Hivi katika mfumo wa fahamu kuna njia kwenye sikio hadi kooni?

wa stendi

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2016
Posts
25,190
Reaction score
27,434
Wakuu poleni na kazi!!
Katika mfumo wa fahamu hivi kwenye sikio kuna njia yeyote inayopita hadi kwenye koo!!nauliza hivi kama kuna madoctor humu naomba kujuzwa kwa sababu mi jana sikio langu lilikuwa linauma nikanunua dawa ile ya tube!wakati nimeweka tone moja sikioni baada ya dakika 2 ile dawa nikaisikia hapa kooni kama kohozi fulani!!hivi wakuu ndo mfumo ulivyo au ni mimi tuu!!
Na nimejaribu kucheki hapa nikashindwa maana mi si mtaalam wa haya mambo naomba kama kuna doctary humu anijuze!!
 
Sio mfumo wa fahamu. Kasome mfumo wa sikio ndo utaelewa.
Kuna uhusiano
 
kheeee hiyo picha inatisha sana kuiangalia duuu kumbe sisi binadamu kwa ndani tuko hivyo
 
Umenikumbusha jambo ambalo nami lilipata kunishangaza, nilikwenda hospital, nikawekwa dawa kwenye jicho, baada ya dakika kadhaa nikasikia ladha chungu sana mdomoni
 
mleta mada ni kweli kunamawasiliano,
so usidhan kwamba ulivyoisikia dawa kooni ni tatizo,no.
Pua na sikio vinakutana kwenye koo
 
Umenikumbusha jambo ambalo nami lilipata kunishangaza, nilikwenda hospital, nikawekwa dawa kwenye jicho, baada ya dakika kadhaa nikasikia ladha chungu sana mdomoni
usishangae ukadhani ni shida,
issue ni kwamba dawa ya macho(ya maji) inapowekwa huingia kwenye mfereji wa machozi(nasoracrimal duct) ambao huipeleka mpaka puani.
Au hujawahi kuona unapolia kamasi nyepesi zinatoka? Ile huwa ni machozi yaliyopitia kwenye huo mfereji hivyo baadhi huingia kooni na nyingine hutokea puani
 
Ni kweli mkuu

Kwa kifupi tu, sikio lako limegawanyika sehemu tatu, outer ear, middle ear na inner ear

Hii sehemu ya inner ear imeunganisha na koo lako kupitia eustachian tube.

Tube hii husaidia kusawazisha pressure ndani ya sikio lako
 
Ni kweli mkuu

Kwa kifupi tu, sikio lako limegawanyika sehemu tatu, outer ear, middle ear na inner ear

Hii sehemu ya inner ear imeunganisha na koo lako kupitia eustachian tube.

Tube hii husaidia kusawazisha pressure ndani ya sikio lako
Mkuu asante kwa kunifungua macho maana nilishtuka sana maana niliweka dawa kwenye sikio nikaisikia hadi kooni kama nimeinywa vile!!
 
Umenikumbusha jambo ambalo nami lilipata kunishangaza, nilikwenda hospital, nikawekwa dawa kwenye jicho, baada ya dakika kadhaa nikasikia ladha chungu sana mdomoni
[emoji15] [emoji15] [emoji15] [emoji87] [emoji87] [emoji87] [emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Umenikumbusha jambo ambalo nami lilipata kunishangaza, nilikwenda hospital, nikawekwa dawa kwenye jicho, baada ya dakika kadhaa nikasikia ladha chungu sana mdomoni
Hiyo nafikiri itakuwa ciproflaxcian ya jicho
 
Kama nimekosea naomba kurekebishwailaijuavyo ni kwamba eustechian tube ipo nyuma ya ngoma ya sikio kazi yake nikubalance pressure ya inner ear, dawa unaisikiaje? Jicho na pua kuunganika ipo wazi maana kuna muda ukipenga kamasi kwa presha kubwa unashangaa kiasi kidogo vha kamasi kinatokea jichoni
 
Je hii eustachian tube inaweza kuziba? Na ikiziba kuna namna ya kuzibua?
 


Thanks
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…