Hivi kupigwa kibuti na mpenzi au kufiwa na mpenzi ipi inauma sana

Hivi kupigwa kibuti na mpenzi au kufiwa na mpenzi ipi inauma sana

<b>Mi nikiwa naye huwa naomba yote hayo yasinitokee,ila ikitokea akanipiga kibuti ndio huwa naona bora afe tu,na wakati mwingine namuombea hata akutane na nyoka nikiwepo ili mimi nimsaidie nyoka amng`ate vizuri.</b>
Duh! Inaonekana una wivu kiasi ambacho upo tayari hata kuua kuliko kuachwa.
 
Bora afe, hasa pale anapokupiga kibuti kwa sababu amepata mwingine wewe hufai. No regret hapo he/she deserve
 
Mkuu umepiga vibuti vingapi na wewe umepiga vingapi! hebu wote hao wageuze marehemu. inakaaje hii




Mi huwa sipigi vibuti mzee, huwa tunatenganishwa tu na mazingira, ili siku tikikutana tena tuendelee.
 
Duh kuna watu kweli wanafikira za kiselfish sijaona mfano.

Yaani yaani unatafuta wepesi wa nafsi yako kiasi cha kujiuliza kama ni bora kwa mwenzi wako kufa kuliko kukuacha.

Huyu alokuwa mpenzi wako unaesema unampenda sana unaweza kumfikiria kufa kweli!

dada haya ni matokeo ya watu kugeuza mahusiano ya kimapenzi kuwa anasa badala ya upendo halisi. kweli haiiingii akilini kuwa umpendaye kwa dhati akuume zaidi anapokuacha (japo yu hai) kuliko anapokufa! kumbuka kuachwa ni tukio moja lakini kufa ni mawili ndani ya moja (two in one) yaani ni kuachwa na kufa. dada katerero na wengine naomba rejeeni habari ya mama wa kweli mwenye huruma na upendo wa kweli kwa mwanaye jinsi alivyokuwa tayari mwanaye achukuliwe na mwanamke mwingine (asiye mama yake) ili tu mtoto asiuawe! japo alikuwa mwanamke kahaba tu, lakini kwake ilikuwa heri mtoto wake abaki hai mikonon mwa mwanake asiye mama yake kuliko awe marehemu (afe) mikononi mwake! how wonderful is this love! Mungu ni mwaminifu, alitenda hukumu ya haki na hatimaye mfalme ajkajua hakika kuwa huyu ndiye mama halisi wa mtoto. habari hiyo inapatikana katika 1 wafalme 3:16-27, na nimeieleza hapa ili tuone thamani ya uhai wa mtu na tutafakatri maana halisi ya mapenzi, hahusiano na urafiki.
 
msiba msiba jamani inauma bora kuachana maana kunasiku mtakutana na kukumbushiana
 
Yaani umuombee mtu mliyependana afe kuliko kukupiga kibuti mhhhhhhh! Miye hili haliniingii akilini hata kidogo na hata siku moja siwezi kukaa chini na kuomba kitu potofu kama hiki.
 
Yaani umuombee mtu mliyependana afe kuliko kukupiga kibuti mhhhhhhh! Miye hili haliniingii akilini hata kidogo na hata siku moja siwezi kukaa chini na kuomba kitu potofu kama hiki.

Hivi kuna aliyeombea mpenzi wake afe? Naona watu wengi hapa wamekosea kulisoma swali/ kusoma kichwa cha mada!

Mimi nilivyoelewa ni kwamba matukio yote mawili, kupigwa kibuti na kufiwa na mpenzi wako yote yanauma. Mwanzisha mada anataka kupata maoni ya watu kuhusu maumivu yepi ni zaidi. Ni hivyo tu labda yeye mwanzisha mada aje aseme tofauti.
 
Aisee mtoa mada umechemka, hivi wawezaje kulinganisha kuachwa na kifo? Kifo is another thing jamaa yangu nijuavyo mm ht kama mtu umemchukia vipi linapokuja suala la kifo ni lazma km ww ni binadamu timamu utaingiwa na roho ya utu na kumsamehe! Mh mrudie mungu akupe nafsi ya kutofautisha kifo na vingne!
 
Humu JF hakuna ambaye hajafiwa Kwa vyovyote maumivu ya kifo hayana mfano! Mbona lipo wazi jamani maumivu kufiwa ni zaidi ya maumivu jamani!
 
Mi nikiwa naye huwa naomba yote hayo yasinitokee,ila ikitokea akanipiga kibuti ndio huwa naona bora afe tu,na wakati mwingine namuombea hata akutane na nyoka nikiwepo ili mimi nimsaidie nyoka amng`ate vizuri.

Aisee PM ww,ni kweli kibuti kinauma sana, lkn ikifikia hatua ya kuona ni bora afe kuliko kibuti alichokupa ni wazi kabisa humpendi na mawazo kama hayo yanaambatana na chuki, hasira,kinyongo na kisasi. Na kuna kitu nakiamini kuwa hata ikatokea nafasi ya kurejesha mahusiano hakutakuwa na msamaha wa kweli hapo. Mi nahisi ukiona mtu anakukosea halafu kashahuku kakumsamehe hakapo kabisa moyoni ujue huyo sio wako huyo.Ila kifo kinauma zaidi, hasa kwa mtu uliyempenda kwa dhati.
 
Hivi kuna aliyeombea mpenzi wake afe? Naona watu wengi hapa wamekosea kulisoma swali/ kusoma kichwa cha mada!

Mimi nilivyoelewa ni kwamba matukio yote mawili, kupigwa kibuti na kufiwa na mpenzi wako yote yanauma. Mwanzisha mada anataka kupata maoni ya watu kuhusu maumivu yepi ni zaidi. Ni hivyo tu labda yeye mwanzisha mada aje aseme tofauti.

ndo hivi nilimaanisha mkuu, wengi naona hawajaelewa, nataka kujua katika hayo matukio mawili, lipi linauma zaidi na kwa muda gani unaweza kumsahau huyo mpenzi,
 
Sijasema kwa kuwa ameniacha basi bora afe, ila nilitaka kujua tofauti ya maumivu yatokanayo na matukio yote hayo mawili, nadhani waliowahi kufiwa na kuachwa wangeweza kutuhabarisha zaidi,
 
Sijasema kwa kuwa ameniacha basi bora afe, ila nilitaka kujua tofauti ya maumivu yatokanayo na matukio yote hayo mawili, nadhani waliowahi kufiwa na kuachwa wangeweza kutuhabarisha zaidi,

maumivu ya kuachwa ni machungu endapo,endapo yule mtu ulimpenda na unahisi amekuacha kichakachuzi
 
dada haya ni matokeo ya watu kugeuza mahusiano ya kimapenzi kuwa anasa badala ya upendo halisi. kweli haiiingii akilini kuwa umpendaye kwa dhati akuume zaidi anapokuacha (japo yu hai) kuliko anapokufa! kumbuka kuachwa ni tukio moja lakini kufa ni mawili ndani ya moja (two in one) yaani ni kuachwa na kufa. dada katerero na wengine naomba rejeeni habari ya mama wa kweli mwenye huruma na upendo wa kweli kwa mwanaye jinsi alivyokuwa tayari mwanaye achukuliwe na mwanamke mwingine (asiye mama yake) ili tu mtoto asiuawe! japo alikuwa mwanamke kahaba tu, lakini kwake ilikuwa heri mtoto wake abaki hai mikonon mwa mwanake asiye mama yake kuliko awe marehemu (afe) mikononi mwake! how wonderful is this love! Mungu ni mwaminifu, alitenda hukumu ya haki na hatimaye mfalme ajkajua hakika kuwa huyu ndiye mama halisi wa mtoto. habari hiyo inapatikana katika 1 wafalme 3:16-27, na nimeieleza hapa ili tuone thamani ya uhai wa mtu na tutafakatri maana halisi ya mapenzi, hahusiano na urafiki.

Miss umeongea vyema, sasa tupe uzoefu wako ulivyoachwa na mpenzi uliempenda kwa dhati au ulipofiwa na mpenzi uliempenda kwa dhati, kipi kilikuuma sana, ulichukua mda gani kumsahau huyo mtu
 
Miss umeongea vyema, sasa tupe uzoefu wako ulivyoachwa na mpenzi uliempenda kwa dhati au ulipofiwa na mpenzi uliempenda kwa dhati, kipi kilikuuma sana, ulichukua mda gani kumsahau huyo mtu

sijawahi kufiwa, ila kipindi cha kubadilishabadilisha shule niliwahi kutengana na rafiki yangu mmoja, kwa kutoelewa kuwa yote yale yalitokana na kubadilibadili shule, yeye alishindwa kuvuta subira, nikasikia katembea na best wangu no. moja. nilijisikia vibaya lakini sio kuumia kivile. niliwaombea na nikaendelea na urafiki wa mawasiliano nao wote wawili huku nikiwaombea kwa Mungu awasamehe kwa kuwa ni vijana wadogo bado kama mimi na hawakujua wanatenda nini. leo ninavyoandika hapa wote wawili wmeishaniomba msamaha na urafiki unaendelea ila ndio hivyo tena fursa ya mapenzi kwa yule kijana ilikwishapotea, umegeuuka kuwa urafiki wa kawaida tu, kweli nikikutana naye huwa hana raha kabisa, ni kama namtesa sana kila ninapoongea naye kwa upendo kama zamani. na ninamwombea maisha marefu na mafaniio tele na anajua kuwa namuombea sana mema maishani mwake, na hilo linazidi kumtesa sana tena sana. hakika tutaushinda ubaya wa kila namna kwa wema pekee
 
Kifo kinauma asikwambie mtu jamani aahhh. Kuachwa kawaida tu mbona??? Usiombe afe hata kama mmepigana vibuti itakuuma kwa sana nikwambie
 
Back
Top Bottom