Hivi kwenye engine ya gari ule mlio hutoka wapi?

injini za zamani mfumo wa cabulater mchanganyiko wa hewa na mafuta kwa pamoja vinagandamizwa ndani combustion chamber kisha ignition plag inachoma na mlipuko unatokea,
Sasa kwa injini za kisasa za petroli kuna injetion fuel plag na kuna ignition spark plag,

Swali:nataka kufahamu ni muda gani mafuta yanatolewa na injection fuel plag ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah swali lako ni gumu mzee. But kilichobadilika kutoka kwenye carburator kuja kwenye Electronic fuel injection. Ni namna tu ambavyo hewa na mafuta vinachanganyika.

Hizi fuel injectors zinafungwa kwenye intake manfold. Na mafuta yatatolewa na injector kama tu yatakuwa yanahitajika kwenye cylinder husika. Nje ya hapo mafuta hayatatoka...

Kwa hiyo kwa sasa mafuta yatakayotolewa na fuel injectors ni yale tu yatakayohitajika. Tofauti na zamani ambapo mafuta yalikuwa yanaenda tu.




Sent using Jamii Forums mobile app
 
HIzo sauti kama wengi walivyosema inatokana na milipuko ndani ya engine kwakua inatokea mingi ndani ya muda mfupi ndo maana unapata sauti iliyonyooka,. Kama hauelewi jaribu kudisconnect plug moja wapo, utagundua sauti inabadilika kidogo na unaweza kuhisi kuna mlipuko ambao kama umemiss.
Hebu pia pitia link hii ya youtube:

utaona sauti ya milipuko kwenye slow motion inavyokua
 

Fiziksi rahisi ni kwamba "energy"(Kiswahili sasa sijui ni nguvu??sio Power) .....energy haiwezi kutengenezwa wala kuharibiwa ila huwa inabadilishwa "form" mfumo

Hivyo basi energy iliyo kwenye mafuta yanapofanya "combustion" kwa lengo la kupata nguvu ya kuendesha gari pia ndo mabaki yake hubadilshwa kuwa sauti/mungurumo na pia joto(injini inapata moto) na saa nyingine hata mwanga hutokea(cheche kwenye eksozi)
 
nimekupata kaka,kwamba ni mafuta yanayohitajika tu,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli Isee. Hasa ule mlio wa Leyland DAF, una kasauti fulani ka kike kazuri kweliii. Sasa gapo sijui makelele yanakuwa yako wapi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…