Hivi kwanini matajiri wakubwa hapa Tanzania ni wahindi na waarabu tu?

Hivi kwanini matajiri wakubwa hapa Tanzania ni wahindi na waarabu tu?

Wamekulia mazingira ya Biashara, Wameanza kushiriki kwenye biashara za familia wakiwa wadogo Sana, Wana nidhamu ya Pesa...wanajua kuiongeza maradufu zaidi!! Sio kwamba sisi wabongo hatuwezi ila Wa-Bongo hawapendani,hawaaminiani...Ukiwaachia watoto wa kibongo mali na biashara kubwa ndani ya miaka mitano watakuwa washafilisika!
Wa - Africa wanaabudu wasichokijua, sometimes wanaweza wakawa wanaabudu kinyume. bila kujua, MUNGU mleta mali ni yupi.
 
Kwangu umasikini naweza itafsiri kama ile hali ya kuwa muhitaj, utajiri ni ile hali ya kujitosheleza au kutosheka.
Hivyo ukiwa na pesa alafu ukawa bahiri ndugu yangu wewe ni masikini.
 
Mimi ilikuwa kila nkienda k.koo na temeke nlikuwa nawaona muha kibao na mazaga yao....swali nkajiuliza "mitaji wanatoa waapi?"

Siku nikamkalisha muha mmoja nnayemkopaga vitu....nkampa sound mpk akasema ukweli.

Kuna matajiri wa kihindi kule k.koo wao mishe zao ni kutoa mikopo kwa vijana hao kisha unarudisha pesa kidogkidogo kwa riba.

Wahindi wanajua kuiheshim pesa...!!yan hawataki utan kbsaa....na pia sio watu wa stareh saaana...!!kingine ht mahitaji huchukua jumla...na pia zaidi wanainuana wao kwa wao sio km sisi unga robo tunarogana kila siku

Wabongo nasi km tukiheshim pesa...tukaacha matumiz yakijinga mbna tutatoboa tuu
 
Unayojifunza kwao unayafanyia kazi?
Nimeipenda sana hii thread na nikupongeze kwa kufikiria hili mkuu labda niseme ili atakaebahatika aone na ajifunze.

Nimebahatika kukaa karibu na Wahindi mwaka wa tatu sasa kwasababu Shemeji yng aliemuoa dadangu ni Muhindi kwahiyo nimepata kujifunza mengi sana kwa kuwa nipo karibu nao kiukweli hawa watu ni wajanja sana kupita kiasi lakini pia wana malengo sana kwenye biashara tena ya muda mrefu na pia wana nidhamu ya pesa sana nimegundua hakuna watu wabahili kama wahindi tena ni matajiri lkn cha kushangaza ni Wabahili kupita kiasi yaani hawanunui kitu mpaka wakihitaji sana na kama ukimuona Muhindi anaenjoy ujue kashawekeza sana na ana uhakika hatoanguka kibiashara.

Na si kila siku anaenjoy unaweza kukuta ni mara moja kwa mwaka then hawa watu unaowaona leo ni matajiri ujue wamerithi kutoka kwa babu zao walikuja kutoka India hawana kitu walianza biashara ndogondogo then ikawa inakua wakazaa watoto wakawakuta baba zao wameikuza biashara then watoto wataoa then watazaa watoto hao wajukuu watakuta ile biashara imekua kubwa sana imagine tangu ile biashara ianzishwe ni miaka 60 yaani Babu alianzisha mjukuu anaikuta biashara kubwa kwahiyo hapati tabu kuiendeleza.

Unajua ndugu wana JF ugumu ni kuanza kuikuza biashara lakini ikifika hatua fulani ni rahisi sana kutengeneza mamilioni ya Fedha kwa mfano-: Ulianza biashara na milioni 5 baada ya miaka 10 una mtaji wa milioni 200 je kufikisha mtaji milioni 1000 ni ngumu jibu sio ngumu.Kitu kingine nilichokiona hawa watu wanasaidiana sana nimeshuhudia baadhi ya wahindi wanatoka India wanakuja kwa Wahindi wenzao ambao ni matajiri wanawaajiri wanawalipa mshahara mara 10 ya waajiriwa wengine hata kama hawana elimu.Na wanawafundisha watoto wao jinsi ya Kuhandle biashara ili isife lkn Leo utamkuta Mwafrica akifungua biashara tu akaanza kuingiza pesa basi starehe nyingi wanawake anabadilisha kama nguo anadharau ndugu zake matokeo yake biashara inamshinda.

Ndugu wana JF mtu yeyote ambae ni mfanyabiashara tajiri amepitia changamoto nyingi sana lkn hawakukata tamaa na biashara ni somo pana sana.Halafu kitu kingine nilichokiona kwa hawa watu ni Kuishi pamoja babuna bibi watoto wao na wake zao na wajukuu zao wote wanakaa nyumba moja hii pia ni Siri ya mafanikio yao kwanza inapunguza gharama za maisha pili inaleta baraka ndani ya nyumba na hata chakula wanapika pamoja na wanakula meza moja wote wao na wake zao na baba zao na mama zao hata na wajukuu zao ila mabinti wakiolewa huwa wanaondoka kwenda kwa mume.Nimechoka kuandika lkn nina mengi niliyojifunza kupitia hawa watu na naendelea kujifunza kila kukicha kupitia hawa watu coz nipo karibu nao
 
Hivi kwanini washamba wengi hapa Tanzania ni wasukuma tu[emoji41]

Umaarufu unachangia, nina uhakika ukikaa utaje makabila kati ya 120+ ukijitahidi sana utataja 30... na utaanza na wasukuma kabla hata ya kabila lako!
 
Nimeipenda sana hii thread na nikupongeze kwa kufikiria hili mkuu labda niseme ili atakaebahatika aone na ajifunze.

Nimebahatika kukaa karibu na Wahindi mwaka wa tatu sasa kwasababu Shemeji yng aliemuoa dadangu ni Muhindi kwahiyo nimepata kujifunza mengi sana kwa kuwa nipo karibu nao kiukweli hawa watu ni wajanja sana kupita kiasi lakini pia wana malengo sana kwenye biashara tena ya muda mrefu na pia wana nidhamu ya pesa sana nimegundua hakuna watu wabahili kama wahindi tena ni matajiri lkn cha kushangaza ni Wabahili kupita kiasi yaani hawanunui kitu mpaka wakihitaji sana na kama ukimuona Muhindi anaenjoy ujue kashawekeza sana na ana uhakika hatoanguka kibiashara.

Na si kila siku anaenjoy unaweza kukuta ni mara moja kwa mwaka then hawa watu unaowaona leo ni matajiri ujue wamerithi kutoka kwa babu zao walikuja kutoka India hawana kitu walianza biashara ndogondogo then ikawa inakua wakazaa watoto wakawakuta baba zao wameikuza biashara then watoto wataoa then watazaa watoto hao wajukuu watakuta ile biashara imekua kubwa sana imagine tangu ile biashara ianzishwe ni miaka 60 yaani Babu alianzisha mjukuu anaikuta biashara kubwa kwahiyo hapati tabu kuiendeleza.

Unajua ndugu wana JF ugumu ni kuanza kuikuza biashara lakini ikifika hatua fulani ni rahisi sana kutengeneza mamilioni ya Fedha kwa mfano-: Ulianza biashara na milioni 5 baada ya miaka 10 una mtaji wa milioni 200 je kufikisha mtaji milioni 1000 ni ngumu jibu sio ngumu.Kitu kingine nilichokiona hawa watu wanasaidiana sana nimeshuhudia baadhi ya wahindi wanatoka India wanakuja kwa Wahindi wenzao ambao ni matajiri wanawaajiri wanawalipa mshahara mara 10 ya waajiriwa wengine hata kama hawana elimu.Na wanawafundisha watoto wao jinsi ya Kuhandle biashara ili isife lkn Leo utamkuta Mwafrica akifungua biashara tu akaanza kuingiza pesa basi starehe nyingi wanawake anabadilisha kama nguo anadharau ndugu zake matokeo yake biashara inamshinda.

Ndugu wana JF mtu yeyote ambae ni mfanyabiashara tajiri amepitia changamoto nyingi sana lkn hawakukata tamaa na biashara ni somo pana sana.Halafu kitu kingine nilichokiona kwa hawa watu ni Kuishi pamoja babuna bibi watoto wao na wake zao na wajukuu zao wote wanakaa nyumba moja hii pia ni Siri ya mafanikio yao kwanza inapunguza gharama za maisha pili inaleta baraka ndani ya nyumba na hata chakula wanapika pamoja na wanakula meza moja wote wao na wake zao na baba zao na mama zao hata na wajukuu zao ila mabinti wakiolewa huwa wanaondoka kwenda kwa mume.Nimechoka kuandika lkn nina mengi niliyojifunza kupitia hawa watu na naendelea kujifunza kila kukicha kupitia hawa watu coz nipo karibu nao
Mkuu safi sana nimejifunza kitu mara nyingi ukichukulia jambo kwa mtazamo hasi hata matokeo huwa hasi.
Tusijiulize kwanini wenzetu wanafanikiwa labda ni wezi ama nini ila tujifunze kwa mazuri kama uliyoainisha Mkuu,
Hili jambo la kuishi na familia zao(Babu,Bibi, Baba, Mama) kwa Amani limenifurahisha Zaidi kwani ndio mwanzo wa kupata baraka na kuinuana kama familia.
 
Biashara za waafrika walio wengi hazisomeki. Pesa wanazungusha kwenye biashara in cash zikizidi wanachimbia chini, records hawaweki, biashara hawaweki kwenye mitandao, wapo simple hawataki kujionyesha, wanaishi kama middle class lakini wako worth billions. Akishtukizia anaenda dukani ananunua VX ya 300m cash. Wapo wengi sana Tanzania. Forbes hawawezi kuwafaamu. Subiria watoto wao wakiridhi hizo Mali uone mlipuko wa mabilionea waafrika kwenye Forbes sababu hawa wengi watatamba sana nakujionyesha alafu watafilisika
Hii ni kweli aseee pure truth 🤗
 
Back
Top Bottom