Ni hoja nzuri sana.. isipokuwa ni vigumu kutekelezeka katika nchi ambayo sera za viwanda haziko tayari kuhakikisha hilo linatokea.. sera za viwanda utadhani zinatungwa na wakoloni huko kusikojulikana halafu zinaletwa hapa nchini ili zitekelezwe..
Matokeo yake ni kwamba tija ya bidhaa zinatengenezwa hapa inakuwa kidogo, na zenyewe kuwa za gharama sana, kuliko hata zinazotoka nje.
Tatizo la kwanza ni kodi ya mitambo ya kutengeneza bidhaa.. utapigwa 200%.
Kodi kwenye mali ghafi.. 200%
Saa nyingine unakuta utengenezaji wa baadhi ya bidhaa unahitaji expertise kutoka nje, work permit ndo utachoka zaidi.
Ukishaanza kutengeneza hizo bidhaa tu, watakotokea kina TRA, BRELA, TFDA, OSHA, NEMC, WCF, ndo hutajuwa.
Lingine kubwa ni upatikanaji wa mitaji. Mabenk ya ndani hayana mpango nadhani na uwezo wa kimkakati kuwezesha uwekezaji katika manufacturing. Sirikali ndo kwanza haitaki kusikia mambo ya guarantee... Mabenk ya nje lakini yenye matawi hapa nchini yako kwa ajili ya kuwawezesha wawekezaji kutoka nchi mama waweze kuvuna hapa nchini. Watu ni wachache wenye access na mitaji kutoka kwenye mabenk ya nje moja kwa moja
Kupata capital kutoka ndani ni virtually impossible. Nguvu ya kufanya manunuzi ya watz (purchasing power) walio wengi bado ni ndogo sana.. ndogo kupindukia. Katika uchumi ambao per capita gdp haifiki dollar 200, ujuwe ni useless kufikiria manufacturing katika uchumi kama huu.
Unakuta katika uchumi kama huu, 75-90% ya kipato cha mtu kinaishia katika bidhaa zinaohusiana na vyakula.. hakuna balance ya kununuwa bidhaa zingine.
Kwa ufupi ni kwamba kwa changamoto nilizozitaja, kupatikana kwa bidhaa zinazotengenezwa hapa nchini ni mgumu na. Bado tutaendelea kununua bidhaa zilizotengenezwa na wanaume wenzetu