Mung Chris
JF-Expert Member
- Sep 12, 2017
- 3,391
- 3,849
Hawa wanawake wengine ni shida, ya ndani analeta hapa mtandaoni kweli dah. somenihapo chini (instagram)
Kilewo najua Haya siyo mageni kwako, tumeyaongea kwa muda mrefu sana. Tumewashirikisha watu wa karibu. Pamoja na hayo yote Kilichonishangaza sasa ni wewe kukataa kuniachia biashara zangu wakati wewe una za kwako. Tena unasaini akaunti yako peke yako halafu akaunti Yangu nimekuweka tunasaini Wote.
Kilewo kwa staili hiyo ya maisha nilianza kukosa Furaha sana na wewe kwa kuona unanitumia wala huna NIA Njema na Mimi, HUNIPENDI, HUNIJALI, huku Ndani MAPENZI YAKAPOTEA KABISA. Mpaka juzi birthday yako sikuwa najiskia kukuwish. Lakini kwa ajili ya Watoto nikajilazimisha. Ngoja niishie hapa.
KILEWO baba Watoto wangu, Dunia inajua NINAVYOKUPENDA. Tatizo langu kubwa na wewe unajua fika siyo wewe kutokuwa na Pesa, BALI KUTUSHIRIKISHA KWA KIDOGO UNACHOPATA wewe kama BABA wa Familia. kwa Sasa nina tatizo kubwa na wewe la kunipiga baada ya kuamua 2018 nitakuwa natoka peke yangu kujipa raha. Unajua sehemu ninazokuwaga nikiwa nimetoka na ndo sababu ulikuja ukanikuta, lakini uliamua kunipiga. Kesi ipo Dawati.
Kilewo ningekuwa na NIA mbaya nisingekuweka kwenye biashara Yangu, nimenunua Viwanja Goba na Bagamoyo, bila uwepo wako, lakini nilikuja kukushirikisha na wewe ukaenda kuongeza majina yako. Sikuwahi kulalamika maana NAKUPENDA na wewe ndo Baba Watoto wangu. Nimetamani kuzaa mtoto wa Tatu lakini kwa ambushi zako nimeogopa. Mambo ya KOMAA KAMANDA hapana. Nikasema Wawili wanatosha.
Kilewo wangu nakuomba tena na tena uniachie biashara zangu niweze kuendelea kutunza hawa Watoto wetu. Toka unipige umeondoka siwezi kutoa ela, hatuna Chakula nyumbani, Madeni ya wafanyakazi, Nyumba nadaiwa n.k
[HASHTAG]#SIRIZANDANI[/HASHTAG]
- joycekiriasuperwoman
Kilewo baba Watoto wangu, yaliyotokea ilibidi yatokee ili kila Mmoja aanze upya safari ya Maisha Yake. Wakati tunaanza huu mwaka nilikuambia huenda mwaka huu tukaachana! Unakumbuka? Well, Lakini jambo moja nakusisitiza hapa, Nimekuomba sana uniachie biashara zangu nisimamie, ili na wewe usinamie biashara zako kutokana na Changamoto zetu hasa za kiuchumi. Wewe Pesa zako unazopata kwenye biashara zako hutaki kushea, Ila Pesa zinazotoka kwenye biashara zangu unataka tushee. Najua ni ujinga wangu wa kukupenda sana ndo umeniponza. Labda ningetenganisha Mapenzi na biashara tusingeishia huku.
Wakati mimi nasajili Kampuni Yangu nilikuweka kwenye kampuni bila shida yoyote na wakati nafungua akaunti za bank nilikuweka pia. umekuwa ukijua kila ela inayoingia pamoja na matumizi yote kwa sababu lazima tusaini Wote na ndiyo Raha ya Mapenzi.
Wewe ulipofungua Kampuni yako uliweka pia jina langu kitu ambacho nilipenda sana, lakini ulipokwenda kufungua akaunti ya bank HUKUNIWEKA. Kiukweli SIKUPENDA, mbaya zaidi ukataka kuwa unasaini Pesa zako kivyako.
Japo nilianza kuona mashaka Lakini nilijipa Moyo, labda ukipata utanishirikisha pia kama Mimi nilivyoamua kukushirikisha kila kitu changu. PESA MWANAHARAMU buana, pale tuu ulipoanza kazi na kampuni yako Ndipo SHIIIDA ilipoanzia, hukutaka kushea hata senti Nyumbani wakati biashara zangu kwa Kipindi chote cha Miaka NANE zimeendesha familia yetu bila tatizo.
Kuna Miradi mbalimbali ambayo ulikuwa ukionyesha NIA ya kuifanya lakini yote ilifeli. Hivyo haikuwa rahisi KUKUJUA kwa upande wa KIUCHUMI sura yako ikoje... Ulijaribu biashara hizo kwa mtaji wa Familia bila kuona matokeo chanya, Pesa zikawa hazirudi lakini tukajipa Moyo biashara ndivyo zilivyo. Mwisho nikakushauri mtaji wa biashara tukope Bank labda utakuwa na nidhamu zaidi ya Pesa ya Mkopo kuliko kutoa ela Nyumbani. Hukupenda huo Ushauri, ukaona nakubania.
Sasa MWAKA huu 2018 tuliongea mengi pale Bahari beach, juu ya mahusiano Yetu na Changamoto zake! Pamoja na yote tuliyoongea nikakuomba kila mtu asimamie biashara zake, kisha tukubaliane kwenye MAJUKUMU ya Familia kwamba nani atafanya Kipi. Lakini pia nikakuambia kwamba Niko radhi kuendelea kutimiza hayo majukumu. [HASHTAG]#SIR[/HASHTAG]
Kilewo najua Haya siyo mageni kwako, tumeyaongea kwa muda mrefu sana. Tumewashirikisha watu wa karibu. Pamoja na hayo yote Kilichonishangaza sasa ni wewe kukataa kuniachia biashara zangu wakati wewe una za kwako. Tena unasaini akaunti yako peke yako halafu akaunti Yangu nimekuweka tunasaini Wote.
Kilewo kwa staili hiyo ya maisha nilianza kukosa Furaha sana na wewe kwa kuona unanitumia wala huna NIA Njema na Mimi, HUNIPENDI, HUNIJALI, huku Ndani MAPENZI YAKAPOTEA KABISA. Mpaka juzi birthday yako sikuwa najiskia kukuwish. Lakini kwa ajili ya Watoto nikajilazimisha. Ngoja niishie hapa.
KILEWO baba Watoto wangu, Dunia inajua NINAVYOKUPENDA. Tatizo langu kubwa na wewe unajua fika siyo wewe kutokuwa na Pesa, BALI KUTUSHIRIKISHA KWA KIDOGO UNACHOPATA wewe kama BABA wa Familia. kwa Sasa nina tatizo kubwa na wewe la kunipiga baada ya kuamua 2018 nitakuwa natoka peke yangu kujipa raha. Unajua sehemu ninazokuwaga nikiwa nimetoka na ndo sababu ulikuja ukanikuta, lakini uliamua kunipiga. Kesi ipo Dawati.
Kilewo ningekuwa na NIA mbaya nisingekuweka kwenye biashara Yangu, nimenunua Viwanja Goba na Bagamoyo, bila uwepo wako, lakini nilikuja kukushirikisha na wewe ukaenda kuongeza majina yako. Sikuwahi kulalamika maana NAKUPENDA na wewe ndo Baba Watoto wangu. Nimetamani kuzaa mtoto wa Tatu lakini kwa ambushi zako nimeogopa. Mambo ya KOMAA KAMANDA hapana. Nikasema Wawili wanatosha.
Kilewo wangu nakuomba tena na tena uniachie biashara zangu niweze kuendelea kutunza hawa Watoto wetu. Toka unipige umeondoka siwezi kutoa ela, hatuna Chakula nyumbani, Madeni ya wafanyakazi, Nyumba nadaiwa n.k
[HASHTAG]#SIRIZANDANI[/HASHTAG]