Hivi kwanini baadhi ya Watanzania wanataka Diamond aanguke?

Hivi kwanini baadhi ya Watanzania wanataka Diamond aanguke?

Si wana wivu Tu.......na wengi wao Ni maskini yani choka Ile mbaya...
 
Kwanini mnalazimisha watu wampende mond wakati mnasema anafanya vizuri???

Kwanini hamhamasishi wengine kupendwa na watanzania ili wakuiwakilisha Tanzania wawe wengi????

Tatizo lenu nyie mnadhani kumsupport mtu mwingine tofauti na mond ni kumchukia.

Na mnadhani kumpenda mond ni kuwachukia wengine wanaojikongoja ili kufikia level za mond.

Acheni mambo yenu bwana.

Kama ni support, tutoe hamasa kwa wasanii wote wa nchi yetu. Kama wafanyavyo wanigeria.

Isije kuwa kama bongo movie. Watu walimsuport kanumba wakawasahau wengine. Alipokufa, akafa na tasnia nzima.

Tubadilikeni kwanza sisi tunaompenda mond kwamba, kumsupport yeye sio kuwachukia wengine
 
wa tanzania wana tabia moja ukiwa na mafanikio unghali umetoka maisha magum lazime wa chukie tuu ndo wa furah au waku shushe i mean ufilisike
hapo hapo ukifa kila mtu atakusifu kwa uliyo tenda
TANZANIA UKITAKA USIFIWE NA KILA MTU KUFA LEO
 
Kwani Diamond akifilisika hela zake ndio zitaenda kwao? [HASHTAG]#Halleluya[/HASHTAG]
 
Mwataka apendwe na kila MTU?

Amekuwa nani?

Mungu mwenye hajawahi kuonekana na anachukiwa sembuse yeye?

Naona ni kawaida tu wanomkosoa wakaze buti na wanaomsapoti wakaze buti, haya ndo maisha

Msilazimishe kila MTU amsifie,

Hata wewe ktk familia yako na majiran si wte wanokusema vizuri,

Hivyo mashabiki zake na yy mwenyewe akubaliane na hali ilivyo
 
Ni roho mbaya tu zinasumbua watu,,na pia wivu wa maendeleo..
 
Adui yako muombee njaa mkuu....na yeye apunguze NYODO..... PIA akumbuke TEMBO HUPONZWA NA MENO YAKE...watu wanamchukia sababu ya alivyonavyo.....hakuna kingine
 
Diamond nae matusi mengi mara vinuka mikojo..kasaau alikotoka huyu mpuuzi..
 
Kiba hana Mashabiki bali ana watu ambao wanamchukia Mondi na sababu kuu tulizoea wasanii wetu ku hit kwa mda fulani na kupotea na kwenda kimataifa tukatambulisha mziki wetu ilikua kama ndoto sasa dogo kaweza ndio tatizo linaanza hapo. Wabongo tunapendwa kunyenyekewa yaani media na mameneja uwahusudu sasa Mondi kabadilisha hili kutoka kwa ma meneja njaa mpaka kuwaajiri yeye kitu ambacho kama kilikuwepo basi hakikua kwa kiwango cha Mondi na kuikuza brand yake mpaka imefika hatua hategemei sana Media kutambulisha kazi zake.

Sasa wa bongo tunapenda tu unafiq na kuonana tukiwa masikini hao kina Kiba kwenye game kitambo wameifanyia nini nchi yetu? Dogo kaweza na atafika mbali tumuunge mkono anaweza.
(samahani kwa povu langu nimeamka nazo)[emoji4] [emoji4] [emoji4]
Kwa nini unamchukia Alikiba? Kwa kifupi Diamond na Alikiba wanachukiwa sana hilo halina ubishi kama mfano ulioutoa hapo yaani hvyo kwa watanzania hii kitu hauiepukiki kamwe na kuwabadilisha watanzania hii kitu haitakuja kutokea
 
Diamond Platnumz ni mwanadamu ana madhaifu yake kama alivyo binadamu yeyote yule. Lakini katika picha kubwa na kimuziki huyu ndugu yetu anaiwakilisha nchi vyema sana huko nje.

Nadhani hili ndilo la Msingi na tungebaki kuliangalia wote kama Watanzania. Kuwa na timu siyo makosa hata Yanga na Simba ni Wapinzani wakubwa lakini tukija kwenye Taifa Stars hizo timu tunazivua na tunavaa Utaifa. (Huu ndiyo Uzalendo jamani)

Utaifa ukiisha tunarudi kwenye timu zetu na kuanza kung'oa viti pale uwanja wa taifa. Hivyo basi kwenye kujenga sifa za wasanii wetu awe Ali Kiba, Diamond au Vanessa Mdee tushindane humu ndani lakini tusifanye chuki kiasi cha kutaka kuchafua sia zao. Hao ni watoto wetu kabisa,watoto wa nchi hii: Hakuna mzazi anayetup watoto jamani.

Tumtie moyo Alikiba na tumtie Moyo Diamond: Pia tuwakosoe pale wanapofanya vibaya hali tukiwa na dhamira safi kabiaa ya kutaka kuwajenga kimuziki. Tuepukane na fitna,majungu na uzandiki l: haya mambo hayajengi kabisa.
Watanzania wengi wamekata tamaa ya maisha yao na mond katoboa life ya kibongo,asili ya watu waliokwama ni kuwaombea mabaya waliofanikiwa ni WIVU WA KIJINGA sana.
Wengi wanaomponda jamaa na kumuombea mabaya hawana wanachomiliki zaidi ya simu na tv.
 
Hali imekuwa mbaya sana, niliona Mange kaanzisha kampeni ya kuhamasisha watu wairipoti nyimbo mpya Daimond youtube ifungiwe kwasababu eti ananunua viewers.
 
Badhi ya watanzania ao unaongelea timu kiba na timu wema ?? We nikilaza mwengine ... dai kapandishwa na watanzania japo kaweka bidi yake piaa.
 
Back
Top Bottom