Hivi mito ya Dar ina samaki?

Hivi mito ya Dar ina samaki?

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Wakuu hivi mito kam Msimbazi, Mzinga nk, ina samaki? Imewahi kuwa na samaki? Ningependa tu kujua.
 
Kwa uchafu uliopo ndani ya mito hiyo, sitegemei kukuta samaki anayefaa kuliwa, hata kama wapo
 
Kwa jinsi ilivyo michafu hata Samaki wenyewe wameghairi kuishi humo.

Ule Mto pale Kigogo mwisho ukipita SAA 9:30 unakuta maji mekundu, SAA 11:00 maji ya Buluu, SAA 13:32 maji meusi, SAA 15:02 maji mekundu, SAA 16:13 maji ya Njano.

Sasa hapo Samaki gani mjinga atakubali kuishi kwenye maji yanabadilika badilika kama Kinyonga?
 
Samaki wapo ila wa kiduwanzi tu.niliwao ona jamaa anavua kambale pale mto msimbazi.

Pia baadhi ya mifereji kama ya mikocheni na msasani ina kambale sana especially misimu ya mvua

Sent from my CPH1803 using JamiiForums mobile app
i second this

samaki wavumilivu wanaoishi hata kwenye shimo la choo kama kambare unawakuta, sometime hata mjini kwenye mifereji wapo.
 
Samaki watoke wapi na wakati hiyo mito karibia yote hubeba maji taka ya chooni na yale ya viwandani? Halafu maji hayo hayo machafu unakuta ndiyo wanamwagilia bustani za mbogamboga! 🥵

Mimi ndiyo maana nikifika Dar, huwa sili mboga za majani!🥦🥬🥕🍆
 
Pongezi za dhati kwa wananchi wanaoishi Tabata Magengeni, Tabata Kimanga Kisukulu, Tandale na viunga vyake, Kigogo Mburahati, Kigogo Luhanga, Polisi post, Mikumi chini huku kwenye lile bonde, Kigogo centre darajani na mitaa ya Gilmani Rutihinda, Jangwani yote hadi Mchikichini.

Haya maeneo yana asili ya chemchem hivyo mashimo yao ya vyoo sio marefu sana sasa ikinyesha mvua automatically vyoo vinaflood.

Sasa na wananchi wa maeneo hayo walivyo wapumbavu huwa wanatapisha vyoo hivyo kipindi cha mvua na kufanya uharibifu mkubwa wa mazingira hasa harufu chafu ya choo kikubwa katika maeneo hayo yaani ni kinyaa mana kila mtaa unakuta unanuka. mavimavi.
 
Kwa jinsi ilivyo michafu hata Samaki wenyewe wameghairi kuishi humo.

Ule Mto pale Kigogo mwisho ukipita SAA 9:30 unakuta maji mekundu, SAA 11:00 maji ya Buluu, SAA 13:32 maji meusi, SAA 15:02 maji mekundu, SAA 16:13 maji ya Njano.

Sasa hapo Samaki gani mjinga atakubali kuishi kwenye maji yanabadilika badilika kama Kinyonga?
Miaka ya nyuma ule mto ulikuwa na samaki, kambale na perege na watu walikuwa wanavua kwa kitoweo lakin baada ya watu kuvamia ule mto kwa kuanza kujenga makazi pembezoni mwa mto na kutiririsha maji machafu ya vyooni mbaya zaidi kuna kiwanda cha nguo kinaitwa NIDA kama sijakosea kipo Tabata nacho kikaanza kutiririsha maji machafu ya kiwandani during those days nilikuwa nasoma primary na njia yngu kubwa kwenda/kurudi shule ilikuwa pale darajani nilishuhudia vijana wengi wa maeneo yale wakiopo hao samaki waliokuwa wanakufa kwa sumu ya maji ya kiwandan since then nadhan samaki ndio waliishia pale mpaka namaliza std 7 nikiwa napita pale nikawa nashuhudia mabadiliko ya rangi ya maji tu mara blue, red, black and etc. Sijui NEMC walikuwa wapi wakati ule na mpaka sasa sijui wapo wapi😣😣,!!! Lile bonde kabla halijaathiriwa na uchafuzi wa mazingira nakumbuka walikuwa wanalima sana mpunga na mchicha
 
Back
Top Bottom