwa.
Wala si lazima reli hiyo ipitie mikoa uliyoitaja, kwani mikoa hiyo nayo inaweza kuwa na miradi kama hiyo. Mradi huo hauzuii kuigwa sehemu nyingine. Unapokuwa na jambo jipya lazima uwe na pa kuanzia. Kwa maelezo yako unakiri kwa limbukeni kuwa kitekinolojia inawezekana na imeshafanyika kwingine duniani kwa mafanikio. Ila kwa mawazo yako pia unaamini kuwa kwa vile hapa ni Tanzania hiyo haiwezekani. Hiyo ndiyo tofauti kubwa iliyopo kati ya wanaoamini kuwa wanaweza na wa aina yako ambao mnaamini kuwa haiwezekani kufanya chochote. Utawala huu kama ungekuwa ndio unaongoza enzi za kujenga reli ya TAZARA basi akina Kibunango wangeshauri iachwe kwani haiwezekani na inapita porini bila kujua kwamba porini kwa leo (2010) ndiko mjini ifikapo 2030.
[Ukipima umbali huo moja kwa moja toka kwenye ramani, utapata kilometa 850.20 hivi. Na sijawahi kuona reli iliyoonyoka toka pointi A hadi B kama ambavyo wewe unavyotaka kutuambia hapa!]
Umbali kutoka Mwanza hadi Dar usikupe shida. Kwa treni za moja kwa moja (ambazo ziko duniani) kama alivyoainisha mtoa kiroja ni kati ya 250 hadi 400 km kwa saa. Kwa hiyo hakuna ubishi kuwa hizo km 1,000 (kwa njia mpya ya mkato na kona za lazima) zinawezekana kabisa kwa saa tatu. Tukubaliane mpaka hapo. Kama nilivyoeleza hapo awali huu ni mpango wa miaka 15. Katika kipindi hicho teknolojia inayoongezeka kila uchao itakuwa na majibu mazuri zaidi.
[Reli ya kati imepita katika mikoa zaidi ya minne(Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, na Mwanza), sasa wewe na slaa wako mnataka kutuambia kuwa mtajenga reli mpya bila kupita katika mikoa hiyo? Mtaipitisha angani nini? Je wananchi wa mikoa iliyobaki wasahau huduma hiyo muhimu kwao kwa usafiri?]

Treni ya sasa itaendelea na shughuli zake kwani huo ni mpango ambao tayari unafanya kazi. Cha muhimu kufahamu ni kuwa tunahitaji kusogea mbele ya hapo. Huwezi kusogea bila kuwa na mipango. Kwa maneno mengine wakati akina Kibunango mnaamini kuwa miaka kumi na tano ijayo Watanzania waendelee kuwa na treni na reli ya mwaka 47 (kilomita 65 kwa saa) wenzenu wanathubutu kubuni mpango mpya. Huu ni uthibitisho kuwa hakuna ubunifu wala uthubutu upane wa Kibunango. Kila kisichokuwepo, hakiwezekani kana kwamba sisi si binadamu kama binadamu wengine duniani.

Kibunango, ukitaka kuwaua wanao hali wakiwa hai waimbie tu huo wimbo wako mtamu kuwa hawawezi. Kama hamu yako ni kuidhoofisha jamii iaminishe kuwa haiwezi kuthubutu kufanya lolote. Ukitaka kulifuta taifa katika ramani ya dunia huna haja ya kutumia nyuklia, wewe lilishe tu sumu kuwa taifa hilo haliwezi, utakuwa umefanikiwa “kupita maelezo”.
Tuliambiwa na akina Kibunango hatuwezi kuongoza TANESCO wakaletwa Net Group Solution, nini kilichotokea? Haikutosha tukaelezwa hatuwezi kuendesha hata kampuni ya maji ya Dar es Salaam, wakaletwa. Benki eti tumezishindwa, wakaletwa. Hawakuishia hapo, hata reli waliyojenga wakoloni na ambayo imeendeshwa kwa miaka mingi kwa ufanisi mzuri tu, ghafla tukawa hatuwezi, imekodishwa kwa kampuni ya Kihindi. Kweli hatuna tunachoweza? Hatujui hata kulima na hivyo ili kuokoa kilimo kwanza, wako mbioni kuleta walowezi. Mambo haya yakiachwa kuendelea bila kukemewa na kusitishwa, Watanzania tunaweza kujikuta kuwa kivutio tu cha watalii, kama walivyo wahindi wekundu Amerika na Australia.
Kwa maana: Dawa ya Mjinga ni kuumia

KWELI UKIPENDA, CHONGO UTAITA KENGEZA!

Of course kuwa na treni ya saa tatu DAR -MWANZA inawezekana kama conditions ziko right, hoja ni kwamba hivi sasa conditions haziko right kabisaa! (Tafadhali rejea kuipitia mada)

HUENDA SIKU:
  • Kila Mtanzania atakapokuwa na uwezo wa kula milo mitatu kwa siku;
  • Kila mwanafunzi wa nchi hii akawa anakaa kwenye dawati;
  • Kila MTZ akawa na maji safi na salama;
  • Kila kaya ikaacha matumizi ya kuni na mkaa;
  • Kila shule na chuo kikawa na maktaba yenye vitabu 'latest';
  • Idadi ya wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi kwa vitendo (yaani katika maabara zenye vifaa vyote muhimu) ikaongezeka walau mara 50 kuliko ilivyo sasa;
  • Na nyie 'wasomi' wetu mlioajiriwa kwenye halmashauri zetu, idara za serikali, taasisi nyingine za ummah na makampuni binafsi mtakapoacha vitendo vya wizi na rushwa, a.k.a, UFISADI ULIOFUMBIWA MACHO;
  • Na pale 'WAKOMBOZI WETU', kama kina Dr. Slaa, watakapoacha kudai kwanza vyama vyao viwalipe MAMILIONI ndipo wafanye kazi ya kutukomboa.
TUKAANZA KUWA NA MATUMAINI KUWA HUENDA TRENI YA MASAA MATATU DAR- MWANZA INAWEZEKANA.
Believe it, hili halitatokea kwa generation hii ya viongozi!
 
Huna hoja zaidi ya hiyo? Nakuonea huruma!
Kama thinking power unayo-display inawakilisha 'wasomi wetu' walio wengi, basi haishangazi kuwa nchi hii inazidi kuzama siku hadi siku! Kama 'wasomi' wetu ambao hamuwakilishi hata 10% ya population ndiyo mentality mliyonayo, vipi hawa 90% ambao 'siyo wasomi'? SAD!
 
Huna hoja zaidi ya hiyo? Nakuonea huruma!
Kama thinking power unayo-display inawakilisha 'wasomi wetu' walio wengi, basi haishangazi kuwa nchi hii inazidi kuzama siku hadi siku! Kama 'wasomi' wetu ambao hamuwakilishi hata 10% ya population ndiyo mentality mliyonayo, vipi hawa 90% ambao 'siyo wasomi'? SAD!

madrassa al sul
 
Nadhani huo ni mtazamo wako kwa upeo wako japo unayoyanukuu hayana reference: Lakini kumbuka ukionyesha kidole kimoja kwa mwenzio kuna vidole vinne vinakunyooshea mwenyewe: Hebu tuambie:

1. Inflation ya Tanzania kufikia 16% mwaka huu 2010 kutoka 6% mwaka 2005, je CCM haina wataalamu?

2. CCM kuahidi kwenye ilani (kwa maandishi) na kushindwa kuweka Mahakama ya Kadhi, je CCM haikuwa na wataalam wa sheria?

3. Kushindwa kununua mazao kutoka kwa wakulima baada ya kuahidi kuwa watanunua mazao yote. Je CCM haikuwa na wataalam au hawana pesa?

4. Kuingia mikataba mibovu ya Richmond, Madini n.k. Je CCM haikuwa na wataalam au hawaambiliki?

5. Watu wachafu mfano Mramba, Chenge, Rostam, Lowassa n.k. kuendelea kugombea na kunadiwa na JK katika majukwaa - je CCM haina wataalamu wa kuwashauri?
 
Jamani Dr. Slaa ana PhD in theology. Please, don't overhype it like it is something very meaningful. It reminds me kuna wadau wakati tumemaliza F6 waliweka Div 1 kwa sababu ya misonge ya Divinity. Wanashangilia lakini Muhimbili hawakugusa.

Ndio anayo PhD ya dini, good for him, but don't run around like it matters. Because, we all know it doesn't even count. The only place his PhD is meaningful is in the pulpit, huku kwengine kote anatupotezea.
 
Jamani Dr. Slaa ana PhD in theology. Please, don't overhype it like it is something very meaningful.

Mkuu, ile ya Kikwete ni ya nini?
BTW, hivi Makamba Sr elimu yake ni ya kiwango gani?
 
Kibunango,

Kujibiwa hoja zoote za dabomani ndio umekuwa uhuni? Kubali tuu kuwa mabadiliko yaja. mnaweza kufanya kama Kenya wakakimbilia kumwapisha Rais nasikia hata wimbo wa Taifa lao wakasahau kuupiga. Naona tu kuanza kuleta Jeshi liseme ni matayarisho ya kuapishana haraka haraka.
 
Woo! Nilikuwa nime-take a brake kusoma hilo article ambayo ingependeza zaidi kwenye gazeti la UHURU, lakini majibu ya Rutashubanyuma yameniokolea muda wangu wa kumalizia the looooong article. and dont forget the 20+billions JK alizotumia ku-renovate Ikulu wakati Mkapa already spent some 9b before he left. WHAT A WASTE! ccm have no shame, no mercy to local raia. .............................
 
Back
Top Bottom