Messi huyo huyo ndie anayevunja rekodi za akina Pele na Zidane na Ronaldinho. Mpira ni zaidi ya mbwembwe uwanjani, ule mpira wa kucheza na jukwaa haupo tena siku hizi.
ndo maana nikasema ukitazama mafanikio ya haraka na ushabiki utamsifu messi anayepewa mpira na xavi ama Iniesta... kuvunja rekodi ni jambo litakalo fanywa sana kwa kizazi hiki... za messi zitavunjwa ndani ya miaka michache mno... ni mabadiliko ndani ya mpira...
kama ni mpenzi wa mpira, tazama the way hazard anavyoweza kukufanya usisimke akicheza.. wengi wanasema anaweza kuwa bora kuliko wote shida yake hataki kujivika ufalme wa kufunga magoli.... hapa ndipo kwenye tatizo.. tunauona ubora kwenye goli tu..mpira si burudani as ilivyokuwa zamani sasa hivi ni matangazo na jambo la kuleta umaarufu wa pesa na sio furaha. ndio maana messi singano analia na simba, Ronaldo anapiga mpira kwa hasira alvaro akishinda.. unaweza jiuliza kwanini Ronaldo anasusa kisa hajapewa pasi azidishe idadi ya magoli ya kupewa.? ni kwasababu akipata golden boot anapiga hela kwenye matangazo ya boxer na t-shirts za fubu(kampuni hii ipo hivi??) ...
demba ba angecheza mbele ya xavi, iniesta,beki inayoingiza mpira kama jordi na alves plus pedro na wengine katika ligi ya uhispania(rejea maneno ya mourinho juu ya ligi hizi mbili) angefunga dozen ya magoli. suarez alifunga goli ngapi katika ubora wake ndani ya liver? katika mwanzo wa kusuasua wa barca angalia katia ngapi...
kwangu ligi ya Spain ilikuwa ligi ya vitu ambavyo hauvioni premier na Bundesliga. ligi ya ujuzi wa man alone van niestroy. ligi ya ufundi wa dinho.. ligi ya Zidane.... ligi ya Ronaldo de lima...
kwenye jambo hili pengine unaweza kufananisha na mchezo wa boxing... Mayweather na manny wamefanya pambano la hela nyingi na heshima kuliko yote duniani.ndio maana Mayweather anapata jeuri yakujiona yuko sawa na Mohammed alli.. tazama ubora wa pambano fananisha na ngumi za Frazier na kina alli na mchezo wa Tyson Mike kijana... unaweza kuona nani ni nani lakini mtaani tunasema Mayweather nomaaaa... wakati kashinda kwa kuomba msaada wa kulala juu ya kamba na kukimbia kama bolt ulingoni...
messi ni bora ila atafanya kazi kunishawishi kuwa yeye ni bora kuliko okocha, kazidi utamu wa Ronaldo wawili wa brazil de lima na dinho.... kamfunika Zidane... au ye ni bora kuliko pele na maradona....