Hivi maana ya neno 'Wabongo' ni nini

MK254

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2013
Posts
32,408
Reaction score
50,809
Mara nyingi huwa naona Watanzania wakijisifia kuitwa 'Wabongo', sasa juzi nimetazama video ya rais Magufuli akizungumza kuhusu matapeli yaliyopiga hela ya maji Tunduma, akasema alifikiria Wabongo wapo Dar es Salaam tu, kumbe na Tunduma wapo, kwa hivyo ina maana hilo jina linahusiana na ukajanja na utapeli tapeli....
 
Unajichanganya weye!Mara Wabongo,mara wa Deeeseem,mara Tunduma.Wote hao ni Wabongo wanaotumia mmbongo.
 
Ishu ni kuwa zamani ilikuwa inamaanisha kuishi dar kunahitaji kutumia ubongo, ndo maana pakaitwa bongo dar-es-salaam. Ila baada ya kuzoeleka sana ikawa inamaanisha watz kwa ujumla, Hivyo ukijiita mbongo unamaanisha mtu unaetumia akili ku-survive kwa namna yoyote ile ikiwemo ujanja, utapeli, to name a few

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Hehehe!! Umeiweka sawa...
 

Ahaaa haaa haaa
Kumbe mnaifuatilia bongo?
 
wah!!bongo lala haswa..yani wako usingizini mpka sasa...
 
Watu wanao ishi kwa kutumia akili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wabongo ni tafsiri ya watu wanaotumia akili siku zote.

Kamwe usije relax ukiwa na mtz kama mnavyofanya nyinyi wakenya. Si unaona mna hustle, halafu wabongo wanasogeza kete tu maisha yanasonga!!!
 
Kipindi cha Nyerere kulikuwa na viwanda vingi ukilinganisha na idadi ya watu, kila mkoa ulikuwa umejitosheleza. Baada ya uchumi wa kijamaa kuanza kuporomoka, watu wakaanza kukimbilia Dar es salaam ambako maisha yalikuwa tofauti na mikoani. Hii ikafanya watu kutumia akili zaidi (ubongo) kuishi Dar es salaam.

Kwa hiyo Dar ikajulikana kama nchi ya Bongo lakini baada ya muda ikaonekana nchi yote maisha yanazidi kuwa magumu hivyo ubongo mwingi ulihitajika kufikiri na ndivyo nchi yote ikapata hilo jina.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…