Hivi kwa Mamlaka ya Hali ya Hewa kuwataka Wakulima wapande mazao ya muda mfupi ndio imetosha?.

Hivi kwa Mamlaka ya Hali ya Hewa kuwataka Wakulima wapande mazao ya muda mfupi ndio imetosha?.

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Siku chache zilizopita nilikuwa safarini na nimeona maeneo mengi Wakulima wakiweka mbegu mashambani.

Ingawa sikuweza kujua aina ya mbegu wanazopanda lakini kwa mazoea tuliyonayo wengi wao watakuwa wanapanda mahindi au Maharage.

Ni jambo la kutia moyo kutokana na kusuasua kwa mvua za msimu lakini najiuliza kama wana taarifa sahihi kutoka kwa Mamlaka za hali ya hewa.

Hivi kwa nini Watu wa TMA na Wizara ya Kilimo wasijitokeze wakiwa pamoja na kutoa ushauri wao badala ya kuacha TMA kuongea tu kama kutimiza wajibu na kisha wanakaa pembeni na kuacha mambo yaende yatakavyokuwa?.

Hawa Wakulima wanapanda sasa hivi na tunawaangalia tu alafu wakikosa mavuno tutasema tuliwaambia hamkusikia...ni nani wa kufuatilia kujua kama wana taarifa za TMA na ni nani wa kushauri ni zao gani wapande?.

Au waachwe tu wacheze kamari, wakipata wapate wakikosa wakose?.
 
Kazi lawama tu,unatakiwa kufuatilia habari Kama raia timamu,ukiwa mkulima unatakiwa kufuatilia tma hasa karibu na msimu,unataka wapite nyumba kwa mnyumba!!?
 
Tuwaache tu wabet hata ukwambia hawakuelewi, Pindi wakishukiwa na kitu kizito ndio wataelewa
 
MKUU SHAURI WEWE KAMA MTAALAMU BASI
Mimi sio Mtaalamu ila ninachotaka ni hao TMA waliotahadharisha kuwa Wakulima wapande Mazao yanayokomaa kwa muda mfupi wasidhani jukumu lao limeisha wakajifungie maofisini.

Wao sasa washikamane na Wizara ya kilimo kuhakikisha Wakulima wanafanya hivyo walivyoshauri.
 
Mimi sio Mtaalamu ila ninachotaka ni hao TMA waliotahadharisha kuwa Wakulima wapande Mazao yanayokomaa kwa muda mfupi wasidhani jukumu lao limeisha wakajifungie maofisini.

Wao sasa washikamane na Wizara ya kilimo kuhakikisha Wakulima wanafanya hivyo walivyoshauri.
GOOD IDEA
 
Tuwaache tu wabet hata ukwambia hawakuelewi, Pindi wakishukiwa na kitu kizito ndio wataelewa
Sidhani kama watafikiwa na Maafisa kilimo na kuelekezwa bado watakaidi.

Hofu yangu ni kuwa wengi wanaendesha mambo kimazoea tu.
 
Kazi lawama tu,unatakiwa kufuatilia habari Kama raia timamu,ukiwa mkulima unatakiwa kufuatilia tma hasa karibu na msimu,unataka wapite nyumba kwa mnyumba!!?
Wewe kwa maoni yako TMA wamefanya vya kutosha kutoa taarifa?.

Huo ni wajibu wao na si hisani, wanalipwa kwa kodi zetu kutoka hao hao Wakulima.

Ni suala la kutimiza tu wajibu kwa mambo ya msingi kuliko kukaa tu pembeni na kuangalia.
 
Sidhani kama watafikiwa na Maafisa kilimo na kuelekezwa bado watakaidi.

Hofu yangu ni kuwa wengi wanaendesha mambo kimazoea tu.
We hawa watu saa ingine ni pasua kichwa unawapa ushauri kwa ajili ya maendeleo ya binafsi lakin wapi
Mfano mzuri angalia wale wazee wa handeni wanafanyiwa mambo kwajili ya maendeleo yao lakini wenyewe hawataki akili zao zimeganda me nahic the same na hawa hata ukiwapa preucation japo kuna wengine wataelewa ila wengi wa watanzania especially vijijini bado hawajapata elimu ya kutosha but now days naona kuna vikundi mbalimbali vinatoa elimu kuhusu kilimo na ufugaji wa kisasa kama wakijikita zaidi na wakifikia lengo tuwaweza kuondokana na hivi vitu kwa kuwa watu wengi wamepata elimu katika jamii yetu
Thanks
 
We hawa watu saa ingine ni pasua kichwa unawapa ushauri kwa ajili ya maendeleo ya binafsi lakin wapi
Mfano mzuri angalia wale wazee wa handeni wanafanyiwa mambo kwajili ya maendeleo yao lakini wenyewe hawataki akili zao zimeganda me nahic the same na hawa hata ukiwapa preucation japo kuna wengine wataelewa ila wengi wa watanzania especially vijijini bado hawajapata elimu ya kutosha but now days naona kuna vikundi mbalimbali vinatoa elimu kuhusu kilimo na ufugaji wa kisasa kama wakijikita zaidi na wakifikia lengo tuwaweza kuondokana na hivi vitu kwa kuwa watu wengi wamepata elimu katika jamii yetu
Thanks
Hakika inasikitisha.
 
Kuna eneo nilikuta kama Wanafamilia, yaani Baba, Mama na Watoto wanatoka au ndio walikuwa wanaenda shambani na Majembe yao.

Sasa ukifikiria kama hizo juhudi zao zinaweza kuwa sawa na kukinga maji na Gunia kwa sababu ya kukosa tu taarifa muhimu.

Na inasemwa "information is power".
 
Wewe kwa maoni yako TMA wamefanya vya kutosha kutoa taarifa?.

Huo ni wajibu wao na si hisani, wanalipwa kwa kodi zetu kutoka hao hao Wakulima.

Ni suala la kutimiza tu wajibu kwa mambo ya msingi kuliko kukaa tu pembeni na kuangalia.
Mimi mkulima,ukifika oktoba nasubiri kwa hamu kujua mvua zitakuaje,najua msimu huu mvua ni chini ya wastani,maana yake kidogo,kwa Kanda ya Kati na magharibi
 
Mimi mkulima,ukifika oktoba nasubiri kwa hamu kujua mvua zitakuaje,najua msimu huu mvua ni chini ya wastani,maana yake kidogo,kwa Kanda ya Kati na magharibi
Na ndio hoja yangu hapa, kwamba tusikae pembeni kwaangalia tu Wakulima wakijitutumua kwa kuandaa mashamba na kupanda mazao ambayo hawataenda kuyavuna.

Wizara ya Kilimo kupitia Mabwana shamba waungane na TMA wawasaidie hawa Wakulima...kama ni kupanda basi waambiwe ni mazao gani wapande.

Ila kama tunawaacha tu wafanye kwa mazoea ili mradi TMA walishasema mvua zitakuwa chini ya wastani sidhani kama ni kuwatendea haki...ni kama tunawachora.
 
Na ndio hoja yangu hapa, kwamba tusikae pembeni kwaangalia tu Wakulima wakijitutumua kwa kuandaa mashamba na kupanda mazao ambayo hawataenda kuyavuna.

Wizara ya Kilimo kupitia Mabwana shamba waungane na TMA wawasaidie hawa Wakulima...kama ni kupanda basi waambiwe ni mazao gani wapande.

Ila kama tunawaacha tu wafanye kwa mazoea ili mradi TMA walishasema mvua zitakuwa chini ya wastani sidhani kama ni kuwatendea haki...ni kama tunawachora.
Tma hutoa taarifa ya jumla oktoba,Kuna maafisa ugani ngazi zote za utawala,wakulima huwa hawashauriki,wanafanya kwa mazowea
 
Siku chache zilizopita nilikuwa safarini na nimeona maeneo mengi Wakulima wakiweka mbegu mashambani.

Ingawa sikuweza kujua aina ya mbegu wanazopanda lakini kwa mazoea tuliyonayo wengi wao watakuwa wanapanda mahindi au Maharage.

Ni jambo la kutia moyo kutokana na kusuasua kwa mvua za msimu lakini najiuliza kama wana taarifa sahihi kutoka kwa Mamlaka za hali ya hewa.

Hivi kwa nini Watu wa TMA na Wizara ya Kilimo wasijitokeze wakiwa pamoja na kutoa ushauri wao badala ya kuacha TMA kuongea tu kama kutimiza wajibu na kisha wanakaa pembeni na kuacha mambo yaende yatakavyokuwa?.

Hawa Wakulima wanapanda sasa hivi na tunawaangalia tu alafu wakikosa mavuno tutasema tuliwaambia hamkusikia...ni nani wa kufuatilia kujua kama wana taarifa za TMA na ni nani wa kushauri ni zao gani wapande?.

Au waachwe tu wacheze kamari, wakipata wapate wakikosa wakose?.
Ulitaka wasemeje?
 
Back
Top Bottom