Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,409
- 13,262
Ukiangalia teuzi za rais ni kama kuna list ya watu ambayo huwa tayari imeandaliwa kwaajili ya kuteuliwa. Yaani teuzi zinawazungukia wale wale.
Unakuta mtu akikosa ubunge au uwaziri atapata uRC, DC, DAS, DED au ukatibu mkuu. Mwingine unakuta alishapita vyeo vingi sasa kesha anza maisha mapya Mara unasikia anapewa uDAS ghafla tena anabadilishwa kuwa RC.
Mwingine unakuta alikuwa na vikashfa awamu zilizopita ghafla unashangaa ni RC tena. Wengine unakuta ni watoto wa viongozi wastaafu au waliokufa.
Yaani kuna watu wanaishi kwa kubadilishiwa vyeo. Mwingine unakuta ni mteule wa kudumu toka enzi za baba wa taifa. Teuzi nyingine kama hizi za maRC unakuta ni kuhamishana tu wale wale.
Sasa unajiuliza hivi wenye sifa hakuna kabisa hadi kuanza kurudia rudia hata wastaafu? Ndipo nikawaza kwamba inawezekana kuna data base ya wateule ambao huwa wanasubiri muda tu wa kukamata vyeo vyao.
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Au nasema uwongo ndugu zangu?
Sent from my TECNO P701 using JamiiForums mobile app
Unakuta mtu akikosa ubunge au uwaziri atapata uRC, DC, DAS, DED au ukatibu mkuu. Mwingine unakuta alishapita vyeo vingi sasa kesha anza maisha mapya Mara unasikia anapewa uDAS ghafla tena anabadilishwa kuwa RC.
Mwingine unakuta alikuwa na vikashfa awamu zilizopita ghafla unashangaa ni RC tena. Wengine unakuta ni watoto wa viongozi wastaafu au waliokufa.
Yaani kuna watu wanaishi kwa kubadilishiwa vyeo. Mwingine unakuta ni mteule wa kudumu toka enzi za baba wa taifa. Teuzi nyingine kama hizi za maRC unakuta ni kuhamishana tu wale wale.
Sasa unajiuliza hivi wenye sifa hakuna kabisa hadi kuanza kurudia rudia hata wastaafu? Ndipo nikawaza kwamba inawezekana kuna data base ya wateule ambao huwa wanasubiri muda tu wa kukamata vyeo vyao.
Msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Au nasema uwongo ndugu zangu?
Sent from my TECNO P701 using JamiiForums mobile app