Hivi kwanini wali wa mkaa ni mtamu kuliko ule wa 'rice cooker'?

Hivi kwanini wali wa mkaa ni mtamu kuliko ule wa 'rice cooker'?

Hahahaa uwiiiiii,hii ndo raha ya jamiiforum
MATANDU.

Muda wa kupakuliwa Chakula, ni raha pale yanapoanza kuondolewa MATANDU.

Hiyo kama upo karibu na Mpishi lazima uombe kuonja MATANDU.

Kama ni Mpishi mwenye gubu, anakutimua, "toka,"mtoto wa KIUME unaleta HILA jikoni" "toka".

MATANDU yakimwagiwa MCHUZI, au MAHARAGE na ROJO yake, acha tu.

Jamani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bahati mbaya sijawah kula wali wa mkaa au wa rice cooker....nimekula wa mchele tu.

The good, the bad and the ugly.
 
Kwanza WALI MWENZIO ni NAZI,,na sio mafuta,,, wali wa NAZI NI BALAA,,,halafu JUU lazima uwe na MATANDU. ,AU MAHABA (watu wa tanga tunaita hivyo)na lazima uwekewe mkaa juu ya sufuria au chungu.,,HALAFU unapata na SAMAKI WA CHUKUCHUKU,,,hatari MKUU ,,,haya mambo ya GESI,,MAJIKO YA UMEME,,,huwezipata LADHA HALISI YA WALI,,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nami pia ndo nachokiona hiko.
Lakini kwa karne hii matumizi ya kuni nia adhabu sana kuzipata hizo kuni na pia ile harufu ya Moshi ukijumlisha na macho kutoa machozi mhhhh.

Last Christmas nilipika biriani kwenye kuni.
Haloooo moto wa kuni nao ni mkali tu kama gas ila niliipata pata.
Lakini biriani ilitoka poa sana.
Naona kama Chungu mwenzie Kuni.
 
Kisamvu nakielewa sana.
Kwanza nikikichemsha naweka saum na kitunguu kiiiva naweka ile top layer ya maziwa fresh.
Kinalala.
Kesho yake naweka nazi na siagi ya karanga.
Kinaliwa ila ni lazima kibaki tena [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
Keshokutwa kinapashwa na siagi ya karanga.
Maharage yaliyolala, pembeni kisamvu na dagaa mchele au samaki wa kukaanga na fresh wali(si kiporo)
+ kisamvu kilicholala

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kisamvu nakielewa sana.
Kwanza nikikichemsha naweka saum na kitunguu kiiiva naweka ile top layer ya maziwa fresh.
Kinalala.
Kesho yake naweka nazi na siagi ya karanga.
Kinaliwa ila ni lazima kibaki tena [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
Keshokutwa kinapashwa na siagi ya karanga.
Maharage yaliyolala, pembeni kisamvu na dagaa mchele au samaki wa kukaanga na fresh wali(si kiporo)
Kumbe humo... utakua kibonge sana wewe 😂😂😂
 
Back
Top Bottom