Pre GE2025 Hivi inteligensia ya Polisi ipo CHADEMA pekee?

Pre GE2025 Hivi inteligensia ya Polisi ipo CHADEMA pekee?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Najiuliza swali kubwa Sana. Hivi inteligensia ya Polisi wa Tanzania ni Kwa CHADEMA tu?. Yani CHADEMA ndio pekee wanaomulikwa na polisi?

Binti anabakwa na vijana Sita na polisi hawajui mpaka Video ilipowekwa hadharani ndipo wakaanza kuhaha ila mpaka Leo hakuna hatua iliyochukuliwa. Nikawa najiuliza Kama Jambo baya Kama Hilo linafanyika na polisi hawajui, je inteligensia yao ni kubwa kiasi gani?. Cha kushangaza polisi wasiokuwa na intelejensia kwenye makosa ya jinai, wanakuwa wepesi kuwa na intelejensia kwenye siasa hasa Kwa chama Cha CHADEMA.

Kwenye Ziara ya Makonda kipindi akiwa mwenezi wa CCM ilionekana wazi polisi wamezidiwa na kupotea Kwa watu. Watu wanatekwa na watu wasiojulikana na kupotelea kusikojulikana na polisi wapo kimya. TLS wameitoa orodha ya watu waliopotea mpaka Leo wanaokaribia 80 ila Polisi wapo kimya Kama hawajui chochote.

Polisi hawajui nani alimshambulia Lissu, polisi hawajui Ben Sanane alipotelea wapi na polisi hawajui Azory Gwanda alipotelea wapi?. Yani itelijensia yao imefikia kikomo. Lakini inteligensia yao ipo juu linapofika suala la CHADEMA ndio utaona unafiki wao.

Polisi badilikeni acheni ujinga.

PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - Hivi hili swali la Oscar Oscar kati ya CCM na jeshi la Polisi nani wanaotakiwa walijibu?
 
Ni kweli raisi wetu hajui lolote juu mambo ya Mbeya. Mbona hakuna tamko lolote? Kwa sababu anapaswa kupewa taarifa kikatiba (ibara ya 32(1) ya hali ya usalama wa nchi.

Viongozi wa CHADEMA mbona wanashushwa hadhi na kuwa kama panya wkt ni viongozi wakubwa pia ktk nchi yetu wanaowakilisha watu wengi sana nchini? Hii inatupeleka wapi?

Uvunjivu wa amani uko upande mmoja tu kila siku na wakati hakuna data zinazothibitisha wao ni wavunjaji wa amani katika taifa mara ngapi na wanawatumia nani kuvunja amani. Mbona juzi tu Mwanza mkutano wa mbunge Mabula ilikuwa hali tete hadi mkutano kuvunjika!

Mbona hatuwaoni ma RPC na makamishna kuwakamata vijana wa CCM waliovunja huo mkutano kwa vurugu? Mimi ni CCM, naipenda sana nchi yangu. Hii siyo!

Waacheni vyama vya siasa wajinadi kama tulivyo huru kujinadi CCM. Tutekeleze 4R za Raisi kwa moyo mmoja na siyo kwa maneno tu hapa polisi wametumia excessive force and with impunity.
 
Najiuliza swali kubwa Sana. Hivi inteligensia ya Polisi wa Tanzania ni Kwa CHADEMA tu?. Yani CHADEMA ndio pekee wanaomulikwa na polisi?

Binti anabakwa na vijana Sita na polisi hawajui mpaka Video ilipowekwa hadharani ndipo wakaanza kuhaha ila mpaka Leo hakuna hatua iliyochukuliwa. Nikawa najiuliza Kama Jambo baya Kama Hilo linafanyika na polisi hawajui, je inteligensia yao ni kubwa kiasi gani?. Cha kushangaza polisi wasiokuwa na intelejensia kwenye makosa ya jinai, wanakuwa wepesi kuwa na intelejensia kwenye siasa hasa Kwa chama Cha CHADEMA.

Kwenye Ziara ya Makonda kipindi akiwa mwenezi wa CCM ilionekana wazi polisi wamezidiwa na kupotea Kwa watu. Watu wanatekwa na watu wasiojulikana na kupotelea kusikojulikana na polisi wapo kimya. TLS wameitoa orodha ya watu waliopotea mpaka Leo wanaokaribia 80 ila Polisi wapo kimya Kama hawajui chochote.

Polisi hawajui nani alimshambulia Lissu, polisi hawajui Ben Sanane alipotelea wapi na polisi hawajui Azory Gwanda alipotelea wapi?. Yani itelijensia yao imefikia kikomo. Lakini inteligensia yao ipo juu linapofika suala la CHADEMA ndio utaona unafiki wao.

Polisi badilikeni acheni ujinga.

PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - Hivi hili swali la Oscar Oscar kati ya CCM na jeshi la Polisi nani wanaotakiwa walijibu?
Uhuni wa kujipendekeza tu ili kupanda vyeo , ila pia hufanya hivi kutengeneza upigaji , mfano majuzi unafikili ilitumika sh ngapi ,ila safari hii police wote waliohusika wapo na bahati mbaya sana.
 
Sawa ndugu yangu. Ni maswali tu kichwani. Naona kama nachanganyikiwa kwa ninachikiona kama mwanachama wa CCM
Kisera bado Chadema hamna kitu nataka tu waachiwe. Wasikamatwe kamatwe kututia doa. Waongeeee mpaka basi.
 
Uhuni wa kujipendekeza tu ili kupanda vyeo , ila pia hufanya hivi kutengeneza upigaji , mfano majuzi unafikili ilitumika sh ngapi ,ila safari hii police wote waliohusika wapo na bahati mbaya sana.
Binafsi nahisi sera za polisi juu ya vyama vya siasa ni lazima ziangaliwe upya ili wafanye balance ya Ibara ya 18 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano na Sheria namba 16 ya makosa ya jinai. Wangekamatwa kama wameleta vurugu lkn sio kama inawezekana wakaleta vurugu. Tuwe na uhakika wa ushahidi kwamba vurugu imetokea
 
Binafsi nahisi sera za polisi juu ya vyama vya siasa ni lazima ziangaliwe upya ili wafanye balance ya Ibara ya 18 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano na Sheria namba 16 ya makosa ya jinai. Wangekamatwa kama wameleta vurugu lkn sio kama inawezekana wakaleta vurugu. Tuwe na uhakika wa ushahidi kwamba vurugu imetokea
Siku zote mtaji wa mapolice tz ni chadema
 
Umeelewa usijitoe kwenye reli
Dr. Santos, mzazi wangu aliwekwa kizuizini mwaka 1955 na wakoloni akimtetea mwalimu Nyerere ktk harakati za uhuru wetu, wakamwachia. Ni mwanzilishi wa TANU pia. Nimekuwa CCM miaka yote ya maisha yangu ingawa sijawahi kugombea hata ujumbe wa nyumba 10 na sio kwamba siwezi. Mwl Nyerere na mama Maria ni family friends wa familia yetu na Butiama ndio nyumbani kwangu. Natetea tu maslahi ya chama changu na nchi. Ni lazima tuwe na mabomba ya mawasiliano kati ya chama chochote kinachotawala na upinzani hata kama chama kinachotawala ni CHADEMA mimi sijali kama ni matakwa ya wananchi na mimi ni CCM. Nchi kwanza vyama badae. Hapa ninachoona vyama vya siasa havina meseji inayoshawishi watu na ni mtu kama Tundu Lisu(confrontantional politics) anayeongea kila siku kwa kutoa mapovu mdomoni bila hekima na siasa za kimtikila, za kibaguzi, ulaghai , matusi na kwa nia ya kuigawa nchi. Hazifai lkn hiyo ni juu yao. Hata hivyo Watanzania sio wajinga. Wanajua tunakosea wapi na wanakosea wapi. Kura zao zinapigwa kwa matokeo hayo niliyoyasema. Nataka tu polisi wawe less involved. Watuachie tuchuane.
 
Dr. Santos, mzazi wangu aliwekwa kizuizini mwaka 1955 na wakoloni akimtetea mwalimu Nyerere ktk harakati za uhuru wetu, wakamwachia. Ni mwanzilishi wa TANU pia. Nimekuwa CCM miaka yote ya maisha yangu ingawa sijawahi kugombea hata ujumbe wa nyumba 10 na sio kwamba siwezi. Mwl Nyerere na mama Maria ni family friends wa familia yetu na Butiama ndio nyumbani kwangu. Natetea tu maslahi ya chama changu na nchi. Ni lazima tuwe na mabomba ya mawasiliano kati ya chama chochote kinachotawala na upinzani hata kama chama kinachotawala ni CHADEMA mimi sijali kama ni matakwa ya wananchi na mimi ni CCM. Nchi kwanza vyama badae. Hapa ninachoona vyama vya siasa havina meseji inayoshawishi watu na ni mtu kama Tundu Lisu(confrontantional politics) anayeongea kila siku kwa kutoa mapovu mdomoni bila hekima na siasa za kimtikila, za kibaguzi, ulaghai , matusi na kwa nia ya kuigawa nchi. Hazifai lkn hiyo ni juu yao. Hata hivyo Watanzania sio wajinga. Wanajua tunakosea wapi na wanakosea wapi. Kura zao zinapigwa kwa matokeo hayo niliyoyasema. Nataka tu polisi wawe less involved. Watuachie tuchuane.
Ccm wamefanya chombo cha umma kama police kuchukiwa na wananchi , umeshauri vizuri juu ya chama chako , ila kama huna wadhifa ndani ya chama huwezi sikilizwa na chama chako
 
Kisera bado Chadema hamna kitu nataka tu waachiwe. Wasikamatwe kamatwe kututia doa. Waongeeee mpaka basi.
Chadema wanachakuongea tena kikubwa tu ndo maana hata viongozi na wanachama wake wakihongwa na kujiunga na ccm hupewa vyeo. Mfano mashinji, lijualikali nk
Sera=sela?
 
Ccm wamefanya chombo cha umma kama police kuchukiwa na wananchi , umeshauri vizuri juu ya chama chako , ila kama huna wadhifa ndani ya chama huwezi sikilizwa na chama chako
Hilo ni neno kubwa. Nakubali lkn mimi kama mimi naamini kwa upenzi nilionao nitasikilizwa. Hiki chama kimetoka mbali na kinabadilika. Na sisi wanachama tunabadilika.
 
Hilo ni neno kubwa. Nakubali lkn mimi kama mimi naamini kwa upenzi nilionao nitasikilizwa. Hiki chama kimetoka mbali na kinabadilika. Na sisi wanachama tunabadilika.
Mkuu ccm ile kwa sasa,
Ccm ya kipindi kile haikuwa na machawa , ya sasa ipo na makunguni na ndo wanajifanya kukijua chama kuliko.

Kuna clip moja hivi mzee mmoja anakili kwamba ccm ya sasa sio ile ya mwalim au enzi zile ya sasa ni yawahuni
 
Back
Top Bottom