Hivi huu udwanzi wa 'Cover' kauleta nani?

Mkuu cover katika context ya muziki ndo nini? tusaidiane wengine hatuelewi
According to wikipedia....

In popular music, a cover version or cover song, or simply cover, is a new performance or recording of a previously recorded, commercially released song by someone other than the original artist or composer.
 
Hata baadhi ya thread humu JF hufanyiwa cover... yaani ni sawa na ku-update application kwenye android phone
 
Kuna wanaosema mbona Adele wimbo wake umerudiwa sana...ni kweli ila kwa mazingira na nafasi ya Adelle sio rahisi kuona tishio kwa wimbo wake kurudiwa na Wanamuziki wasio na majina, kwani hata huyo Mrudiaji naye hana cha kupoteza....ila mtu kama Joe hawezi kufanya hivyo bila kuwasiliana na Adele kwanza.

Manu Dibango angeweza kupotezea tu pale vionjo kutoka wimbo wake vilipotumiwa na Michael Jackson kwenye mziki wake...lakini kwa kuwa Dibango aliiona fursa akampeleka MJ mahakamani na kulipwa fidia....kumbuka ni kionjo tu sembuse wimbo mzima..ubunifu wa mtu/watu lazima uheshimiwe.

Tatizo tulilonalo huku kwetu kubwa ni la kutozingatia sheria mwanzo mpaka pale unapojitokeza mzozo ndio watu wanatafuta sheria ziko wapi.

Hiyo kazi uliyoirudia bila mazungumzo ikitokea kuanza kukupa dili usitarajie mwenye kazi yake atakaa pembeni na kukuangalia tuu, lazima mtashikana mashati...ni bora mmalizane mapema na labda hata unaweza kupata ruhusa bila malipo yoyote.

Kuheshimu sanaa ya ubunifu ni pamoja na kuwa na taratibu na sio kuacha kila mtu afanye anavyotaka...kila cover ya bongo ipate baraka ya mwenye haki miliki (kwa maandishi)....hizo za kina Adele zifanyeni tu mnavyotaka, coz ukishakuwa Mnyonge una kibali automatic cha kuhurumiwa na jamii kutoka mbinguni...na Adele hawezi hata kukutafuta akuulize.
 
Cover kama nchi za wenzetu kuna watu zinawapa pesa na umaarufu japo si sana laikn ni mtindo wa kawaida tuu

Kuna cover zna kuwaga kali kulko wimbo yenyewe
nakubaliana na wewe kabisa mkuu kuna cover huwa ni kali zaidi ya original kwa mfano ule wimbo wa hello- adelle, joe thomas aliufanyia cover kali sana. lakini nikirudi kwenye point ya mtoa mada sio issue sana kila wimbo kuutolea cover inarudisha nyuma creativity.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…