Hivi mjini matajiri wanaishije? Kiukweli kila nikiwatazama kulinganisha na hali yangu, naishia kusema maisha ni fumbo!

Hivi mjini matajiri wanaishije? Kiukweli kila nikiwatazama kulinganisha na hali yangu, naishia kusema maisha ni fumbo!

Kama wewe ni mwenzangu na Mimi tunaopambana anagalao tufike sehemu nzuri, kuna ile unawatazama waliofanikiwa na mbilinge zao za maisha unaishia kusema hakika utajiri ni Ngumu.

Just see few Case studies

- Mtu ana mabasi 7 isitoshe amechukua mkopo mrefu benki, marejesho kila mwezi bahati mbaya basi tatu zinakula mbanga bila kutarajia. Lakini cha ajabu unamkuta tajiri ana kula maisha party after party hawazi.

- Kuna wale matajiri waliofilisiwa kipindi cha JPM kwa makosa ya uhujumu uchumi. Mali zao nyingi zilitaifishwa but tuna kutana nao as if nothing happened 😁😁 na wanapambana kama hamna kilichotokea.

Kuna wenzangu na Mimi unapambana unapata hela kiasi flani unaanzisha mradi wako bahati mbaya ukifeli na wewe umefeli na inakuwa ni simulizi ya Karne kwa kila mtu 😁😁😁

Hakika nihitimishe kwa kusema maisha ni fumbo gumu sana ndugu zangu.
Backup Generator umeme ukizima ghafla inawaka hapo hapo na umeme ukirudi inasubiri kipindi kidogo inajizima yenyewe, ndio hivyo nimekufafanulia sasa km huna backup Generator imekula kwako usishangae sana matajiri wana umoja wao wanapeana tag kunyanyuana mmoja wao anapofeli hawapo pekeyao wapo kundi unaweza kuta matajiri 100 wameungana hao 100 wakimchangia tajiri mwenzao mmoja aliekwama hata milioni 50 50 tu mwenzao anarudi kwenye mstari then atakua anarejesha taratibu taratibu
 
Back
Top Bottom