Hivi Mbunge Shabiby alifikiria kuhusu waajiriwa wanaokatwa bima ya afya?

Hivi Mbunge Shabiby alifikiria kuhusu waajiriwa wanaokatwa bima ya afya?

Mgeni wa Jiji

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2017
Posts
9,758
Reaction score
18,431
Wakuu mimi sina mambo mengi sana hapa najaribu kufikiria, hivi Mh. Shabiby aliwaza kweli kuwa kuna watu ambao wao wanakatwa bima moja kwa moja kwenye mishahara yao?

Hawa wataondolewaje kwenye huo mfumo aliopendekeza sababu na wao ni wamiliki wa simu watakaokatwa bima mara mbili.

Labda alimaanisha watu wakatwe ili kuchangia wengine je hii ni sahihi?, kwanini mtu alazimishwe kulipia matibabu ya mtu mwingine bila hiyari yake.

Najaribu kuwaza tu wakuu, huu mfumo sidhani kama utakuwa na tija kwa taifa, badala yake fedha tunazokusanya kama taifa.zielekezwe kwenye mambo ya msingi kitaifa na sio posho na matumizi yasiyo ya muhimu na lazima.

Kwa sekta ya utalii tu kama tukiitumia vizuri hatutakuwa na wasiwasi kwenye huduma kama afya, elimu na miundombinu. Lakini badala ya kuwaza na kutekeleza haya tunatafuta njia rahisi za ukusanyaji hela.

Haya je ununuzi wa vocha ukipungua, hizo fedha zitapatikana vipi? Je, haoni kuwa hii itapandisha gharama za vifurushi na huduma za mitandao?

Mimi ni hayo tu waungwana.
 
Mimi nilishasema watu waliovimbiwa huwa hawajui kama kuna watu ambao wamelala na njaa , na nilikomenti kwenye uzi mwingine wa namna hii kuwa yule mavirusi yake yakishapanda kichwani anakua anabwabwaja tu hamna anachojua cha maana
 
Yeye hawazi hilo, wakuliwaza ni sisi ambao kimsingi hatuwezi kubadilisha chochote tunachoweza ni kulalamika tu.
 
Viongozi walivyo wa ajabu wanaweza kupitisha ili wazo, mitandao ya simu ikipandisha gharama ya vifurushi kuendana na thamani halisi, viongozi hao hao wataanza kuisonga songa mitandao ya simu.
 
Wakuu mimi sina mambo mengi sana hapa najaribu kufikiria, hivi Mh. Shabiby aliwaza kweli kuwa kuna watu ambao wao wanakatwa bima moja kwa moja kwenye mishahara yao?

Hawa wataondolewaje kwenye huo mfumo aliopendekeza sababu na wao ni wamiliki wa simu watakaokatwa bima mara mbili.

Labda alimaanisha watu wakatwe ili kuchangia wengine je hii ni sahihi?, kwanini mtu alazimishwe kulipia matibabu ya mtu mwingine bila hiyari yake.

Najaribu kuwaza tu wakuu, huu mfumo sidhani kama utakuwa na tija kwa taifa, badala yake fedha tunazokusanya kama taifa.zielekezwe kwenye mambo ya msingi kitaifa na sio posho na matumizi yasiyo ya muhimu na lazima.

Kwa sekta ya utalii tu kama tukiitumia vizuri hatutakuwa na wasiwasi kwenye huduma kama afya, elimu na miundombinu. Lakini badala ya kuwaza na kutekeleza haya tunatafuta njia rahisi za ukusanyaji hela.

Haya je ununuzi wa vocha ukipungua, hizo fedha zitapatikana vipi? Je, haoni kuwa hii itapandisha gharama za vifurushi na huduma za mitandao?

Mimi ni hayo tu waungwana.
Hili bunge la mchongo linadhoofisha sana watu wa kada ya kati na chini, Rev. Mtikila was right ipo siku ngozi nyeupe itawakandamiza watu weusi, alianza Zungu, amekuja Shabiby, Rostam tusubiri wengine
 
Back
Top Bottom