Hivi Madaktari wetu huwa wanashindwa kutafsiri matokeo ya vipimo?

Hivi Madaktari wetu huwa wanashindwa kutafsiri matokeo ya vipimo?

Nafaka

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
12,154
Reaction score
31,246
Nimekuwa nikisikia habari za mtu kuambiwa na ugonjwa huu akawa anatibiwa ugonjwa kwa muda mrefu halafu baadae inakuja kugundulika hana huo ugonjwa.

Kuna mdada aliwahi kuhojiwa, aliambiwa na kansa akawa anachomwa mionzi kwa muda wa miaka 2 hadi wakataka kumkata ziwa, ila familia ikampeleka India kufika kule akaaambiwa hana cancer wala nini, ana tatizo dogo tu wakampa dawa na wakamwambia baada ya mwezi atakuwa salama. Dada alikuwa ashapitia majanga mengi mpaka kunyonyoka nywele.

Sasa kuna mke wa rafiki yangu, kwa zaidi ya miaka 5 wanamwambia ana vidonda vya tumbo anapewa madawa ya kutibu vidonda vya tumbo, pia alikuwa anaumwa shingo anaambiwa sijui mshipa gani wa fahamu umebinywa na kitu gani, hapo hayo majibu eti yamepatikana baada ya kufanyiwa MRI, kapigwa X-rays za kutosha pia. Lakini uwa anapata afadhali na hali inajirudia.

Juzi kaumwa sana wakamfanyia kipimo cha endoscope hospital nyingine, kile kipimo cha kudumbukiza camera mpaka huko kwenye utumbo. Yani hana cha vidonda vya tumbo wala nini bali ana fungus kwenye utumbo eti. Pia maumvu ya shingo wakagundua siyo mshipa kugandamizwa bali ana tatizo ingine tu siyo serious kama alivyokuwa ameambiwa.

Nikakumbuka kuna jamaa Mwarabu nilikuwa nasoma naye, mama yake alijifungua mtoto anajicho kama lina weusi, eti hospital ya mkoa wakasema ana kansa walitoe, mama akaamua kumpeleka Nairobi, wakagundua hana cancer yani ndivyo lilivyo tu wala halina tatizo na baada ya muda ule weusi ulikuwa unapotea taratibu mpaka ukaisha.

Sasa nikabaki ninajiuliza, hivi hawa wataalam wetu uwa wanashindwa tasiri vipimo wanavochukua wanafanya kubahatisha tu?
 
Madaktari ni binadamu na kila mmoja ana uelewa wake anapokuwa Darasani.

Siyo kila daktari anajua, wengine ni vilaza tu.

Ila tatizo kubwa kwetu kama watanzania ni ugumu wa kukiri jambo fulani silijui au nimeshindwa.

Hali hii imesababisha wagonjwa wengi kufariki au kutafutiwa matibabu sahihi when it's too late.

Yaani unakuta mtumishi wa afya huko zahanati badala ya kumfanyia referral mgonjwa ambaye anaona kabisa ameshashindwa, lakini anajifanya yuko nondo, mwishowe anakuja kumfanyia referral mgonjwa akiwa kwenye hali tete.

Na hali hii siyo kwa madaktari pekee, ni karibia sekta nzima ya afya. Maabara ndio kabisa, yale maparasites wanaoyakariri huwa ni wachache sana.

Wajanja huwa wanafanya team up ikionekana hawaelewi elewi.

Unaweza kuambiwa una ugonjwa fulani kumbe siyo.

Ukiona unatibiwa hupati unafuu ujue kabisa you're treating the wrong case.

Fanya vipimo maabara hata 5 ili uwe na uhakika.

Na madaktari walivyo, unakuta mtu kakariri tu cases ambazo ni common eneo husika kama Maralia, Typhoid, UTI,

Ikitokea rare disease tayari anakuwa hajui chochote cha kufanya. Ndio maana unakuta mtu ana dengue fever kawa diagnosed ana Maralia.

Mpaka ihe kujulikana haikuwa Maralia it's too late.
 
Hahahahahahaahhaah
Me waga wananichosha sana
 
Madaktari ni binadamu na kila mmoja ana uelewa wake anapokuwa Darasani.

Siyo kila daktari anajua, wengine ni vilaza tu.

Ila tatizo kubwa kwetu kama watanzania ni ugumu wa kukiri jambo fulani silijui au nimeshindwa.

Hali hii imesababisha wagonjwa wengi kufariki au kutafutiwa matibabu sahihi when it's too late.

Yaani unakuta mtumishi wa afya huko zahanati badala ya kumfanyia referral mgonjwa ambaye anaona kabisa ameshashindwa, lakini anajifanya yuko nondo, mwishowe anakuja kumfanyia referral mgonjwa akiwa kwenye hali tete.

Na hali hii siyo kwa madaktari pekee, ni karibia sekta nzima ya afya. Maabara ndio kabisa, yale maparasites wanaoyakariri huwa ni wachache sana.

Wajanja huwa wanafanya team up ikionekana hawaelewi elewi.

Unaweza kuambiwa una ugonjwa fulani kumbe siyo.

Ukiona unatibiwa hupati unafuu ujue kabisa you're treating the wrong case.

Fanya vipimo maabara hata 5 ili uwe na uhakika.

Na madaktari walivyo, unakuta mtu kakariri tu cases ambazo ni common eneo husika kama Maralia, Typhoid, UTI,

Ikitokea rare disease tayari anakuwa hajui chochote cha kufanya. Ndio maana unakuta mtu ana dengue fever kawa diagnosed ana Maralia.

Mpaka ihe kujulikana haikuwa Maralia it's too late.
NINI KIFANYIKE[emoji21]
 
Madr WA bongo ni kama waganga WA kichawi aka wazee WA ramli
Lakini haohao ndio wanaowatibu na mnapona.
Hizo ni rare cases tu,zisiwafanye muwaone hivyo.
Daktari na yeye ni binadamu,hakuna aliye mkamilifu..anaweza kukosea.
Haimaanishi kwamba hajui.
 
Lakini haohao ndio wanaowatibu na mnapona.
Hizo ni rare cases tu,zisiwafanye muwaone hivyo.
Daktari na yeye ni binadamu,hakuna aliye mkamilifu..anaweza kukosea.
Haimaanishi kwamba hajui.
Ramli ipo pale pale
 
Nimekuwa nikisikia habari za mtu kuambiwa na ugonjwa huu akawa anatibiwa ugonjwa kwa muda mrefu halafu baadae inakuja kugundulika hana huo ugonjwa.

Kuna mdada aliwahi kuhojiwa, aliambiwa na kansa akawa anachomwa mionzi kwa muda wa miaka 2 hadi wakataka kumkata ziwa, ila familia ikampeleka India kufika kule akaaambiwa hana cancer wala nini, ana tatizo dogo tu wakampa dawa na wakamwambia baada ya mwezi atakuwa salama. Dada alikuwa ashapitia majanga mengi mpaka kunyonyoka nywele.

Sasa kuna mke wa rafiki yangu, kwa zaidi ya miaka 5 wanamwambia ana vidonda vya tumbo anapewa madawa ya kutibu vidonda vya tumbo, pia alikuwa anaumwa shingo anaambiwa sijui mshipa gani wa fahamu umebinywa na kitu gani, hapo hayo majibu eti yamepatikana baada ya kufanyiwa MRI, kapigwa X-rays za kutosha pia. Lakini uwa anapata afadhali na hali inajirudia.

Juzi kaumwa sana wakamfanyia kipimo cha endoscope hospital nyingine, kile kipimo cha kudumbukiza camera mpaka huko kwenye utumbo. Yani hana cha vidonda vya tumbo wala nini bali ana fungus kwenye utumbo eti. Pia maumvu ya shingo wakagundua siyo mshipa kugandamizwa bali ana tatizo ingine tu siyo serious kama alivyokuwa ameambiwa.

Nikakumbuka kuna jamaa Mwarabu nilikuwa nasoma naye, mama yake alijifungua mtoto anajicho kama lina weusi, eti hospital ya mkoa wakasema ana kansa walitoe, mama akaamua kumpeleka Nairobi, wakagundua hana cancer yani ndivyo lilivyo tu wala halina tatizo na baada ya muda ule weusi ulikuwa unapotea taratibu mpaka ukaisha.

Sasa nikabaki ninajiuliza, hivi hawa wataalam wetu uwa wanashindwa tasiri vipimo wanavochukua wanafanya kubahatisha tu?
Tz yetu, kila kitu ni bahati nasibu. Inatisha, na inasikitisha
 
Madaktari ni binadamu na kila mmoja ana uelewa wake anapokuwa Darasani.

Siyo kila daktari anajua, wengine ni vilaza tu.

Ila tatizo kubwa kwetu kama watanzania ni ugumu wa kukiri jambo fulani silijui au nimeshindwa.

Hali hii imesababisha wagonjwa wengi kufariki au kutafutiwa matibabu sahihi when it's too late.

Yaani unakuta mtumishi wa afya huko zahanati badala ya kumfanyia referral mgonjwa ambaye anaona kabisa ameshashindwa, lakini anajifanya yuko nondo, mwishowe anakuja kumfanyia referral mgonjwa akiwa kwenye hali tete.

Na hali hii siyo kwa madaktari pekee, ni karibia sekta nzima ya afya. Maabara ndio kabisa, yale maparasites wanaoyakariri huwa ni wachache sana.

Wajanja huwa wanafanya team up ikionekana hawaelewi elewi.

Unaweza kuambiwa una ugonjwa fulani kumbe siyo.

Ukiona unatibiwa hupati unafuu ujue kabisa you're treating the wrong case.

Fanya vipimo maabara hata 5 ili uwe na uhakika.

Na madaktari walivyo, unakuta mtu kakariri tu cases ambazo ni common eneo husika kama Maralia, Typhoid, UTI,

Ikitokea rare disease tayari anakuwa hajui chochote cha kufanya. Ndio maana unakuta mtu ana dengue fever kawa diagnosed ana Maralia.

Mpaka ihe kujulikana haikuwa Maralia it's too late.
Ila tatizo kubwa kwetu kama watanzania ni ugumu wa kukiri jambo fulani silijui au nimeshindwa.
inshu kubwa iko hapa
 
I've been sick recently kila nikipima eti sina ugonjwa nashangaa kabisa I fall weak how comes siumwi?? Mambo ndo kama hivi
Ukiambiwa hauumwi,inabid utafute hospital ambayo iko bora zaidi.
Kuna watu tulishaambiwa kuwa hatuna ugonjwa,tukahis tumerogwa kwenda kwa sangoma hakuna nafuu iliyopatikana tatizo ilikuwa n macho baadae tukarudi hospital kubwa yenye vifaa vya uhakika,ikagundulika mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye macho n kama imeziba lakin tayari tulikuwa tumeshachelewa
 
Usomaji wetu ni shida eti unapewa picha ya tatizo hata haina muonekano mzuri afu unaambiwa huyo sijui ni parasite gani wakati picha inaonesha ukungu tu,mwisho wa siku tunaishia kukariri
 
Mkuu unaelewa ulichoongea kweli?

Daktari akikosea ina maana mtu kafa. Acha kutetea ujinga.
Sitetei ujinga mkuu.
Hizo case hutokea Mara chache hata Mimi imewahi nitokea daktari alikosea kung'oa jino..akang'oa lisilo na tatizo lenye tatizo likaachwa..lakini huyo ni daktari bingwa anayewang'oa watu vizuri miaka na miaka..daktari ni binadamu pia,hayupo perfect muda wote.
 
Wife aliambiwa ana uvimbe tumboni anaitaji operation tumekaa tumejiandaa kwa siku ya operation , siku imefika tukakuta daktari mwingine. Akaletewa file kusoma na picha zote akasita kufanya operation wakaitana uko tukaambiwa hakuna uvimbe tuondoke walikosea kusoma vipimo , aiseee
 
Back
Top Bottom