Hivi huyu Vandernbroeck anatutafuta nini Wanamsimbazi?

Nimetizama uchambuzi wa Azam tv kwa kweli pale hakuna kocha, naamini huyu kocha anazidiwa uwezo na seleman matola tena na makocha wengi wa bongo, sema sisi watu weusi tatizo letu tunaabudu sana ngozi nyeupe.
 
Basi mimi ni mtu pekee niliyemkataa kocha hata baada ya ushindi wa goli 3.

Timu ina wachezaji wenye vipaji vikubwa sana lakini tatizo linaonekana ni mwamuzi.

Mpira uko na pace ya chini mno kiasi kwamba kwamba kupata matokeo,kunategemea timu unayocheza nayo wasiwe na morali pia.Ukikutana hata na timu ya daraja la 3 yenye morali huwezi shinda kwa kasi ile ya mpira.

Hatuingilii kazi ya mwalimu lakini tunaona amekosa mbinu mpya kuvitumia vipaji vilivyopo
 
Tatzo sio coach tatizo wachezaji mkuu wamekosa Sana magoli

Sent from my Infinix X690 using JamiiForums mobile app
 
Kwako GENTAMYCINE anasemaje🤣🤣🤣🤣🤣
 
Hakuna aliyesema tunataka tuwe tunashinda game zote daima, ila pia hakuna shabiki aliye tayari kuona timu inapata matokeo kwa bahati nasibu au kufungwa kizembe zembe.

Hivi umefatilia performance ya Simba kwenye hizi game tatu za mwisho (mbili za VPL na hii ya CL) ? Hii Simba inayowatia pressure mashabiki wake wenyewe wewe unaona iko sawa? Hakuna aliyesema tunataka tuwe tunashinda game zote daima, ila pia hakuna shabiki aliye tayari kuona timu inapata matokeo kwa bahati nasibu au kufungwa kizembe zembe.

Hivi umefatilia performance ya Simba kwenye hizi game tatu za mwisho (mbili za VPL na hii ya CL) ? Hii Simba inayowatia pressure mashabiki wake wenyewe wewe unaona iko sawa?
 
Hapo utaona tofauti ya simba na yanga, simba hawana subira ni jazba tu, si watu wa kufanyanha utafiti.

Mtu kama haji manara atawasidia nini mropokaji yule shule hamna.

Ukitaka kumlaumu Kishingo, Anza na MO, na uongozi wote wa simba

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Mwanzo wa mwisho wana Simba

Ile peak ya mafanikio kwa kikosi husika ilishapita zamani ikifika pale Simba ilivyotinga robo fainali CAF

BAADA YA pale curve ikaanza kubend

Na Sasa wananchi Ni zamu curve inaaanza kupanda

Kutesa kwa zamu
Ligi bado mbichi.Hata Everton/Tottenham/Southampyon ziliwahi kuongoza kuleee!
 
Hivi wewe ukocha ulisomea wapi?
Nilisomea pale Mpapai wa Mbao Academy.

Kwani unataka kusema nini hapa,kwamba kwakuwa sikusomea ukocha basi sipaswi kukosoa mbinu,mfumo na hulka ya kocha Sven Vandernbroeck?

Mkuu,hiyo ni sawa na kusema sisi Wanatanzania tulikosea kuwakosoa wale Madaktari bingwa wa Muhimbili waliomfanyia upasuaji wa kichwa mgonjwa aliyepaswa kufanyiwa upasuaji wa mguu kwakuwa tu hatujasomea udaktari. Na hata Mahakama iliyoamuru huyo mgonjwa alipwe mamilioni kwa kosa hilo lililofanyoka,baada ya miaka kadhaa kupita, nayo ilifanya makosa kwavile hao Mahakama haina utaalamu wa mambo ya tiba.
 
Kwa iyo kwa mawazo yako unaona Simba mechi ya juzi na Fc platinum walifungwa kizembe zembe sio?
Kweli wee hupendi mpira unaipenda simba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…