Hivi hawa Watanzania 'wanyonge' wana sifa zipi? Na wanapataje hizo sifa?

Hivi hawa Watanzania 'wanyonge' wana sifa zipi? Na wanapataje hizo sifa?

Wanakubali kuswagwa kama kondoo. Hawawezi kusimama kudai haki zao hata wakiibiwa, wakidhulumiwa, wakitukanwa, wakidharaulika, wakitumiwa, wakidanganywa, wakiumizwa na kuuliwa.

Wao huwa na tabia ya kulalamika chini chini na kumwachia Mungu mateso yao. Watawala hufurahia hali hiyo kwakuwa hutawala bila hofu kwa kisingizio kuwa wanawatetea wanyonge kumbe wanawamaliza.

Msemakweli ni mpenzi wa Mungu. Au nasema uwongo ndugu zangu?
 
Binafsi mimi sio mnyonge! Hata kama nalala njaa au sina fwedhaaaaa ila mambo ya kuitana "MNYONGE" yaishue Lumumba tu hukohuko... [emoji847][emoji847]
 
Inaonekana neno 'wanyonge' limeshika kasi katika matumizi yake hapa Tanzania, na kutumiwa sana na baadhi ya wakuu kabisa wa nchi. Kwa mujibu wa baadhi ya machapisho, 'wanyonge' maana yake ni 'masikini sana', au 'watu wadhaifu katika jamii'. Kwa Kiingereza ni 'disadvantaged', 'abject poor', au 'weaker people.'

Sasa tangu tupate uhuru CCM wapo madarakani, iweje mpaka leo baadhi ya viongozi wao wakuu waliopewa dhamana bado wanalalamika juu ya uwepo wa wanyonge mpaka kufikia kusema wao ni viongozi wa wanyonge?

Kwa nini wanyonge hawajaisha?

Nani anasababisha uwepo wa wanyonge?

Na kusema kuwa mimi kama kiongozi mkuu nitatetea haki za wanyonge, je nani atatetea haki za wasiokuwa wanyonge? Nani anayetoa haki kwa wananchi? Au wasiokuwa wanyonge upata haki ndani ya sekunde?
Sifa:-
1) UWE MTOTO WA MKULIMA, MWALIMU, MCHUNGAJI au MFUGAJI->wale wa zamani.

2) UWE ULISOMA SHULE ZA KAWAIDA SIYO MIDIAM

3)KATIKA MAISHA YAKO UWE UMEWAHI KUCHUNGA MBUZI, KULIMA KWA JEMBE LA MKONO, KUTEMBEA PEKU, KUTEMBEA MWENDO MREFU KWENDA SHULE, KUISHI KWENYE NYUMBA ISIYO NA BATI

->Hii haijalishi hali ya maisha uliyo nayo sasa.
->Kwa vigezi hivyo wewe ni MNYONGE au MTOTO WA MASKINI
 
Inaonekana neno 'wanyonge' limeshika kasi katika matumizi yake hapa Tanzania, na kutumiwa sana na baadhi ya wakuu kabisa wa nchi. Kwa mujibu wa baadhi ya machapisho, 'wanyonge' maana yake ni 'masikini sana', au 'watu wadhaifu katika jamii'. Kwa Kiingereza ni 'disadvantaged', 'abject poor', au 'weaker people.'

Sasa tangu tupate uhuru CCM wapo madarakani, iweje mpaka leo baadhi ya viongozi wao wakuu waliopewa dhamana bado wanalalamika juu ya uwepo wa wanyonge mpaka kufikia kusema wao ni viongozi wa wanyonge?

Kwa nini wanyonge hawajaisha?

Nani anasababisha uwepo wa wanyonge?

Na kusema kuwa mimi kama kiongozi mkuu nitatetea haki za wanyonge, je nani atatetea haki za wasiokuwa wanyonge? Nani anayetoa haki kwa wananchi? Au wasiokuwa wanyonge upata haki ndani ya sekunde?
Dharau ya Viongozi Nchi hii Umasikini umeletwa na CCM na Majina yanatolewa na Hao Hao VIONGOZI
 
Inaonekana neno 'wanyonge' limeshika kasi katika matumizi yake hapa Tanzania, na kutumiwa sana na baadhi ya wakuu kabisa wa nchi. Kwa mujibu wa baadhi ya machapisho, 'wanyonge' maana yake ni 'masikini sana', au 'watu wadhaifu katika jamii'. Kwa Kiingereza ni 'disadvantaged', 'abject poor', au 'weaker people.'

Sasa tangu tupate uhuru CCM wapo madarakani, iweje mpaka leo baadhi ya viongozi wao wakuu waliopewa dhamana bado wanalalamika juu ya uwepo wa wanyonge mpaka kufikia kusema wao ni viongozi wa wanyonge?

Kwa nini wanyonge hawajaisha?

Nani anasababisha uwepo wa wanyonge?

Na kusema kuwa mimi kama kiongozi mkuu nitatetea haki za wanyonge, je nani atatetea haki za wasiokuwa wanyonge? Nani anayetoa haki kwa wananchi? Au wasiokuwa wanyonge upata haki ndani ya sekunde?
Sifa yakuwa Mnyonge ni kuwa MJINGA

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Kiukweli ni neno dhalilishi kwa wananchi na inashangaza linavyotumiwa Kama silaha ya viongozi kujificha huku wakiwahadaa kwa vitambulisho vya machinga. Huwezi kutaqala watu wako na kwa miaka mingi na ukawaita watu wako majina ya hovyo ni dharau kubwa.
Tatizo tumebatizwa jina la WANYONGE na kwa kiasi kikubwa tumelikubali, kwa kuwa tumewaachia watu wachache ndiyo wawe wenye kufikiri kwa ajili yetu. Tanzania ni ya watanzania wote si ya CCM wala Chadema wala ACT wala chama chochote si ya waislamu wala wakristo wala imani yoyote, wala si ya kabila lolote. Hili neno tulikatae kwani kuna kiongozi alishawaita watu wapumbavu, haya ni maneno ya dharau na kejeli kutoka kwa viongozi.
 
Back
Top Bottom