Hivi kuna kocha bora amewahi kutokea Ulaya kama Jose Mourinho?

Carlo Ancelotti, Zidane and Paisley ndio makocha wenye UEFA Champions tatu .. Mourinho kachukua mbili tu
Mourinho anawazidi rekodi ya kuchukua ktk nchi 3 tofauti na kubeba vikombe vya ligi kuu za nchi mbali mbali nyingi duniani kuliko hao wote uliowataja.

Ukiulizia ktk miaka 15 iliyopita Kocha yupi aliyepata mafanikio tele ktk nchi tofauti zaidi ya 1 ni Jose Mourinho ndiye atayekuwa anaongoza.
 
Wale ni wacheza wa la masia, kwan man utd hakuna?[emoji3]
Pep ni kocha bora kuliko maurinho, maurinho alikwa madrid yenye wachezaji wakubwa na wa thamani kuhwa lakin hakumfikia pep kwa mafanikio[emoji3]
Tena acha kabisa kuufananisha huo uchwaro wako na Special One, nimeshakula pesa nyingi sana kwa wajinga wasiojua ubora wa Mourinho kwa kulinganishwa na hilo libaguzi lako la rangi.
 
wewe mgonjwa akili,ni sawa na kumwambia mtoto

Wa masikini kwani kakatazwa kusoma shule za feza bdala za kayumba ili afaulu
Una shida ya kufikiri mahala, mfano uliotoa na swali uliloulizwa haviendani kabisa. Hakuna mantiki.
 
ndomana wamemtimua mourinho,kanunua pogba,lukaku,fred bdo akawa anataka kununua wakati ferguson hakuwa na matumizi hayo,matumizi hayo zinafanya timu zinazonunua hadhi man city na chelsea
Huu ni utaahira kutaka Morinyo awe kama Alex, ni sawa na kutaka Trump afanye kama Obama, huo utakua utaahira. Kila mtu yuko yeye na ana mbinu zake.
 
Kwani makocha wengine wanakatazwa kununua wachezaji?
 
Jose ni specialist wa mpira wa Ulaya.

Alianza Porto, haikua na kombe, akaipa makombe. Akaja Chelsee, haikua inajulikana akaipa mataji.

Akaenda Inter, AC Milan ilishaitoa Inter barabarani, Josee akairudisha road na mataji juu.

Baada ya Madrid kukosa vikombe kwa misimu kadhaa wakamuomba mtaalam awasaidie, baada ya Josee kufika pale akawa anajitwisha tu makombe.

Chelsee wakamtaka tena, akarudi na akawasaidia pale alipoweza wakamtimua.

Man wakamuomba awasaidie angalau kucheza champions leage baada ya kuikosa kwa misimu kadhaa, kweli alipofika pale Manchester wakacheza champions leage.

Binafsi hata mimi ukiniuliza kocha anaeujua mpira wa ulaya siwezi kuacha kumtaja huyu jamaa.
 
Man U inahitaji matengenezo ya juu ambayo hayategemei kocha pekee, so Mourinho alistahili kufukuzwa lkn bila shaka ss hv atakuwa anaonekana umuhimu wake laiti Man U wangesajili kikosi kipya kabisa km ilivyofanya Man City
Baada ya kumtimua, matokea yamekua mazuri sasa?
 
Naomba uzi uishie hapa hapa maana umemaliza kila kitu Chifu.

Mourinho ataendelea kuwa Special One wa muda wote japo akijirekebisha ktk kutokosana na Wachezaji ataendelea zaidi ya hapo.

Kwa ball position hayuko vzr kiviiile lkn kwa mbinu za ushindi hakuna Kocha yeyote awezaye kufikia rekodi yake.
 
Nakubaliana nawe mtoa Mada..
Kwenye list ya makocha bora mou lazima awepo.. haina haja ya kuweka rekodi zake, mataji yake wakati iko wazi kabisaa ni kujichosha.
hao wanaosema kuwa ullianza kushangilia mpira Juzi.. wao ndo wameanza kushangilia mpira Juzi baada ya mou kufanya vibaya na wale mabishoo kina pogba!. Wengine wanasema pep. hivi pep ni wazamani??
Kitakwimu pep kwa mou bado sana.
Mou ile mechi ya UEFA na barca hapa juzi angewapiga barca live kabisaa.. (hapa watu watanijia juu) pep kwa mou bado ni mwanafunzi kama vile mou alivyo mwanafunzi kwa Louis Van gal!!
Pep toka ameondoka barca UEFA hajachukua tena! Pale Bayern aliletwa special kwa ajiri ya UEFA na sio kombe lile la bundersliga! Licha ya yeye kubomoa ile borussia aliyoitengeneza jugern klop lakini bado mfupa wa UEFA ulimshinda! Madrid walijipigia nje ndani sita zile! Athletico Madrid walijipigia nao.. akabaki kuchukua bundersliga mpka Bayern wakachoka!
Siku zote falsafa ya pep ni kudhoofisha wapinzani kwa kuwabomolea kikosi!..yaani anakudhoofisha kwa kukuchukulia silaha zako ili akupige ukiwa hauna kitu!.. Sasa Licha ya usajili wote alioufanya lakini angalia UEFA inavyomtoa jasho!.. mambo anayoyafanya pep mou alishafanya zamani! kilichobaki ni kurudia (hapa simaanishi mfumo na tactical,open play)
Pep is not mature enough.. Usizungumzie barca maana ile barca ilitokea kutoka mbinguni!.. Kuna wakati pep amekunja nne katulia tuu hana wasiwsi anajua ule utatu mtakatifu utafanya kazi, nao ule utatu ulitii..

Kwangu Mimi kipimo cha pep kuwa kocha aliyekomaa kwa tactical, formation, ni kuchukua UEFA tuu nje ya ile barca!!
Utawezaje sasa kumfananisha na mou?? mtu ambaye anaweza kwenda hapo juve na kuweka cv yake mezani na mabosi wakatetemeka kwa hofu kuu??
Tatizo la mou ambalo linamfanya kwa sasa aonekane ni kocha mbovu..
ni ule mfumo wake kupitwa na muda..!
Ninaposema muda namaaanisha kwanzia soka lenyewe la sasa limebadilika kwa kiasi kikubwa.
Wachezaji nao wa sasa wako soft mnoo kutokana na soka lilivyobadilika!
Watu kama Drogba, Michael essien , Javier zaneti waliweza kucheza mfumo ule wa mou bila shida yoyote ..
Lakini pogba, Jesse lingald na Anthony martial nao unategemea wacheze mfumo wa kupaki basi??? no way!
Kinachompa soko pep kwa sasa ni ile modern football yake, yenye udambwiudambwi mwingi,

Pep is not mature enough.
Mourinho is the best..

Nawasilisha ndugu mtoa Mada
 
Wale ni wacheza wa la masia, kwan man utd hakuna?[emoji3]
Pep ni kocha bora kuliko maurinho, maurinho alikwa madrid yenye wachezaji wakubwa na wa thamani kuhwa lakin hakumfikia pep kwa mafanikio[emoji3]
Madrid walimnunua Mourinho ili kuvunja utawala wa Baka, pamoja na kwamba hakuchukua UEFA lakini aliondoka baka ikiwa underdog kwa Madrid.
 
Zaidi ya SAF hakuna mwingine.
 
Huyu ananunua mataji,pale city first eleven yote wapya kasoro sterling na fenandinho..angalia katumia kiasi gani cha pesa ukilinganisha na wenzake
Club imetumia 1bn kujijenga, wakati Man U wametoa 1bn kwa wamiliki wa club
 
Yeyote anayepinga hili ujue Mou kamuumiza na club yake. Poleni ni mambo ya soka tu
 

Mi napingana na ww kwa maana namuona Mourinho ni kocha wa kawaida kama wengne tu. Naongea haya kwa hoja zifuatazo.
1. Inatokea muda fulan kocha akakutana na wacheaji ambao anaendana nao wakamuelewa mpaka ikafikia kuchukua ubingwa, tumeliona hilo kwa makocha wengine pia kama Raniel akiwa Leicester city alibeba ubingwa from nowhere.
2. Morinho alipendwa zaid baaya ya kuwaondoa Barca nusu fainal mwaka 2010 timu ambayo watu wengi kwa kipind kile wapenz wengi wa mpira waliichukia hasa mashabiki wa ligi ya uingereza hasa baada ya kuipiga Manchester United mwaka 2009.
3. Ni kocha wa muda mfupi kwa matumizi. Kwa maana hawez kukaa muda mrefu kwenye timu kutokana na tabia zake za mikwaruzo either kwa management au wachezaji. Hili sina haja ya kulisema maana kila mmoja anajua kila anakopita lazma watu waparurane.
4. Kipindi Morinho anaanza makeke yake soka lilikua limetawaliwa na makocha wazee so yeye alikua miongon mwa vijana machachar kwenye hiyo tasnia. Ukitaka kuona hilo angalia sasa hv ambapo vijana ndio wametawala soka la dunia kwa upande wa makocha na wachezaji kiujumla si unaona anavyohaha kutaka kurudisha heshima yake halaf watu wanamchapa tu[emoji23]
Naomba nihitimishe kwa kusema kwamba ni kocha mzur ila sio kwa hzo sifa unazo mmwagia mkuu.
........Choupa moting safarini chunya.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…