Hivi hawa Watanzania 'wanyonge' wana sifa zipi? Na wanapataje hizo sifa?

Hivi hawa Watanzania 'wanyonge' wana sifa zipi? Na wanapataje hizo sifa?

Mwanamayu

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2010
Posts
11,662
Reaction score
6,888
Inaonekana neno 'wanyonge' limeshika kasi katika matumizi yake hapa Tanzania, na kutumiwa sana na baadhi ya wakuu kabisa wa nchi. Kwa mujibu wa baadhi ya machapisho, 'wanyonge' maana yake ni 'masikini sana', au 'watu wadhaifu katika jamii'. Kwa Kiingereza ni 'disadvantaged', 'abject poor', au 'weaker people.'

Sasa tangu tupate uhuru CCM wapo madarakani, iweje mpaka leo baadhi ya viongozi wao wakuu waliopewa dhamana bado wanalalamika juu ya uwepo wa wanyonge mpaka kufikia kusema wao ni viongozi wa wanyonge?

Kwa nini wanyonge hawajaisha?

Nani anasababisha uwepo wa wanyonge?

Na kusema kuwa mimi kama kiongozi mkuu nitatetea haki za wanyonge, je nani atatetea haki za wasiokuwa wanyonge? Nani anayetoa haki kwa wananchi? Au wasiokuwa wanyonge upata haki ndani ya sekunde?
 
Kiukweli ni neno dhalilishi kwa wananchi,na inashangaza linavyotumiwa Kama silaha ya viongozi kujificha huku wakiwahadaa kwa vitambulisho vya machinga. Huwezi kutaqala watu wako na kwa miaka mingi na ukawaita watu wako majina ya hovyo ni dharau kubwa.
CCM wanadharau sana, JK hakuwahi kuita watu wanyonge, unyonge ni udhaifu tena mkubwa sana.
 
Leo wanyonge ni mtaji wa kisiasa.

Wanyonge are persons of no fixed abode.

Wakulima tunawafahamu.

Wafanyakazi tunawafahamu.

Mwalimu alisema nchi hii ni ya wakulima na wafanyakazi.

Lakini kundi hili la waanyonge wapo tu, hawana kufanya kazi wala kulima.

Wala hawalipi kodi.

Wapo wapo tu.

Hao wamo machinga, mama ntilie, matapeli, mishen town na wengine.

Wamekuwa mtaji mkubwa wa kisiasa na wanatumiwa kwa convenience ya wanasiasa.

Matatizo yao wala hayatatuliwi, maana yakitatuliwa mtaji unaondoka.

Watanzania tujihadhari na utapeli huu wa kuwaita watu eti wanyonge.
 
Inaonekana neno 'wanyonge' limeshika kasi katika matumizi yake hapa Tanzania, na kutumiwa sana na baadhi ya wakuu kabisa wa nchi. Kwa mujibu wa baadhi ya machapisho, 'wanyonge' maana yake ni 'masikini sana', au 'watu wadhaifu katika jamii'. Kwa Kiingereza ni 'disadvantaged', 'abject poor', au 'weaker people.'

Sasa tangu tupate uhuru CCM wapo madarakani, iweje mpaka leo baadhi ya viongozi wao wakuu waliopewa dhamana bado wanalalamika juu ya uwepo wa wanyonge mpaka kufikia kusema wao ni viongozi wa wanyonge?

Kwa nini wanyonge hawajaisha?

Nani anasababisha uwepo wa wanyonge?

Na kusema kuwa mimi kama kiongozi mkuu nitatetea haki za wanyonge, je nani atatetea haki za wasiokuwa wanyonge? Nani anayetoa haki kwa wananchi? Au wasiokuwa wanyonge upata haki ndani ya sekunde?
Nikweli kabisa Tanzania imeshakombelewa tangu 1961 sasa unyonge umetoka wapi? am just curious!
 
Nilishasema wanyonge wa Tz Ni Kama kina mzee Halima. Watu wasio na msimamo, watu wanaonunuliwa au kurubuniwa kirahisi kwa Bei ndogo. Mnakumbuka kipindi Cha wajumbe....wale nao Ni wanyonge
 
Unyonge siyo sifa wala hali ya kujivunia. Kiongozi yeyote mwenye nia njema na nchi hii lazima apige vita unyonge na kuutokomeza. Viongozi wanaojidai kuwa watetezi wa wanyonge bila ya kuweka bayana mikakati ya kuwainua kisayansi hiyo ni hadaa ya kisiasa. Tunataka viongozi wetu wapimwe kwa kuondoa umaskini na unyonge na siyo kujivunia kundi kubwa la wanyonge. Nchi nyingine zinajivuna kupunguza umaskini na unyonge, sisi tunajivuna kukuza na kupalilia unyonge.
 
Kwanza kabisa kitendo cha kiongozi kudai yeye atatumikia wanyonge tayari hafai. Kwa mfano mimi siwezi kukubali kuitwa mnyonge ina mana huyu kiongozi atanibagua. Ile dhana ya mwenye nacho kaiba ndio mahali pake na mnyonge ni dhaifu hana maamuzi kisiasa na kijamii pia.

Ndio maana wanasiasa wanajifichia huko sababu wanajua wanyonge bado wamelala kiakili na kifikra ni rahisi kuwatawala
 
Ukisha declare kwamba wewe ni mnyonge, basi ruksa kupanga nguo zako za mitumba kwenye barabara ya mwendokasi, raha iliyoje kwa wanyonge....tuliambiwa hii nchi ni tajiri sana, ghafla tukasikia 'najua mtanikumbuka kwa sababu nimesakirifaisi maisha yangu kwa ajili ya watanzania maskini' haya sakirifaisi imeshatolewa lakini wanyonge bado wapo na mwingine anajipanga kujisakirifaisi kwa ajili ya wanyonge.....yetu macho na masikio...
 
Inaonekana neno 'wanyonge' limeshika kasi katika matumizi yake hapa Tanzania, na kutumiwa sana na baadhi ya wakuu kabisa wa nchi. Kwa mujibu wa baadhi ya machapisho, 'wanyonge' maana yake ni 'masikini sana', au 'watu wadhaifu katika jamii'. Kwa Kiingereza ni 'disadvantaged', 'abject poor', au 'weaker people.'

Sasa tangu tupate uhuru CCM wapo madarakani, iweje mpaka leo baadhi ya viongozi wao wakuu waliopewa dhamana bado wanalalamika juu ya uwepo wa wanyonge mpaka kufikia kusema wao ni viongozi wa wanyonge?

Kwa nini wanyonge hawajaisha?

Nani anasababisha uwepo wa wanyonge?

Na kusema kuwa mimi kama kiongozi mkuu nitatetea haki za wanyonge, je nani atatetea haki za wasiokuwa wanyonge? Nani anayetoa haki kwa wananchi? Au wasiokuwa wanyonge upata haki ndani ya sekunde?
Wapo lumumba, sifa yao kubwa ni kuitete serikali hata kama inafanya kinyume na katiba ya nchi wao wataitetea mpaka kifo kitakapowatenganisha na serikali
 
Inaonekana neno 'wanyonge' limeshika kasi katika matumizi yake hapa Tanzania, na kutumiwa sana na baadhi ya wakuu kabisa wa nchi. Kwa mujibu wa baadhi ya machapisho, 'wanyonge' maana yake ni 'masikini sana', au 'watu wadhaifu katika jamii'. Kwa Kiingereza ni 'disadvantaged', 'abject poor', au 'weaker people.'

Sasa tangu tupate uhuru CCM wapo madarakani, iweje mpaka leo baadhi ya viongozi wao wakuu waliopewa dhamana bado wanalalamika juu ya uwepo wa wanyonge mpaka kufikia kusema wao ni viongozi wa wanyonge?

Kwa nini wanyonge hawajaisha?

Nani anasababisha uwepo wa wanyonge?

Na kusema kuwa mimi kama kiongozi mkuu nitatetea haki za wanyonge, je nani atatetea haki za wasiokuwa wanyonge? Nani anayetoa haki kwa wananchi? Au wasiokuwa wanyonge upata haki ndani ya sekunde?
a
 
Inaonekana neno 'wanyonge' limeshika kasi katika matumizi yake hapa Tanzania, na kutumiwa sana na baadhi ya wakuu kabisa wa nchi. Kwa mujibu wa baadhi ya machapisho, 'wanyonge' maana yake ni 'masikini sana', au 'watu wadhaifu katika jamii'. Kwa Kiingereza ni 'disadvantaged', 'abject poor', au 'weaker people.'

Sasa tangu tupate uhuru CCM wapo madarakani, iweje mpaka leo baadhi ya viongozi wao wakuu waliopewa dhamana bado wanalalamika juu ya uwepo wa wanyonge mpaka kufikia kusema wao ni viongozi wa wanyonge?

Kwa nini wanyonge hawajaisha?

Nani anasababisha uwepo wa wanyonge?

Na kusema kuwa mimi kama kiongozi mkuu nitatetea haki za wanyonge, je nani atatetea haki za wasiokuwa wanyonge? Nani anayetoa haki kwa wananchi? Au wasiokuwa wanyonge upata haki ndani ya sekunde?
Ni ukweli usiofichika kwamba kwenye nchi zetu hizi za kiafrika bado kuna Changamoto ya umasikini. Na waheshimiwa huwa wanalitumia hili neno "wanyonge" ilikupunguza kisaikolojia gap lililopo kati yao na wananchi wa kawaida kabisa wa hali ya chini.

Lakini ishu siyo kutumia neno wanyonge bali ishu ni kwa namna gani hao viongozi wanajitolea kuwasaidia hao wanyonge wenyewe..
 
Back
Top Bottom