Hivi Michael Jackson alikuja Tanzania na kugoma kushuka uwanja wa ndege na kusalimiana na Mzee Mwinyi kisa Tanzania hewa yake ni chafu?

Hivi Michael Jackson alikuja Tanzania na kugoma kushuka uwanja wa ndege na kusalimiana na Mzee Mwinyi kisa Tanzania hewa yake ni chafu?

Ilichukuliwa Tanzania; ile sehemu ya Elephants na forest

MJ alikuwa anaipenda sana Africa

Wengi wanadhan MJ alikuwa anajichubua but uzushi mtupu

MJ had skin disorder, Virtiligo , skin disorder that destroys pigmentation

Hizo story kuwa aliona TZ chafu ni story za Chadema na Tundu Lissu
Huwa nikiangalia MJ alivyotumia talanta yake kuusaidia ulimwengu huu na kufikisha jumbe na prophecies lkn watu wanavyokuja kumchafua ndipo nakumbuka duniani hapa jipiganie ww tu na labda circle yako.

Ngoma kama Earth song, ile ni prophecy, we're the world, heal the world, hamna msanii dunia hii aliofanya hayo. Lkn leo hii MJ anaonekana kama alichukia weusi na masikini wakati alikua ni mtu mwenye upendo sana kwa wasio jiweza
 
mdogo wangu hata mimi hiyo story nikiisikia ila hakugoma kushuka inasemekana siku anatimba MJ kuna sehemu ya jiji walikuwa wamechoma taka sasa ule moshi ukawa unaelekea maeneo ya airport ukichanganya na ule moshi wa pale feri wa kukaanga samaki ikawa hewa mchanganyiko kama anajua zaidi aongezee nyama
Hamna lolote. Hizo ni story za vijiwe vya kahawa. Michael Jackson ana mtindo wa kuvaa barakoa tokea huko US.

Sehemu nyingi anapokwenda huwa anafunika uso wake na barakoa sasa waswahili wakaona kuwa hiyo ni ishara ya kuzuia harufu mbaya wakatunga uongo wao.

Michael Jackson hana hizo dharau za kwenda sehemu na kuwaponda wenyeji wakati amekwenda kujichanganya na watu vijijini huko.

Hizo ni story za uvumi na si kweli.
 
Huwa nikiangalia MJ alivyotumia talanta yake kuusaidia ulimwengu huu na kufikisha jumbe na prophecies lkn watu wanavyokuja kumchafua ndipo nakumbuka duniani hapa jipiganie ww tu na labda circle yako.

Ngoma kama Earth song, ile ni prophecy, we're the world, heal the world, hamna msanii dunia hii aliofanya hayo. Lkn leo hii MJ anaonekana kama alichukia weusi na masikini wakati alikua ni mtu mwenye upendo sana kwa wasio jiweza
Kama uliisikiliza vzuri Earth Song alikua anamlaum Mungu.
 
Hajawahi kutoa kauli hiyo ety kuna harufu mbaya, MJ alienda mbugani. acheni useng3

Hayo mambo ya kushika pua na kuziba pua na mdomo hy ni kawaida yake hata ukiwa kwake, alishawahi kuhojiwa na kusema kuna muda pua yake inamkosesha uhuru kutokana na operesheni

Popobawa ni chai tuu hakunaga hizo ishu

Sasa pale ferry pana harufu gn mbaya ad mwanaume mzima uanze kukimbia.? Nyie ndo mkiitwa upinde mnaanza kukasirika
Kilichoripotiwa na vyombo vya hbari wakati huo ndo hicho.
 
Kwani alikuja Tanzania kuongea na Mwinyi, yule ni mwanamziki alialikwa kuja kuimba, kuna picha yoyote anaimba ? Yule mbana pua alikatisha ziara
 
Wazee leo imebidi niulize,
Maana naona watoto wa miaka ya 90 kama tulikua tunapigwa fiksi mno na wazazi au wakubwa wetu....

Nimekua miaka ya 2000 na hivi nikiamini stori niliyoikuta kuwa mwanzoni mwa miaka ya 1990 sijui 1992 alikujaga bana Wako Jack (MJ) Gwiji Michael Jackson hapa Ti-ziii

Eti nasikia mwamba alifungua mlango wa ndege pale airport kabla hajashuka chini alipokuwa akisubiriwa na umati ikiwapo Rais Mwinyi enzi hizo, eti MJ akabinya pua yake kama mtu alonakinyaa akasema Tanzania inanuka haina hewa safi ya yeye kuvuta ...

Eti mwamba MJ akamwambia rubani wa ndege wang'oe...yaani hakushuka ndege likageuza hilo marekani....😂😂

Sasa wadau nimeuliza hivi maana leo nimekuta hiyo picha hapo nimeambatanisha na post ya MJ akiwa nyumbani kwa Mwinyi enzi hizo. yaani wamerelax wanakula stori....

Imebidi niulize hawa wazazi au watu wa zamani walikua wanatuchukuliaje watoto aisee!? kwa fiksi walizokuwa wanatupa!?

Yaani mimi mpaka leo na utu uzima wangu nilikua naamini kuwa MJ sio mwana kabisa kwa kitendo alichokifanya😂😂 kumbe nililishwa maneno mbofumbofu na story za kitaa enzi hizo hakuna vyanzo vya habari hata kuhakiki ukweli wa story...

Tuachage kulisha matango pori watoto sio vizuri jamani.....

Rest in peace MJ na Mzee RuksaView attachment 2921940
Hata mm hiyo story niliisikia, na ndo nilielewa hivyo hadi leo kabla sijaiona hii picha.
 
Vijana wa siku hizi wanapenda sana kueneza taarifa za uwongo bila hata kuzichambua kwanza kabla ya kuzieneza; Huyu alieanzisha thread hii tayari naye anachangia kusambaza taarifa za uwongo. Kama MJ hakushuka kwenye ndege hiyo picha aliyopiga na Mwinyi walikuwa wapi.

MJ alikuwa na tabia ya kuweka face mask (bala ya korona) kuzuia hewa ya vumbi hata aakiwa Marekani. ALipokuja Tanzania alikuwa na face mask hiyo, ambayo alikuwa akiivua anapokutana na viongozi wa serikali kama anavyookena kwenye picha hiyo na pia alipopokelewa na Hassan Diria aliyekuwa Waziri wa Mambo ya nje wakati huo
1709490727323.png

1709490968187.png
 
alibana pua kwa sababu msimu anakuja ulikua msimu wa joto kali. na kipindi cha joto kali hewa huwa ni thick. hiyo ilikua ndio sababu ya yeye kupata shida ya kuvuta hewa ikaonekana akishika pua yake na athari zaidi ni pua yake vile ilikua imefanyiwa surgery.
 
Back
Top Bottom