Hivi kwanini ajira za lecturers zinakua readvertised sana?

Hivi kwanini ajira za lecturers zinakua readvertised sana?

El marabiosh

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2019
Posts
2,382
Reaction score
4,978
Ni kwanini hizi ajira zinarudiwa kutangazwa inamaana watu wanaacha kazi au watu hawaapply?
 
Hao hao ma academicians huwa wanazibana gpa ,mfano mzuri Ni udsm Kuna vijana wazuri mno wanaenda pale Ila wanabania wanaishia kupata gpa ya kawaida mno.

Lengo kuwa wao soko lap libakie juu kabisa. Jiulize eti lecturer anasafiri from dar to dodoma or iringa kufundisha.
Inatakiwa hii mitihani iwe inatungwa na kusahishwa na bodi husika ama jopo liundwe Ila huyu huyu mtu mmoja anaweza akawa ana fitina na mtu ama binti akamkataa Basi anamkomoa tu.

Yaani wanatumia madaraka yao kuwanyanyasa
 
Kuna kitu hakiko sawa nahisi sijui kama wakuu mmeona hicho kitu unajua nimekuwa nikijiuliza sana why hizi academician Positions zimekuwa readvertsised mara nyingi ikabidi nijaribu kudadisi na hili ndio jibu langu japo mnaweza kosoa kama sitakuwa sahihi

Tuanze kuangaza zamani vyuo vilipataje Wakufunzi tuchukulia case study iwe UDSM!! Hapohapo tukumbuke hakuna chuo wala kozi ya kusomea ili uwe mkufunzi!

Zamani wale waliokuwa wanafanya vizuri hasa kwa undergraduate Degree chuo kiliwabakiza wanakuwa Tutorial assistant katika idara yenye uhitaji au alipofanya vizuri anawekwa katika hiyo idara anatafutiwa scholarship kwa urahisi tu anasomeshwa Masters hadi PhD katika vyuo bora kabisa ulimwenguni ukisoma ile Prospectus ya chuo utaona huyu sijui kapta PhD Oxford, huyu, Njimegen yule Alberta huyu sijui Cape town huyu Kwazulu natal yule sijui Calgarly univeristy na seneti ya chuo ndio ilikuwa na mandate ya kuajiri sasa leo

Hii ajira zote zinapitia Utumishi Dadeki kazi ipo hapo!? Hivi kwa ulimwengu wasasa nani asome hadi PhD katika Programmes ambazo hata kupata ajira ni kipengele tu Yaan mtu asome Fine and Performing art sijui libarary studies , Sijui Developments studies Yaan alenge kuwa mkufunzi nani huyo!??

Mfumo wa Utumishi ni mzuri kwa kazi za kawaida tu ila academician naomba wawaachie tu vyuo wenyewe waandae wakufunzi wao!!

Kuna watu nawafamu wamemaliza pale UDSM na GPA 4.4 za MBB sujui Microbiology wapo tu kutaa wanauza asali toka kaliua Tabora wanaleta DODOMA hapa!!

Ukichunguza kwa umakini snaa utagundua zile Programmes zisizo na future na zisipendwa nyingi ndio zinaongoza kuwa READVERTISE sana wakuu

MWISHO
 
Ph.D kuipata ni kasheshe. Ni mara chache sana mwenye Ph.D kuwepo mtaani hana kazi.
 
Back
Top Bottom