Hivi Mkurugenzi mmoja wa halmashauri kukaa kituo kimoja kwa zaidi ya miaka 3 hakuwezi kuwa sababu ya kutengeneza ufisadi?

Hivi Mkurugenzi mmoja wa halmashauri kukaa kituo kimoja kwa zaidi ya miaka 3 hakuwezi kuwa sababu ya kutengeneza ufisadi?

Nimekuwepo kwenye utumishi wa umma huu mwaka 4 sasa katika halmashauri moja huku mkoani Morogoro.Tangu nilipofika katika halmashauri hii 2020 nilimkuta mkurugenzi ambaye tayari alikuwepo hapa tangu 2018.

Kwa muda huu wa miaka 3 ambao nimekuwepo hapa,nimeona na kusikia dili nyingi za kifisadi zikifanyika kupitia mtandao wa maafsa waliotengenezwa na mkurugenzi huyo ili kupitisha dili chafu. Mbinu anayotumia kuwateka maafsa hao ni pamoja na kuwatengenezea mazingara magumu ya kiutendaji na kimaslahi, huku akiwajengea uoga kwa kuwakaripia na wengine kutowapa majukumu yao ya kiofisi kabisa.Haya mambo aliyafanya kwa muda wa kati ya mwaka 1 hadi 2 kwa mujbu wa watumishi niliowakuta hapo,na kwa wale waliojishusha na kukubali kupelekwapelekwa kwa matakwa yake,ndiyo baadae walikuja kuwa njia ya kupitisha dili zake chafu mpaka leo.

Mimi kwa ushuhuda wangu mwenyewe nimethibitisha kupitia Afsa usafirisha wa halmashauri ambaye yeye alibaki na msimamo wa kufuata kanuni na taratibu za kazi yake,akiewekwa pembeni na na nafasi yake kupewa Afisa mmoja wa elimu msingi,yeye mwenye taaluma yake amekuwa msoma magazeti ofisini bila ya jukumu lolote mwaka wa 2 huu sasa.

Kwa kupitia TO wa mchongo,pesa kuanzia za matengenezo ya gari,mafuta,vipuri n.k zinapigwa na magari ni mabovu siku zote.Utaratibu wa kisheria wa ukaguzi wa magonjwa ya gari na matengenezo haufuatwi tena na gari zinatengenezwa mitaani kwa gharama ndogo huku zimetolewa pesa nyingi.

Wito wangu ni kwa Rais Samia, asijiamini kwamba huku chini pako vizuri na kumbe ndiyo kunaufisadi mkubwa unaosababishwa na hawa wakurugenzi kwa kukaa halmashauri moja muda mrefu na kupelekea kutengeneza cheni za upigaji.

Kifupi ufisadi ni janga kubwa kwa sasa.
Huwezi kurekebisha kila kitu Wacha wazipige
 
Hata siko serikalini mkuu,
Ila harakat zangu nafanya kazi sn na watu wa serikalini, hasa hao wakurugenzi.

Hebu acheni chuki za kijinga,number hazidanganyi,jamaa mchapakazi sana[emoji4]
Ndo maana unamtetea jamaa wako huyooo, ukute ana sifa mbaya wee unampamba tyuuh, binamu acha hizo bhana
 
Jamaa anasagiwa Sana kunguni
Na wafanyakazi wa serikali maana hawapi pumzi,Ni kazi kazi, ukizingua anakuzingua.

Ila panga pangua zote wanasali na kuomba ila jamaa anabakishwa TU.

Wati hawajui kupima performance ya mtu,

Unafikiri wanahamisha hamisha tu?

Jamaa mnyonge mnyongeni,
Ile halmashaur kaijenga Sana TU.
Watumishi Wana nidhamu haswa[emoji4]
Unajua ni magari mangapi yapo juu ya mawe na madereva baadhi wamekaa tu bila ya majukumu kwa zaidi ya miaka 2!?.Unajua kuwa kuna magari yapo gereji mwaka 4 sasa na baadhi yalilipiwa pesa lakini hazikufika!?.
Huyo mtu wako anajificha katika hayo unayo sema,lakini ndani ya ofisi kuna ufisadi mkubwa kupitia hao maafsa aliowatengene,na nikawaida kuwa mstari wa mbele kumtetea kama ufanyavyo.
Serikali ina ajiri mtumishi ili akafanye kazi kwa mujbu wa kanuni na sheria za kazi na ndipo alipwe mshahara.Sasa wewe unaona ni sahihi mtumishi kuondolewa katika nafasi yake na akabaki kusaini tu kitabu cha maudhurio asubuhi na mchana kisha anakaa tu bila ya kazi na huku anaendelea kulipwa mshahara?.
 
Hahahaaa!Tupa jiwe giza ukisikia yalaa!Jua tayari.Bila shaka wewe ni sehemu ya mwanamtandao wake,umizeni tu watumishi wengine kwa hongo mnazopewa ili kupitisha dili zenu.Ila hipo siku mtakuja hungama.
Pole Sana mkuu

Ebu acha chuki zako tujenge taifa letu

Una tuhuma dhidi yake weka ushahidi mezani, Sio kuzusha Maneno ya uongo kumchafua bure jamaa.

Ushahidi wangu nmeshakupa tayar
-fuatilia makusanyo mapato ya ndani ya mkoa,halmashaur Yake iko namba ngap.

Kashusha ushuru na tozo kandamizi ili Watu walipe waache magendo,sahv Unalipa ushuru wako Safi na hatukimbizani Tena na polisi Kama zamani.

-fuatilia matokeo ya kielimu kuanzia STD 4,7 Hadi form 4,halmashaur Yake iko namba ngapi kitaifa.
Walimu walevi,watoro na wazembe anawanyoosha kweli kweli.

Mwaka Juzi naskia Kuna mtendaji kalewa kilabuni kaibiwa ushuru na mashine ya risiti,mkurugenz kamfuma kamlamba sticky Kama mwanafunzi[emoji1787]

-Fuatilia response ya wakulima na wafanyabiashra waliowekeza kwny halmashaur Yake Ni Kias gani anakubalika.

Halmashaur Yake ukiwa mwekezaji na mdau wa maendeleo unanyenyekewa mno.

WATUMISHI WAZEMBE NA WAPIGA DILI MNATESEKA SANA AISEE[emoji4]
 
Hata siko serikalini mkuu,
Ila harakat zangu nafanya kazi sn na watu wa serikalini, hasa hao wakurugenzi.

Hebu acheni chuki za kijinga,number hazidanganyi,jamaa mchapakazi sana[emoji4]
Mkuu!Gari inaweza kuendelea kukaa gereji mwaka mzima ili hali pesa ya matengenezo ilitolewa kesh?.T.O na madereva wake wa wili wote wamekalishwa benchi kwa zaidi ya miaka 2 sasa na huku wakilipwa mishahara,kwako wewe hii hipo sawa?.
 
Ndo maana unamtetea jamaa wako huyooo, ukute ana sifa mbaya wee unampamba tyuuh, binamu acha hizo bhana
Binamu,
Kwny harakati zangu Nmefanya kazi na wakurugenzi wengi sn Hapa nchini.

Hasa kwny biashara za mazao,
Changamoto kubwa Ni watumish wa chini kua POA POA na mkurugenz, urasimu kila Kona.

Unanyanyasika Sana maana huna pa kusemea,wote mkurugenz,watumish Ni usumbufu,urasimu na rushwa Kwenda mbele.

Sasa halmashari ya jamaa,Yuko very strict na hataki konakona na urasimu kwa wadau wake wa maendeleo.

Ndo maana hata akiwa na Jambo lake,
Response ya wafanyabiashara,wakulima na wadau wa maendeleo iko chap Sana[emoji4]
 
Mkuu!Gari inaweza kuendelea kukaa gereji mwaka mzima ili hali pesa ya matengenezo ilitolewa kesh?.T.O na madereva wake wa wili wote wamekalishwa benchi kwa zaidi ya miaka 2 sasa na huku wakilipwa mishahara,kwako wewe hii hipo sawa?.
Hayo Mambo yenu ya ndani wafanyakazi wake ata siyajui,nadhan mna vikao vya ndani, mkae myaongee myamalize.

Jamaa mbona msikivu sn, japo ubabe Kias flan anao, pale akitaka kuforce jambo lake lipite.

Binafs nmeongelea kwa general view, Kwa niliyoyasikia na kwa jinsi nilivofanya nae kazi na navomjua.

Ila takwimu za performance yake kiujumla hazidanganyi,ndo maana kaaminiwa kukaa pale MDA mrefu hivo
 
Mkuu!Gari inaweza kuendelea kukaa gereji mwaka mzima ili hali pesa ya matengenezo ilitolewa kesh?.T.O na madereva wake wa wili wote wamekalishwa benchi kwa zaidi ya miaka 2 sasa na huku wakilipwa mishahara,kwako wewe hii hipo sawa?.
Ila si mnalipwa lakni nikafikiri mnakaa benchi na hamlipwi daah 😃😃😃


Labda na yeye kasomea hayo mambo anawapunguzia majukumu,

Ishini na Mkurugenzi wenu vizuri ndio boss wenu
 
Hayo Mambo yenu ya ndani wafanyakazi wake ata siyajui,nadhan mna vikao vya ndani, mkae myaongee myamalize.

Jamaa mbona msikivu sn, japo ubabe Kias flan anao pale akitaka kuforce jambo lake.

Binafs nmeongelea general view Kwa niliyoyasikia na kwa jinsi nilivofanya nae kazi na navomjua.

Ila takwimu za performance yake kiujumla hazidanganyi,ndo maana kaaminiwa kukaa pale MDA mrefu hivo
Hawa wanawivu tu, huyo T.O ajue kua mkurugenzi ndio boss wake akisema a na yeye aitikie a ukienda beyond hapo anaishia kujuta kama hivi

Aishi na mkurugenzi kwa akili ata enjoy😂😂😂


Tatizo ujuaji mwingi ndo unaponza
 
Pole Sana mtumishi,

Ebu acha chuki zako tujenge taifa letu

Una tuhuma dhidi yake weka ushahidi mezani, Sio kuzusha Maneno ya uongo kumchafua bure jamaa.

Ushahidi wangu nmeshakupa tayar
-fuatilia makusanyo mapato ya ndani ya mkoa,halmashaur Yake iko namba ngap.

Kashusha ushuru na tozo kandamizi ili Watu walipe waache magendo,sahv Unalipa ushuru wako Safi na hatukimbizani Tena na polisi Kama zamani.

-fuatilia matokeo ya kielimu kuanzia STD 4,7 Hadi form 4,halmashaur Yake iko namba ngapi kitaifa.
Walimu walevi,watoro na wazembe anawanyoosha kweli kweli.

Mwaka Juzi naskia Kuna mtendaji kalewa kilabuni kaibiwa ushuru na mashine ya risiti,mkurugenz kamfuma kamlamba sticky Kama mwanafunzi[emoji1787]

-Fuatilia response ya wakulima na wafanyabiashra waliowekeza kwny halmashaur Yake Ni Kias gani.

Halmashaur Yake ukiwa mwekezaji na mdau wa maendeleo unanyenyekewa mno.

WATUMISHI WAZEMBE NA WAPIGA DILI MNATESEKA SANA AISEE[emoji4]
Kwako wewe ni sawa dereva muajiriwa hanyimwe gari ila ndugu yake asiye muajiri na wala hana mkataba apewe gari?.
 
Ungeenda kuweka kwenye post ingekuwa jambo jema coz sio kila mtu atapitia COMMENTS zote kutafutiza kama kuna mtu kataja. Mtoa POST angeweka kwenye UZI wake
Tatizo Mtoa mada kaileta kimajungu zaidi,

Ile kutupa jiwe gizani, mtandao Kama jf hayo Mambo yashapitwa na Wakati, alipaswa aweke wazi ili asaidiwe tatizo lake.

Kumbe tatizo lake Ni Madreva waliosimamishwa kazi kwa uchakavu wa magari uko gereji[emoji4]
 
Tatizo Mtoa mada kaileta kimajungu zaidi,

Ile kutupa jiwe gizani, mtandao Kama jf hayo Mambo yashapitwa na Wakati, alipaswa aweke wazi ili asaidiwe tatizo lake.

Kumbe tatizo lake Ni Madreva waliosimamishwa kazi kwa uchakavu wa magari uko gereji[emoji4]
Huyu atakuwa T.O bILA CHAKA
 
Hawa wanawivu tu, huyo T.O ajue kua mkurugenzi ndio boss wake akisema a na yeye aitikie a ukienda beyond hapo anaishia kujuta kama hivi

Aishi na mkurugenzi kwa akili ata enjoy[emoji23][emoji23][emoji23]


Tatizo ujuaji mwingi ndo unaponza
Kabisa,
mtoa mada tatizo lake nadhan liko hapo

akae vzur na boss wake wayamalize

Hapo huenda Ni kutunishiana misuli,

Transport officer anasema
"utanifanya Nini boss,ushahidi hamna?"

Boss anasema,
"Hutaki kufuata maelekezo yangu,kazi sikufukuzi, wilaya sikuhamishi, utakaa benchi usome magazeti asbh Hadi jioni,uishi kwa mshahara tu mwezi Hadi mwezi"

Ujue nnavowajua Madreva wa serikali
Ni wazee wa maadili ya vifusi,michanga,posho za safari,n.k.

Gari ikikaa MDA mref sn gereji na hujazoea maisha hayo ya kutegemea mshahara tu, month to month ni hatar sana

Njaa inauma balaa,
Hata pesa ya bia au kuhonga upati[emoji1]
 
Back
Top Bottom